Sunday, December 28, 2025

HALI YA MVUA KUBWA NCHINI

 HALI YA MVUA KUBWA NCHINI


Dar es Salaam, 28 Desemba, 2025:
Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) inapenda kutoa taarifa ya mwenendo wa Mvua Kubwa zinazoendelea kunyesha katika maeneo mbalimbali hapa nchini. 

Mnamo tarehe 26 hadi 27 Desemba, 2025 Mamlaka iliendelea kutoa Tahadhari ya vipindi vya Mvua Kubwa katika maeneo mengi nchini kuanzia tarehe 26 hadi 29 Desemba, 2025. Kwa mujibu wa Tahadhari hiyo maeneo yaliyotarajiwa kuathirika na vipindi hivi vya mvua kubwa ni pamoja na Mikoa ya Kigoma, Tabora, Katavi, Rukwa, Mbeya, Songwe, Iringa, Njombe, Dodoma, Singida, Songea, Morogoro, Lindi, Mtwara, Arusha, Manyara, Kilimanjaro, Tanga, Dar es Salaam, Pwani (ikijumisha Kisiwa cha Mafia) pamoja na Visiwa vya Unguja na Pemba. 

Kuanzia usiku wa kuamkia leo hadi hivi sasa maeneo mengi nchini yameendelea kupata vipindi vya Mvua Kubwa zikiambatana na upepo mkali na hivyo kusababisha uharibifu wa mali na miundombinu katika baadhi ya maeneo hapa nchini. Hadi kufikia saa 3:00 kamili asubuhi ya leo viwango vya mvua kubwa vinavyozidi milimita 50 ndani ya saa 24 vilipimwa katika vituo vya Same (milimita 94.5), Morogoro (milimita 58.6) na Tabora (milimita 55.4). Aidha, viwango vya mvua vilivyopimwa katika vituo vingine ni pamoja na Hombolo (milimita 49.5), Kibaha (milimita 43.6), Dodoma (milimita 36.6) na Iringa (milimita 35.6). 

Hadi muda huu tumepokea taarifa kuwa mvua hizo zimesababisha athari katika miundombinu ya reli ya zamani ya MGR kwa kuathiri madajara katika eneo la Kidete, Wilaya ya Kilosa Mkoa wa Morogoro na Gulwe Wilaya   Dodoma; kusababisha hitilafu za umeme wa TANESCO pamoja na umeme wa SGR; na pia Barabara kuu ya Morogoro - Iringa eneo la Mama Marashi - Mikumi kumetokea maporomoko ya mawe na tope kurundikana barabarani.

Mvua hizo zimesababisha miundombinu na shughuli za usafiri wa abiria na shehena kwa ujumla kuathirika, hususan kupitia Reli ya SGR.

Kwa ujumla Serikali inaendelea na juhudi za kurejesha hali hiyo katika hali yake ya kawaida. 

Mifumo ya hali ya hewa iliyopo kwa sasa inaonesha kuendelea kuimarika kwa Ukanda Mvua na hivyo kuendelea kusababisha vipindi vya Mvua Kubwa katika baadhi ya maeneo ya mikoa ya Arusha, Manyara, Kilimanjaro, Mara, Simiyu, Rukwa, Songwe, Mbeya, Iringa, Njombe, Morogoro, Ruvuma, Lindi na Mtwara kwa siku ya kesho tarehe 29 Desemba, 2025. 

USHAURI: Wananchi wanashauriwa kuendelea kufuatilia na kuzingatia taarifa za utabiri kutoka Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania pamoja na kupata ushauri na miongozo ya wataalam katika sekta husika ili kujikinga na athari zinazoweza kujitokeza.

Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) inaendelea kufuatilia mwenendo wa mifumo ya mifumo ya hali ya hewa hapa nchini na itaendelea kutoa taarifa mara kwa mara kila inapobidi.
 


