Monday, November 17, 2025

TANZANIA YAIMARISHA UWEZO WA BURUNDI KATIKA USIMAMIZI WA UBORA WA HUDUMA ZA HALI YA HEWA



30 Oktoba, 2025: Bunjumbura, Burundi

Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA), ikishirikiana na Shirika la Hali ya Hewa Duniani (WMO) na Taasisi ya Hali ya Hewa ya Burundi (IGEBU), ilifanikiwa kufanya mafunzo ya kujenga uwezo wa Mfumo wa Udhibiti wa Ubora (QMS) kwa wafanyakazi zaidi ya arobaini (40) wa IGEBU, mjini Bujumbura, Burundi, kuanzia tarehe 13 hadi 30 Oktoba 2025. Mafunzo hayo yalitolewa na wataalamu wa TMA kupitia mfumo wa ushirikiano wa kimataifa wa huduma za hali ya hewa katika ukanda wa Afrika Mashariki.

Kupitia mpango wa WMO wa Athari za Hali ya Hewa na Mifumo ya Tahadhari ya Mapema Afrika Mashariki (CREWS), mafunzo hayo yalilenga kujenga uwezo wa kitaasisi wa IGEBU ili kuoanisha mifumo yake kwa kiwango cha udhibiti ubora cha ISO 9001:2015. Wataalamu wa QMS kutoka TMA, walitoa mafunzo endelevu kwa wafanyakazi wa IGEBU, kuwaongoza kupitia  ukaguzi wa ndani na mipango ya usimamizi.

Akizungumza wakati wa kufunga mafunzo hayo katika ukumbi wa Chandelier, Bujumbura, Burundi, Mkurugenzi wa Ofisi ya WMO Kanda ya Afrika, Dkt. Agnes Kijazi alipongeza dhamira ya IGEBU na mchango wa Tanzania katika kujenga uwezo wa kikanda.

"Dhamira hii ni ushuhuda wa kile kinachoweza kupatikana kupitia ushirikiano kwa kuwekeza katika mifumo bora, kuimarisha imani katika huduma za hali ya hewa, msingi wa ustahimilivu na maendeleo endelevu." Alisema, Dkt Kijazi.

Katika hatua nyingine, Mkurugenzi wa Taasisi ya Hali ya Hewa ya Burundi (IGEBU), Bw. Deogratius Babonwanayo, alitoa shukrani kwa mafunzo yaliyotolewa na kuthibitisha dhamira ya IGEBU ya kuelekea kwenye Mfumo wa Udhibiti Ubora (QMS). 

Naye Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanania (TMA) na Makamu Mwenyekiti wa Jopo la Kimataifa la Mabadiliko ya Sayansi ya Hali ya Hewa na Tabianchi (IPCC), Dkt. Ladislaus Chang’a alishiriki kwa njia ya mtandao, akithibitisha kuendelea kujitolea kwa TMA katika maendeleo ya kikanda kupitia ushirikiano na kubadilishana ujuzi.

Mafunzo ya QMS yalilenga kuimarisha mifumo ya ndani ya IGEBU na kuimarisha mshikamano wa kikanda katika kutoa huduma za hali ya hewa zenye ubora. Juhudi hizo zinaletwa na msukumo wa kimataifa wa WMO ili kuhakikisha nchi zote zinaweza kutoa taarifa za hali ya hewa zenye ubora kwa wakati, zitakazoaminika na zinazoweza kutekelezeka kwa ajili ya kufanya maamuzi sahihi katika shughuli zote za kijamii na kiuchumi na kulinda maisha ya watu na mali zao.

Friday, November 14, 2025

Tanzania Strengthens Burundi’s Path Toward Quality Management in Meteorological Services: Tanzania–Burundi Partnership in Action

 













30 October 2025, Bujumbura, Burundi

The Tanzania Meteorological Authority (TMA), in close collaboration with the World Meteorological Organization (WMO) and the Institut Géographique du Burundi (IGEBU), successfully concluded a Quality Management System (QMS) capacity-building mission in Bujumbura, Burundi, from 13 to 30 October 2025. This technical assistance, delivered by TMA experts through a South–South cooperation framework, reflects Tanzania’s leadership in advancing operational excellence in meteorological services across East Africa.

