Tuesday, October 3, 2023

UFAFANUZI WA TAARIFA YA TAHADHARI INAYOSAMBAA KUHUSU UWEPO WA PACIFIC EL NINO NA ATLANTIC EL NINO.


Dodoma; Tarehe 2 Oktoba, 2023;

Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) inapenda kutoa ufafanuzi kuhusu taarifa ya tahadhari inayosambaa kuhusu uwepo wa Pacific Elnino na Atlantic El nino hatari sana na kuitaka jamii kununua jiki, water guard kwa ajili ya kuweka kwenye maji ya kunywa pamoja na masuala mengine yaliyoelezwa kwenye ujumbe huo, Aidha, ujumbe huo umekuwa ukisambaa kwenye mitandao ya kijamii na hivyo kuleta taharuki kwa wananchi.

Taarifa hiyo sio sahihi, taarifa sahihi ilitolewa tarehe 24 Agosti, 2023 kwa vyombo vya habari na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TMA Dkt. Ladislaus Chang’a na kutolewa maelekezo na viongozi mbalimbali wa nchi sambamba na kusambazwa kupitia vyanzo rasmi vya habari.

Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania inaendelea kusisitiza umma kufuatilia na kuzingatia taarifa za hali ya hewa zinazotolewa na TMA pamoja na ushauri wa kisekta unaotolewa na Taasisi zenye Mamlaka kulingana na sheria na taratibu za nchi. Aidha, ikumbukwe kuwa ni kosa kwa mujibu wa sheria Na, 2 ya mwaka 2019 ya Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania kwa mtu yeyote kutoa tahadhari ya hali mbaya ya hewa kinyume na taratibu na bila idhini ya Mamlaka. 

No comments:

Post a Comment

Featured Post

DKT. KIJAZI: KIWANGO CHA USAHIHI WA UTABIRI WA MSIMU WA VULI 2019 KIWE CHA JUU ZAIDI.

Mkurugenzi mkuu wa TMA na Makamu wa Tatu wa Rais wa Shirika la Hali ya Hewa Duniani Dkt. Agnes Kijazi (katikati mwenye suti nyeusi) waka...