Saturday, December 20, 2025

TMA YASISITIZA UMUHIMU WA KUFUATILIA NA KUZINGATIA TAARIFA ZA HALI YA HEWA

 Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania ( TMA) na Makamu Mwenyekiti wa Jopo la Kimataifa la Sayansi ya Mabadiliko ya Hali ya Hewa Duniani ( IPCC) Dkt. Ladislaus Chang'a akieleza umuhimu wa kufuatilia na kuzingatia taarifa za hali ya hewa pamoja na tahadhari za hali mbaya ya hewa wakati wa kikao cha kamati ya Wataalam ya Kitaifa ya Usimamizi wa Maafa tarehe 19 Disemba, 2025 Jijini Dodoma


Kikao hicho kiliongozwa na Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu Dkt. Jim Yonazi






Tuesday, December 16, 2025

MAFUNZO YA USIMAMIZI WA MIRADI YA MAENDELEO KWA MENEJIMENTI YA MAMLAKA YA HALI YA HEWA TANZANIA

 MAFUNZO YA USIMAMIZI WA MIRADI YA MAENDELEO KWA MENEJIMENTI YA MAMLAKA YA HALI YA HEWA TANZANIA 











Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Hali ya hewa Tanzania (TMA) na Mwakilishi wa kudumu wa Tanzania katika Shirika la Hali ya Hewa Duniani(WMO), Dkt. Ladislaus Chang'a  alifungua  mafunzo ya usimamizi wa miradi ya  maendeleo kwa menejimenti ya Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) yanayoendeshwa na Chuo Cha Uhasibu Arusha (IAA),  ambapo mafunzo hayo yamejikita zaidi  katika usimamizi wa miradi ya uwekezaji wa miundombinu kama “Capital Expenditure (CapEx)”.


 Dkt. Chang'a katika ufunguzi alisema kuwa TMA ikiwa ni Taasisi ya Serikali  iliyopewa majukumu ya kutoa huduma za hali ya hewa, kuratibu na kudhibiti shughuli zote zinazohusiana na masuala ya hali ya hewa nchini. Mamlaka inashiriki pia kutekeleza miradi mbalimbali yenye malengo yanayochangia kufanikisha utekelezaji wa majukumu ya TMA ya kitaifa, kikanda na kimataifa.


Aidha, alieleza kuwa miongoni mwa miradi ambayo inatekelezwa na TMA ni ikiwemo miradi ya uwekezaji wa miundombinu mbalimbali “Capital Expenditure (CapEx)”, Ujenzi wa Kituo cha Ufuatiliaji wa matukio ya Tsunami (Tsunami Centre), TMA inapata ufadhili wa kujenga vituo vipya vitatu (3) vya kupima hali ya hewa katika anga za juu kupitia mradi wa (SOFF) na nyinginezo nyingi. 


Kwa upande wake Mtiva wa Kitivo cha Mafunzo ya Insia na Sayansi za Jamii, Dkt. Leticia Rwabishungi wa chuo Cha Uhasibu Arusha aliwashukuru sana  TMA kwa kufika  IAA kwa mafunzo  ya usimamizi wa miradi na kusema chuo kina kozi nyingi sio tu Uhasibu bali kozi mbalimbali na kwa ngazi zote hivyo aliwakaribisha kuendelea kupata mafunzo katika chuo cha IAA.


Mojawapo ya walioshiriki katika ufunguzi wa mafunzo hayo ni  Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania, Mkurugenzi wa Huduma za Ushauri wa Chuo cha IAA,  Menejimenti ya Mamlaka ya Hali ya Hewa, Wakufunzi kutoka Chuo cha IAA, Wataalamu mbalimbali kutoka TMA, IAA na UNDP.


Mafunzo haya yameanza Disemba 15 mpka 19, mwaka 2025.