Implemented through the WMO Climate Risk and Early Warning Systems (CREWS) East Africa initiative, the mission focused on building the institutional and human capacity of IGEBU to align its processes with the ISO 9001:2015 QMS standard. The TMA delegation, composed of QMS experts Mr. Geofrid Chikojo and Mr. Danford Nyenyema, provided sustained on-the-ground mentorship to IGEBU staff, guiding them through training sessions, internal audit simulations, and management planning.

The closing ceremony, held at Le Chandelier in Bujumbura, was graced by Dr. Agnes Kijazi, Director of the WMO Regional Office for Africa, who praised both IGEBU’s commitment and Tanzania’s contribution to regional capacity-building.

She remarked, “This mission is a powerful testament to what can be achieved through South–South collaboration. By investing in quality systems, we are strengthening trust in our climate and weather services, the cornerstone of resilience and sustainable development.”

In her address, Dr. Kijazi also acknowledged the instrumental role of TMA in supporting peer institutions in the region, noting that such technical missions promote long-term sustainability, standardization, and shared excellence across African National Meteorological and Hydrological Services (NMHSs).

The event was also attended by the Permanent Representative of Burundi with WMO Mr Deogratius Babonwanayo, who expressed appreciation for the support received and reaffirmed IGEBU’s commitment to moving toward QMS certification. The Permanent Representative of Tanzania with WMO and IPCC Vice Chair, Dr. Ladislaus Chang’a participated virtually, reaffirming TMA’s dedication to regional advancement through cooperation and knowledge exchange.

Throughout the mission, IGEBU established a dedicated internal audit team, conducted its first management review meeting, and mobilized over 40 staff members in practical training activities. A comprehensive internal audit simulation was successfully implemented, and a tailored roadmap for ISO 9001:2015 certification was developed.

This QMS mission not only strengthened IGEBU’s internal systems but also reinforced regional solidarity in delivering high-quality, user-oriented meteorological and climate services. The effort aligns with WMO’s global push to ensure that all countries can deliver quality, reliable, timely, and actionable weather and climate information and products  for informed decision making in all socio-economic activities and for protection of life and properties amid growing climate risks.

Monday, October 27, 2025

MWENENDO WA KIMBUNGA “CHENGE” KATIKA ENEO KUSINI MASHARIKI MWA BAHARI YA HINDI

 

Dar es Salaam, 27 Oktoba, 2025 Usiku:

Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) inaendelea kutoa taarifa ya mwenendo wa kilichokuwa Kimbunga “CHENGE” katika katika maeneo ya pwani ya nchi yetu.

 

Kimbunga “CHENGE” kimepoteza nguvu yake na kusambaratika kabisa wakati kikikaribia ukanda wa pwani ya nchi yetu. Hata hivyo, mvua na mawingu yaliyokuwa yakiambatana na kimbunga hicho yamesambaa katika maeneo ya ukanda wa pwani hususan katika mikoa ya Lindi, Pwani, Dar es salaam na Tanga pamoja na visiwa vya Unguja na Pemba na kusababisha vipindi vya mvua katika baadhi ya maeneo hayo. Kwa mfano hadi kufika saa 12 jioni ya leo, kituo cha hali ya hewa kilichopo uwanja wa ndege wa Julius Nyerere Dar es salaam kimeripoti mvua ya milimita 9.1 kwa kipindi cha saa 9 zilizopita. Vilevile katika kipindi hicho, kituo cha hali ya hewa kilichopo katika bandari ya Dar es Salaam kimeripoti mvua ya milimita 3.5.

 

Uchambuzi wa mifumo ya hali ya hewa unaonesha kuwa mabaki ya Kimbunga hicho yanatarajiwa kuendelea kusababisha vipindi vichache vya mvua kwa usiku wa leo tarehe 27 na siku ya kesho 28 ya Mwezi Oktoba, 2025 kwa maeneo ya mikoa ya Pwani, Dar es salaam na Tanga pamoja na visiwa vya Unguja na Pemba na maeneo jirani. Hata hivyo, hakuna madhara makubwa yanayotarajiwa.

