Thursday, September 12, 2024

MHE. MWIGULU: SERIKALI ITAENDELEA KUIPA KIPAUMBELE TMA

 



12 Septemba 2024, Arusha: Waziri wa Fedha, Mhe. Mwigulu Lameck Nchemba ameipongeza Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) na kuahidi kuwa Serikali kupitia Wizara ya Fedha itaendelea kuipa kipaumbele kwa kuwa huduma za hali ya hewa zinasaidia katika mipango mbalimbali ya maendeleo.

“Wataalam wa hali ya hewa mnafanya kazi nzuri, utabiri unaotolewa hivi sasa ni wa usahihi na umesaidia sana katika masuala ya kiuchumi na kijamii na mipango ya nchi kwa ujumla”. Alizungumza Dkt. Mwigulu alipotembelea banda la TMA katika viwanja vya AICC, Arusha wakati akifunga rasmi Jukwaa la 16 la Ununuzi la Afrika Mashariki. 

Matumizi sahihi ya huduma za hali ya hewa ni suala mtambuka kwani husaidia katika mipango na uendeshaji wa shughuli za kiuchumi na kijamiii hususani katika kupunguza madhara yatokanayo na hali mbaya ya hewa kwa umma

Wednesday, September 11, 2024

TMA YASISITIZA UMUHIMU WA MATUMIZI YA HUDUMA ZA HALI YA HEWA KWA WADAU WA UNUNUZI













 10 Septemba 2024, Arusha:

Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imetoa elimu kwa wadau mbalilmbali wa Ununuzi kuhusu matumizi sahihi ya huduma za hali ya hewa pamoja na kuchangia gharama za upatikanaji wa huduma hizo katika utekelezaji wa miradi mbalimbali ya ujenzi nchini. 

Hayo yalizungumzwa na Mkurugenzi wa Huduma za Utabiri, Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA), Dkt. Hamza Kabelwa katika mada aliyoiwasilisha katika Jukwaa la 16 la Ununuzi la Afrika Mashiriki katika Ukumbi wa AICC, Arusha, linalofanyika tarehe 09 hadi 12 Sepetemba, 2024.

Dkt. Kabelwa alieleza kuwa, kiasi kikubwa cha matumizi ya fedha kinahusisha ununuzi, ni vyema huduma za hali ya hewa zikapewa kipaumbele katika utekelezaji wa Mipango ya Ununuzi na miradi mbalimbali ya maendeleo nchini ili kuongeza thamani ya fedha katika mradi. “Kwa kipindi cha hivi karibuni tumeshuhudia miradi mingi ikisimama kutokana na madhara yatokanayo na hali mbaya ya hewa, ni muda muafaka sasa wadau wanaohusika kuhakikisha wanatumia huduma hizo wakati wa ubunifu na kabla ya kuanza utekelezaji wa miradi yao”. Alisisitiza Dkt. Kabelwa.

Aidha, washiriki walijulishwa kwamba, huduma hizo mahsusi zinahitaji kuchangiwa gharama kidogo ambazo ziliwasilishwa rasmi katika hotuba ya Waziri wa Fedha ya Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa mwaka 2024/25, kifungu cha 158 ilikieleza mapendekezo ya mabadiliko ya kufanya marekebisho ya Sheria ya Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania, sura 157 kuhusu Ada za Hali ya hewa kwa usalama wa uendeshaji wa Miradi ya Ujenzi. Lengo likiwa ni kuongeza tija na ufanisi wa utendaji kazi na kuimarisha usalama wa watu na mali.

Katika hatua nyingine, wataalaam kutoka TMA kupitia maonesho yanayoendelea katika viwanja vya AICC, walieleza pia huduma za hali ya hewa zinahitaji uwekezaji wa miundombinu ya kisasa na gharama kubwa za uendeshaji ili kuwezesha utoaji wa huduma bora, hivyo ni vyema kwa wadau mbalimbali kujitokeza kutumia huduma hizo sambamba na kuchangia gharama kidogo ya huduma mahsusi.

Saturday, September 7, 2024

TMA YAWAKUMBUSHA WAHANDISI KUZINGATIA HUDUMA ZA HALI YA HEWA KATIKA UTEKELEZAJI WA MIRADI

 








06 Septemba 2024, Dar es Salaam: 

Wahandisi nchini wamekumbushwa umuhimu wa huduma za hali ya hewa sambamba na kuchangia gharama za upatikanaji wa huduma hiyo katika utekelezaji wa miradi yao. Hayo yalizungumzwa na Mkurugenzi wa Huduma za Utabiri, Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA), Dkt. Hamza Kabelwa katika mada iliyowasilishwa katika Mkutano wa  21 wa Wahandisi uliyojumuisha wahandisi wa ndani na nje ya nchi katika Ukumbi wa Mlimani City, Dar es Salaam, tarehe 05 hadi 06 Sepetemba, 2024.

Dkt. Kabelwa alieleza kuwa, katika hotuba ya Waziri wa Fedha ya Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa mwaka 2024/25, kifungu cha 158 ilijumuisha mapendekezo ya mabadiliko ya kufanya marekebisho ya sheria ya Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania, sura 157 kuhusu Ada za Hali ya hewa kwa usalama wa uendeshaji wa miradi ya ujenzi. “Lengo la hatua hiyo ni kuongeza mapato yatakayowezesha utoaji wa huduma mahsusi za hali ya hewa ili kuongeza tija na ufanisi wa utendaji kazi na kuimarisha usalama wa watu na mali katika maeneo ya miradi ya ujenzi, ambapo mchakato wa upatikanaji wa huduma hizo unahitaji uwekezaji wa miundombinu ya kisasa na gharama kubwa za uendeshaji”. Alifafanua Dkt. Kabelwa. 




Featured Post

DKT. KIJAZI: KIWANGO CHA USAHIHI WA UTABIRI WA MSIMU WA VULI 2019 KIWE CHA JUU ZAIDI.

Mkurugenzi mkuu wa TMA na Makamu wa Tatu wa Rais wa Shirika la Hali ya Hewa Duniani Dkt. Agnes Kijazi (katikati mwenye suti nyeusi) waka...