TMA YAPONGEZWA KWA KUIMARISHA IMANI YA WATANZANIA KUPITIA TAARIFA SAHIHI ZA HALI YA HEWA





Arusha 15 Disemba 2025,

Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) ilipata fursa adhimu ya kutembelewa na Naibu Waziri wa Uchukuzi, Mheshimiwa David Kihenzile(MB), katika Mkutano Mkuu wa 18 wa Tathmini ya Utendaji wa Sekta ya Uchukuzi. Mkutano huo ulifanyika katika Ukumbi wa AICC, Jijini Arusha.

Katika mkutano huo, Mheshimiwa Naibu Waziri aliipongeza Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania kwa mchango wake mkubwa katika utoaji wa taarifa sahihi na za kuaminika za hali ya hewa, ambazo zimeendelea kusaidia kuboresha usalama na ufanisi katika sekta ya uchukuzi na kuwa taasisi yenye kuaminiwa na Watanzania.

Mkutano huo unafanyika kwa muda wa siku tatu, kuanzia tarehe 15 - 17 Desemba 2025 na kuwakutanisha wadau mbalimbali wa sekta ya uchukuzi.

Friday, November 28, 2025

HALI YA JOTO KALI NCHINI

 


Dar es Salaam, 28 Novemba, 2025:

Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) inapenda kutoa taarifa ya hali la joto katika maeneo mbalimbali nchini. 

Kumekuwepo na ongezeko la Joto katika baadhi ya maeneo hapa nchini hususan yale yanayopata misimu miwili ya mvua kwa mwaka kwa miezi ya hivi karibuni. Hali hii imesababishwa na kusogea kwa Jua la Utosisambamba na upungufu wa mvua unaojitokeza katika maeneo hayo. Kwa kawaida vipindi vya Jua la Utosi nchini hufikia kilele mwishoni mwa mwezi Novemba wakati Jua la Utosi likiwa linaelekea kusini (Tropiki ya Kaprikoni) na hali hiyo hujirudia tena mwezi Februari wakati Jua la Utosi likiwa linaelekea kaskazini (Tropiki ya Kansa). Jua la Utosi huambatana na hali ya ongezeko la Joto kwa sababu uso wa Dunia katika eneo tajwa huwa karibu zaidi na Jua kuliko maeneo mengine. 

Katika kipindi cha mwezi Novemba2025 hali ya ongezeko la Joto imeendelea kujitokeza katika baadhi ya maeneo nchini, ambapo hadi kufikia tarehe 27 Novemba2025 kituo cha hali ya hewa cha Moshi (Kilimanjaro)kiliripoti kiwango cha juu zaidi cha nyuzi joto 35.7°C mnamo tarehe 21 Novemba, 2025 ikiwa ni ongezeko la nyuzi joto 4.2°C ukilinganisha na wastani wa muda mrefu kwa mwezi Novemba katika kituo hicho. Kituo cha hali ya hewa cha Ilonga (Morogoro) kiliripoti nyuzi joto 35.5°C mnamo tarehe 20 Novemba (ongezeko la nyuzi joto 2.7°C). Kituo cha hali ya hewa Morogoro kiliripoti nyuzi joto 34.5°C mnamo tarehe 26 Novemba (ongezeko la nyuzi joto 2.3°C). Kituo cha Ibadakuli (Shinyanga) kiliripoti nyuzi joto 33.6°C mnamo tarehe 14 Novemba (ongezeko la nyuzi joto 2.2°C), na Dar es salaam nyuzi joto 33.2 °Cmnamo tarehe 19 na 21 Novemba (ongezeko la nyuzi joto 1.6°C).

Aidha, ongezeko la unyevu angani (Relative humidity) katika kipindi hiki linalosababishwa na mvuke wa Bahari hususan katika maeneo ya ukanda wa pwani na maeneo jirani limechangia pia mwili kuhisi joto zaidi ya viwango vinavyoripotiwa.

Hata hivyo, katika kipindi cha mwezi Desemba, 2025vipindi vya mvua vinatarajiwa kujitokeza katika maeneo mengi nchini. Hali hii inatarajiwa kusababisha kupungua kwa Joto katika baadhi ya maeneo hususan yanayopata misimu miwili ya mvua kwa mwaka.

