Dar es Salaam, 6 Februari 2025
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) na Makamu wa Mwenyekiti wa Jopo la Kimataifa la Sayansi ya Mabadiliko ya Hali ya Hewa na Tabianchi (IPCC) Tarehe 6 Februari 2025 alipata fursa ya kuwahamasisha na kuwajengea uwezo zaidi kuhusu sayansi ya mabadiliko ya hali ya hewa na athari zake na namna ya kukabiliana nayo kwa wataalamu wa baadhi ya taasisi zisizo za kiserikali waliokuwa wanashiriki mafunzo ya siku moja yanayohusiana utekelezaji wa miradi ya kijamii kwa kuzingatia athari za mabadiliko ya tabia nchi "Partner's Capacity Building on Climate Action Integration into Development Programming".
Mafunzo hayo yamefadhiliwa na Ubalozi wa Ireland nchini. Taasisi zilizohudhuria mafunzo haya ni pamoja na Taasisi ya Benjamin Mkapa Foundation, AMREF International, UZIKWASA na Pangani fm.
Pamoja na kuelezea shughuli na taratibu za IPCC, Dkt.Chang'a amewahamasisha washiriki wa mafunzo kushiriki kwa wingi katika maandalizi ya ripoti za IPCC katika mzunguko wa saba ulioanza Julai 2023 na utakamilika kati ya 2029 au 2030 kwa kufanya tafiti na kutoa maoni kwenye ripoti mbalimbali za IPCC, "ushiriki wako unaweza kuwa walao kuweka maoni kwenye eneo moja la ripoti za IPCC na ukawa kwenye kumbukumbu miongoni wa wataalamu waliofanikisha ripoti hizi", alisema Dkt. Chang'a.
No comments:
Post a Comment