Monday, June 23, 2025

TMA YASHIRIKI KATIKA MAONESHO YA KUADHIMISHA WIKI YA UTUMISHI WA UMMA 2025.

 


Dodoma, tarehe 18 Juni 2025.

 

Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imepata fursa ya kushiriki katika maonesho ya kuadhimisha wiki ya utumishi wa Umma yanayofanyika katika viwanja vya Chinangali Park, Dodoma kuanzia tarehe 16 hadi 23 Juni 2025.

 

Kupitia maonesho hayo wageni kutoka sekta mbalimbali nchini wameendelea kutembelea banda la TMA ikiwemo Waziri wa Nchi – Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene ili kujifunza masuala mbalimbali yalioandaliwa katika utoaji elimu juu ya huduma zitolewazo na TMA kwa manufaa ya jamii na maendeleo ya Taifa,

 

Kaulimbiu ya maonesho hayo ni “Kujenga Mifumo Thabiti ya Utoaji Huduma kwa Maendeleo Endelevu”.

 

No comments:

Post a Comment

Featured Post

DKT. KIJAZI: KIWANGO CHA USAHIHI WA UTABIRI WA MSIMU WA VULI 2019 KIWE CHA JUU ZAIDI.

Mkurugenzi mkuu wa TMA na Makamu wa Tatu wa Rais wa Shirika la Hali ya Hewa Duniani Dkt. Agnes Kijazi (katikati mwenye suti nyeusi) waka...