Kwa taarifa hii wananchi wanashauriwa kuendelea kuzingatia taarifa na tahadhari za hali mbaya ya hewa zinazotolewa na Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania sambamba na kutafuta, kupata na kufuata ushauri wa wataalam katika sekta husika ili kupunguza athari zinazotokana na hali mbaya ya hewa.

Monday, November 17, 2025

TANZANIA YAIMARISHA UWEZO WA BURUNDI KATIKA USIMAMIZI WA UBORA WA HUDUMA ZA HALI YA HEWA



30 Oktoba, 2025: Bunjumbura, Burundi

Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA), ikishirikiana na Shirika la Hali ya Hewa Duniani (WMO) na Taasisi ya Hali ya Hewa ya Burundi (IGEBU), ilifanikiwa kufanya mafunzo ya kujenga uwezo wa Mfumo wa Udhibiti wa Ubora (QMS) kwa wafanyakazi zaidi ya arobaini (40) wa IGEBU, mjini Bujumbura, Burundi, kuanzia tarehe 13 hadi 30 Oktoba 2025. Mafunzo hayo yalitolewa na wataalamu wa TMA kupitia mfumo wa ushirikiano wa kimataifa wa huduma za hali ya hewa katika ukanda wa Afrika Mashariki.

Kupitia mpango wa WMO wa Athari za Hali ya Hewa na Mifumo ya Tahadhari ya Mapema Afrika Mashariki (CREWS), mafunzo hayo yalilenga kujenga uwezo wa kitaasisi wa IGEBU ili kuoanisha mifumo yake kwa kiwango cha udhibiti ubora cha ISO 9001:2015. Wataalamu wa QMS kutoka TMA, walitoa mafunzo endelevu kwa wafanyakazi wa IGEBU, kuwaongoza kupitia  ukaguzi wa ndani na mipango ya usimamizi.

Akizungumza wakati wa kufunga mafunzo hayo katika ukumbi wa Chandelier, Bujumbura, Burundi, Mkurugenzi wa Ofisi ya WMO Kanda ya Afrika, Dkt. Agnes Kijazi alipongeza dhamira ya IGEBU na mchango wa Tanzania katika kujenga uwezo wa kikanda.

"Dhamira hii ni ushuhuda wa kile kinachoweza kupatikana kupitia ushirikiano kwa kuwekeza katika mifumo bora, kuimarisha imani katika huduma za hali ya hewa, msingi wa ustahimilivu na maendeleo endelevu." Alisema, Dkt Kijazi.

Katika hatua nyingine, Mkurugenzi wa Taasisi ya Hali ya Hewa ya Burundi (IGEBU), Bw. Deogratius Babonwanayo, alitoa shukrani kwa mafunzo yaliyotolewa na kuthibitisha dhamira ya IGEBU ya kuelekea kwenye Mfumo wa Udhibiti Ubora (QMS). 

Naye Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanania (TMA) na Makamu Mwenyekiti wa Jopo la Kimataifa la Mabadiliko ya Sayansi ya Hali ya Hewa na Tabianchi (IPCC), Dkt. Ladislaus Chang’a alishiriki kwa njia ya mtandao, akithibitisha kuendelea kujitolea kwa TMA katika maendeleo ya kikanda kupitia ushirikiano na kubadilishana ujuzi.

Mafunzo ya QMS yalilenga kuimarisha mifumo ya ndani ya IGEBU na kuimarisha mshikamano wa kikanda katika kutoa huduma za hali ya hewa zenye ubora. Juhudi hizo zinaletwa na msukumo wa kimataifa wa WMO ili kuhakikisha nchi zote zinaweza kutoa taarifa za hali ya hewa zenye ubora kwa wakati, zitakazoaminika na zinazoweza kutekelezeka kwa ajili ya kufanya maamuzi sahihi katika shughuli zote za kijamii na kiuchumi na kulinda maisha ya watu na mali zao.