 

Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) inaendelea kufuatilia mwenendo wa mabaki ya kimbunga “CHENGE” na athari zake kwa mifumo ya hali ya hewa hapa nchini na itaendelea kutoa taarifa kila inapobidi.

 

USHAURI: Watumiaji wa Bahari na wananchi kwa ujumla wanashauriwa kuendelea kufuatilia na kuzingatia taarifa za utabiri kutoka Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania pamoja na kupata ushauri na miongozo ya wataalam wa kisekta.

Saturday, October 25, 2025

MWENENDO WA KIMBUNGA “CHENGE” KATIKA ENEO LA KUSINI MAGHARIBI MWA BAHARI YA HINDI

 


Dar es Salaam, 25 Oktoba, 2025 Mchana:

Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) inaendelea kutoataarifa ya mwenendo wa Kimbunga “CHENGE katika Bahari ya Hindi, Kaskazini mwa Kisiwa cha Madagascar

 

Kimbunga “CHENGE” kimeendelea kusalia baharini nakusogea kuelekea magharibihuku kikipungua nguvu yake. Hadi asubuhi ya leo kilikuwa katika eneo la Bahari umbali watakribani kilometa 1,280 Mashariki mwa pwani ya kisiwa cha Mafia.

 

Uchambuzi wa mifumo ya hali ya hewa unaonesha kuwaKimbunga hicho kinatarajiwa kuendelea kusogea kuelekeaMagharibi zaidi mwa Bahari ya Hindi ulipo ukanda wa pwaniwa nchi yetu huku kikiendelea kupungua nguvu yake kadrikinavyosogeaHali hiyo inatarajiwa kusababisha uwezekanomdogo wa ongezeko kidogo la kasi ya upepo na mawimbimakubwa ya Bahari kati ya tarehe 26 hadi 28 ya Mwezi Oktoba, 2025 kwa maeneo ya ukanda wa pwani ya nchi yetuVilevileupo uwezekano mdogo wa vipindi vichache vya mvua kubwa kujitokeza hususani katika maeneo ya visiwa vyaUnguja na Pemba pamoja na mikoa ya Morogoro, Pwani, Dar es salaam na Tanga na maeneo jirani katika kipindi hicho cha tarehe 26 na 28 ya Mwezi Oktoba 2025.

 

Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) inaendeleakufuatilia mwenendo wa kimbunga CHENGE na athari zakekwa mifumo ya hali ya hewa hapa nchini na itaendelea kutoataarifa kila inapobidi.

 

USHAURI: Watumiaji wa Bahari na wananchi kwa ujumlawanashauriwa kuendelea kufuatilia na kuzingatia taarifa za utabiri kutoka Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania pamoja na kupata ushauri na miongozo ya wataalam wakisekta.

Friday, October 24, 2025

MWENENDO WA KIMBUNGA “CHENGE” KATIKA ENEO LA KUSINI MAGHARIBI MWA BAHARI YA HINDI

 


Dar es Salaam, 24 Oktoba, 2025 Mchana:

Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) inaendelea kutoa taarifa ya mwenendo wa Kimbunga “CHENGE” katika Bahari ya Hindi, Kaskazini Mashariki mwa Kisiwa cha Madagascar.

 

Kimbunga “CHENGE” kimeendelea kusalia baharini na kusogea kuelekea Magharibi, yaani kuelekea pwani ya nchi yetu. Hadi kufikia asubuhi ya leo Kimbunga “CHENGE” kilikuwa katika eneo la Bahari ya Hindi umbali wa takribani kilometa 1,680 Mashariki mwa pwani ya Mtwara.

 

Uchambuzi wa mifumo ya hali ya hewa inaonesha kuwa Kimbunga hicho kinatarajiwa kuendelea kusogea kuelekea Magharibi zaidi mwa Bahari ya Hindi ulipo ukanda wa pwani wa nchi yetu huku kikipungua nguvu yake kadri kinavyosogea. Hali hiyo inatarajiwa kusababisha uwezekano mdogo wa vipindi vya ongezeko la mvua, upepo na mawimbi makubwa ya Bahari kati ya tarehe 26 hadi 28 ya Mwezi Oktoba, 2025 hususan kwa maeneo ya mikoa ya Mtwara, Lindi, Pwani, Dar es salaam na Tanga pamoja na visiwa vya Unguja na Pemba.