Friday, November 14, 2025

Tanzania Strengthens Burundi’s Path Toward Quality Management in Meteorological Services: Tanzania–Burundi Partnership in Action

 













30 October 2025, Bujumbura, Burundi

The Tanzania Meteorological Authority (TMA), in close collaboration with the World Meteorological Organization (WMO) and the Institut Géographique du Burundi (IGEBU), successfully concluded a Quality Management System (QMS) capacity-building mission in Bujumbura, Burundi, from 13 to 30 October 2025. This technical assistance, delivered by TMA experts through a South–South cooperation framework, reflects Tanzania’s leadership in advancing operational excellence in meteorological services across East Africa.

Implemented through the WMO Climate Risk and Early Warning Systems (CREWS) East Africa initiative, the mission focused on building the institutional and human capacity of IGEBU to align its processes with the ISO 9001:2015 QMS standard. The TMA delegation, composed of QMS experts Mr. Geofrid Chikojo and Mr. Danford Nyenyema, provided sustained on-the-ground mentorship to IGEBU staff, guiding them through training sessions, internal audit simulations, and management planning.

The closing ceremony, held at Le Chandelier in Bujumbura, was graced by Dr. Agnes Kijazi, Director of the WMO Regional Office for Africa, who praised both IGEBU’s commitment and Tanzania’s contribution to regional capacity-building.

She remarked, “This mission is a powerful testament to what can be achieved through South–South collaboration. By investing in quality systems, we are strengthening trust in our climate and weather services, the cornerstone of resilience and sustainable development.”

In her address, Dr. Kijazi also acknowledged the instrumental role of TMA in supporting peer institutions in the region, noting that such technical missions promote long-term sustainability, standardization, and shared excellence across African National Meteorological and Hydrological Services (NMHSs).

The event was also attended by the Permanent Representative of Burundi with WMO Mr Deogratius Babonwanayo, who expressed appreciation for the support received and reaffirmed IGEBU’s commitment to moving toward QMS certification. The Permanent Representative of Tanzania with WMO and IPCC Vice Chair, Dr. Ladislaus Chang’a participated virtually, reaffirming TMA’s dedication to regional advancement through cooperation and knowledge exchange.

Throughout the mission, IGEBU established a dedicated internal audit team, conducted its first management review meeting, and mobilized over 40 staff members in practical training activities. A comprehensive internal audit simulation was successfully implemented, and a tailored roadmap for ISO 9001:2015 certification was developed.

This QMS mission not only strengthened IGEBU’s internal systems but also reinforced regional solidarity in delivering high-quality, user-oriented meteorological and climate services. The effort aligns with WMO’s global push to ensure that all countries can deliver quality, reliable, timely, and actionable weather and climate information and products  for informed decision making in all socio-economic activities and for protection of life and properties amid growing climate risks.

Monday, October 27, 2025

MWENENDO WA KIMBUNGA “CHENGE” KATIKA ENEO KUSINI MASHARIKI MWA BAHARI YA HINDI

 

Dar es Salaam, 27 Oktoba, 2025 Usiku:

Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) inaendelea kutoa taarifa ya mwenendo wa kilichokuwa Kimbunga “CHENGE” katika katika maeneo ya pwani ya nchi yetu.

 

Kimbunga “CHENGE” kimepoteza nguvu yake na kusambaratika kabisa wakati kikikaribia ukanda wa pwani ya nchi yetu. Hata hivyo, mvua na mawingu yaliyokuwa yakiambatana na kimbunga hicho yamesambaa katika maeneo ya ukanda wa pwani hususan katika mikoa ya Lindi, Pwani, Dar es salaam na Tanga pamoja na visiwa vya Unguja na Pemba na kusababisha vipindi vya mvua katika baadhi ya maeneo hayo. Kwa mfano hadi kufika saa 12 jioni ya leo, kituo cha hali ya hewa kilichopo uwanja wa ndege wa Julius Nyerere Dar es salaam kimeripoti mvua ya milimita 9.1 kwa kipindi cha saa 9 zilizopita. Vilevile katika kipindi hicho, kituo cha hali ya hewa kilichopo katika bandari ya Dar es Salaam kimeripoti mvua ya milimita 3.5.

 

Uchambuzi wa mifumo ya hali ya hewa unaonesha kuwa mabaki ya Kimbunga hicho yanatarajiwa kuendelea kusababisha vipindi vichache vya mvua kwa usiku wa leo tarehe 27 na siku ya kesho 28 ya Mwezi Oktoba, 2025 kwa maeneo ya mikoa ya Pwani, Dar es salaam na Tanga pamoja na visiwa vya Unguja na Pemba na maeneo jirani. Hata hivyo, hakuna madhara makubwa yanayotarajiwa.

 

Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) inaendelea kufuatilia mwenendo wa mabaki ya kimbunga “CHENGE” na athari zake kwa mifumo ya hali ya hewa hapa nchini na itaendelea kutoa taarifa kila inapobidi.

 

USHAURI: Watumiaji wa Bahari na wananchi kwa ujumla wanashauriwa kuendelea kufuatilia na kuzingatia taarifa za utabiri kutoka Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania pamoja na kupata ushauri na miongozo ya wataalam wa kisekta.

Saturday, October 25, 2025

MWENENDO WA KIMBUNGA “CHENGE” KATIKA ENEO LA KUSINI MAGHARIBI MWA BAHARI YA HINDI

 


Dar es Salaam, 25 Oktoba, 2025 Mchana:

Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) inaendelea kutoataarifa ya mwenendo wa Kimbunga “CHENGE katika Bahari ya Hindi, Kaskazini mwa Kisiwa cha Madagascar

 

Kimbunga “CHENGE” kimeendelea kusalia baharini nakusogea kuelekea magharibihuku kikipungua nguvu yake. Hadi asubuhi ya leo kilikuwa katika eneo la Bahari umbali watakribani kilometa 1,280 Mashariki mwa pwani ya kisiwa cha Mafia.

 

Uchambuzi wa mifumo ya hali ya hewa unaonesha kuwaKimbunga hicho kinatarajiwa kuendelea kusogea kuelekeaMagharibi zaidi mwa Bahari ya Hindi ulipo ukanda wa pwaniwa nchi yetu huku kikiendelea kupungua nguvu yake kadrikinavyosogeaHali hiyo inatarajiwa kusababisha uwezekanomdogo wa ongezeko kidogo la kasi ya upepo na mawimbimakubwa ya Bahari kati ya tarehe 26 hadi 28 ya Mwezi Oktoba, 2025 kwa maeneo ya ukanda wa pwani ya nchi yetuVilevileupo uwezekano mdogo wa vipindi vichache vya mvua kubwa kujitokeza hususani katika maeneo ya visiwa vyaUnguja na Pemba pamoja na mikoa ya Morogoro, Pwani, Dar es salaam na Tanga na maeneo jirani katika kipindi hicho cha tarehe 26 na 28 ya Mwezi Oktoba 2025.

 

Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) inaendeleakufuatilia mwenendo wa kimbunga CHENGE na athari zakekwa mifumo ya hali ya hewa hapa nchini na itaendelea kutoataarifa kila inapobidi.

 

USHAURI: Watumiaji wa Bahari na wananchi kwa ujumlawanashauriwa kuendelea kufuatilia na kuzingatia taarifa za utabiri kutoka Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania pamoja na kupata ushauri na miongozo ya wataalam wakisekta.

Featured Post

DKT. KIJAZI: KIWANGO CHA USAHIHI WA UTABIRI WA MSIMU WA VULI 2019 KIWE CHA JUU ZAIDI.

Mkurugenzi mkuu wa TMA na Makamu wa Tatu wa Rais wa Shirika la Hali ya Hewa Duniani Dkt. Agnes Kijazi (katikati mwenye suti nyeusi) waka...