 

Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) inaendelea kufuatilia mwenendo wa kimbunga “CHENGE” na athari zake kwa mifumo ya hali ya hewa hapa nchini na itaendelea kutoa taarifa kila inapobidi.

 

USHAURI: Watumiaji wa Bahari na wananchi kwa ujumla wanashauriwa kuendelea kufuatilia na kuzingatia taarifa za utabiri kutoka Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania pamoja na kupata ushauri na miongozo ya wataalam wa kisekta.

Wednesday, October 22, 2025

UWEPO NA MWENENDO WA KIMBUNGA “CHENGE” KATIKA ENEO LA KUSINI MAGHARIBI MWA BAHARI YA HINDI

 

Dar es Salaam, 22 Oktoba, 2025:

Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) inatoa taarifa ya uwepo na mwenendo wa Kimbunga “CHENGE” katika Bahari ya Hindi, Kaskazini Mashariki mwa Kisiwa cha Madagascar umbali wa takribani kilometa 2400 kutoka Mashariki mwa pwani ya Mtwara.

 

Kimbunga “CHENGE” kilianza kujitengeneza Mashariki mwa Bahari ya Hindi mnamo tarehe 17 Oktoba, 2025 na kiliendelea kusalia katika eneo hilo huku kikiimarika.

 

Uchambuzi wa mifumo ya hali ya hewa kwa sasa inaonesha kuwa Kimbunga “CHENGE” kinatarajiwa kuelekea Magharibi zaidi mwa Bahari ya Hindi ulipo ukanda wa pwani ya nchi yetu katika kipindi cha siku nne hadi tano zijazo (kati ya tarehe 26 hadi 27 ya Mwezi Oktoba, 2025), huku kikipungua nguvu yake.

 

Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) inaendelea kufuatilia mwenendo wa kimbunga “CHENGE” na athari zake kwa mifumo ya hali ya hewa hapa nchini na itaendelea kutoa taarifa kila inapobidi.

 

USHAURI: Watumiaji wa bahari na wananchi kwa ujumla wanashauriwa kuendelea kufuatilia na kuzingatia taarifa za utabiri kutoka Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania pamoja na kupata ushauri na miongozo ya wataalam wa kisekta.

Friday, October 17, 2025

UTABIRI WA MVUA ZA MSIMU NOVEMBA 2025 HADI APRILI 2026 WATOLEWA RASMI


 Dar es Salaam, Tarehe 17 Oktoba, 2025

Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imetoa rasmi utabiri wa mvua za msimu kwa maeneo yanayopata mvua mara moja kwa mwaka. Maeneo hayo ni mikoa ya Kigoma, Katavi, Singida, Dodoma, Rukwa, Songwe, Mbeya, Iringa, Njombe, Lindi, Mtwara, Ruvuma na Kusini mwa Morogoro katika kipindi cha miezi ya Novemba, 2025 hadi Aprili, 2026.

Akitoa utabiri huo kwa vyombo mbalimbali vya habari katika ukumbi wa Ubungo Plaza, Kaimu Mkurugenzi Mkuu, TMA na Makamu Mwenyekiti wa Jopo la Kimataifa la Sayansi ya Mabadiliko ya Hali ya Hewa na Tabianchi (IPCC), Dkt. Ladislaus Chang’a alisema Mvua za Chini ya Wastani hadi Wastani zinatarajiwa katika mikoa ya Kigoma, Tabora, Katavi, Singida na Dodoma. Aidha, mvua za Wastani hadi Chini ya Wastani zinatarajiwa katika mikoa ya Njombe, Iringa, Mbeya, Songwe, Rukwa, Ruvuma, Mtwara na Lindi pamoja na kusini mwa mkoa wa Morogoro.


Mvua zinatarajiwa kuanza kati ya wiki ya tatu na ya nne ya mwezi Oktoba, 2025 katika mikoa ya Tabora, Katavi na Kigoma; na kusambaa katika mikoa ya Rukwa, Songwe, Mbeya, Iringa, Njombe pamoja na kusini mwa mkoa wa Morogoro kati ya wiki ya pili na ya tatu ya mwezi Novemba, 2025 na zinatarajiwa kuisha kati ya wiki ya nne ya mwezi Aprili na wiki ya kwanza ya mwezi Mei 2026 katika maeneo mengi” Alifafanua Dkt. Chang’a.


“Msimu unatarajiwa kutawaliwa na vipindi virefu vya ukavu na mtawanyiko wa mvua usioridhisha katika maeneo mengi japo Kipindi cha nusu ya pili ya msimu (Februari – Aprili, 2026) kinatarajiwa kuwa na ongezeko la mvua ikilinganishwa na nusu ya kwanza (Novemba, 2025 – Januari, 2026). Aliongezea Dkt. Chang’a.

Akieleza athari zinazoweza kujitokeza, Dkt. Chang’a alisema Mvua za Chini ya Wastani zinazotarajiwa katika maeneo mengi zinaweza zikasababisha upungufu wa unyevu wa udongo, jambo ambalo linaweza kuathiri ukuaji na maendeleo ya mazao na kupunguza mavuno hususani kwa mazao yanayotegemea mvua. Aidha, kupungua kwa kina cha maji kwenye mabwawa na mtiririko wa maji kwenye mito kunaweza kutokea, hali ambayo inaweza kupunguza upatikanaji wa maji kwa matumizi mbalimbali huku upatikanaji wa maji na malisho kwa ajili ya mifugo ukitarajiwa kuathirika.

Kwa maelezo kamili kuhusu utabiri huu tembelea; www.meteo.go.tz 

Thursday, October 16, 2025

JAJI MSHIBE AWATAKA WASHINDI WA TUZO ZA HABARI ZA HALI YA HEWA 2025 KUTORUDI NYUMA

 






















Dar es Salaam, tarehe 16 Oktoba 2025.

 

“Washindi wote mliopata tuzo za habari za hali ya hewa 2025 nawasihi msibweteke sababu nimeona washindi wengi waliopata TUZO mwaka jana hawapo mwaka huu, inapaswa ikiwa umepata tuzo mwaka huu basi mwaka unaofuata ufanye vizuri zaidi” Alizungumza hayo Mwenyekiti wa Bodi ya Mamlaka ya Hali ya hewa Tanzania (TMA) na mgeni rasmi katika hafla ya utoaji TUZO za wanahabari bora wa habari za hali ya hewa kwa mwaka  2025 iliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT), Dar es Salaam, tarehe  16 Oktoba 2025.

 

Jaji Mshibe alianza kwa zoezi la kukabidhi Tuzo hizo za Wanahabari bora, ambapo mshindi upande wa Luninga na Redio alikuwa ni Lisungu Kambona kutoka ZCTV, mshindi upande wa Magazetini alikuwa ni Penina Malundo kutoka gazeti la Majira, mshindi kutoka Zanzibar tuzo ilichukuliwa na Amour Khamis Ali kutoka Assalam FM, mshindi upande wa Mitandao ya Kijamii alikuwa ni Juma Issihaka kutoka Mwananchi Digital.

 

Jaji Mshibe aliongezea, kwa kuwataka waandishi wa habari kuendelea kutoa taarifa za hali ya hewa zenye uhakika na kwa weledi mkubwa huku akiwapongeza TMA kwa kuendelea na kuimarisha utoaji wa TUZO zinazoleta motisha kwa waandishi wa habari katika kuhabarisha na kuelimisha jamii kuhusu taarifa za hali ya hewa nchini.

 

Aidha, hafla hiyo ya tuzo ambayo n ya  sita tangu kuanzishwa kwake mwaka 2019, ilitanguliwa na warsha ya  wanahabari kuhusu mwelekeo wa mvua za msimu unaoanzia mwezi Novemba 2025 hadi Aprili 2026. Mamlaka inatarajia kutoa rasmi utabiri huo tarehe 17 Oktoba 2025, Ubungo Plaza.


Featured Post

DKT. KIJAZI: KIWANGO CHA USAHIHI WA UTABIRI WA MSIMU WA VULI 2019 KIWE CHA JUU ZAIDI.

Mkurugenzi mkuu wa TMA na Makamu wa Tatu wa Rais wa Shirika la Hali ya Hewa Duniani Dkt. Agnes Kijazi (katikati mwenye suti nyeusi) waka...