Wednesday, July 23, 2025

BODI YA TMA YAFANYA ZIARA YA KIKAZI RADA YA HALI YA HEWA BANGULO, PUGU NA KITUO CHA HALI YA HEWA JNIA














Dar es Salaam; Tarehe 23 Julai, 2025;

Bodi ya Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imefanya ziara ya kikazi ya kukagua utendaji kazi wa Mamlaka katika kituo cha Rada ya Hali ya Hewa, Bangulo, Pugu na Ofisi za TMA zilizopo katika Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere, Dar es Salaam, tarehe 23 Julai 2025.Ziara hiyo iliongozwa na Mwenyekiti wa Bodi Mhe. Jaji Mshibe Ali Bakari na Makamu Mwenyekiti, Dkt. Emmanuel Mpeta.

Akizungumza wakati wa ziara hiyo, Jaji Mshibe alisema lengo la ziara ni kukagua  na kutathmini usimamzi na utendaji kazi wa miundombinu ya TMA  na kutathmini  utekelezaji wa Maagizo na Maelekezo ya Bodi katika kuboresha huduma na pia kutambua changamoto zilizopo,  na kuona Taasisi ilipo na inapoelekea. “Bodi imekuwa ikitoa maelekezo hivyo leo ilikuwa ni siku maalum kuangalia utekelezaji wake”.Alisema Jaji Mshibe.

Alisisitiza kuwa TMA ya sasa imepiga hatua kubwa katika uboreshaji wa miundombinu ya utoaji huduma. Aidha, aliishukuru Serikali ya Awamu ya Sita kwa kuendelea kuiwezesha Mamlaka kwa miundombinu ya kisasa.

Kwa upande wake, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TMA na  Makamu Mwenyekiti wa Jopo la Kimataifa la Mabadiliko ya Tabianchi Dkt, Ladislaus Chang’a aliishukuru Bodi kwa kutembelea  na kujionea utendaji kazi wa Mamlaka katika  Uangazi, Uchakataji wa data na utoaji wa utabiri na kujionea miundombinu ya Kisasa ambayo Serikali imeiwezesha TMA kuipata. Pia alishukuru Bodi  kwa maelekezo ambayo wamekuwa wakiyatoa kupitia vikao mbalimbali vya bodi, na kuiwezesha TMA kuendelea kuwa bora.

Akitoa ufafanuzi wa faida za uwekezaji wa miundombinu ya kisasa katika sekta ya hali ya hewa nchini alisema “ Kupitia rada za hali ya hewa, Mamlaka imefanikiwa kuboresha utabiri wa hali ya hewa pamoja na kuendesha mafunzo ya rada kwa nchi za Afrika Mashariki na Kati,  wataalamu wa hali ya  hewa kutoka nchi 10 za  Afrika Mashariki na Kati walipata mafunzo mjini Mwanza , Tanzania na  kuendelea  kuipa heshima kubwa nchi yetu”. 

Aliongeza kwa kufafanua kuwa, Serikali imeendelea kuhakikisha usimamizi wa mitambo hii ya kisasa inakuwa endelevu kwa kuajiri na kuwezesha wataalamu kupata mafuzo husika, ambapo mpaka sasa TMA ina  wahandisi 30.

Katika hatua nyingine wajumbe wa Bodi walipata fursa ya kutembelea Kompyuta Kubwa ya Kisasa (Computer Cluster) yenye uwezo mkubwa wa kuchambua na kuchakata taarifa za hali ya hewa na kuimarisha utoaji utabiri katika maeneo madogomadogo na mahsusi kwa haraka na usahihi zaidi. 

Thursday, July 17, 2025

TANZANIA STRENGTHENS REGIONAL METEOROLOGICAL CAPACITIES IN EAST AFRICA


 Dar es Salaam, Tanzania – 16th July 2025

The Tanzania Meteorological Authority (TMA) continues to demonstrate strong leadership in strengthening meteorological services across East Africa, following the implementation of resolutions from the East African Community (EAC) Heads of Meteorological Services meeting held in Entebbe, Uganda from 23rd to 24th May 2024.

As part of this effort, Dr. Mafuru Kantamla, Manager of the Central Forecasting Office, conducted a training workshop on severe weather forecasting for the South Sudan Meteorological Services (SSMS). The training held in Juba from 16th  to 19th  June 2025, brought together operational forecasters to develop and strengthen their skills in generating five-days weather forecasts and issuing early warnings for high-impact weather events.

In a parallel initiative, TMA Quality Management System (QMS) experts, Dr. Geofrid Chikojo and Mr. Danford Nyenyema, conducted the Inception Phase for QMS implementation at Burundi’s Meteorological Service (IGEBU) from 27th  to 31st  January 2025 and  9th  to 13th  June 2025. The experts facilitated IGEBU on the preparation and establishment of key QMS documents, procedures, and internal auditing processes.

These missions were carried out in collaboration with the World Meteorological Organization (WMO), supported through the Climate Risk and Early Warning Systems East Africa (CREWS EA) Project.

Commenting on these developments, Dr. Ladislaus Chang’a, Acting Director General of TMA and Vice Chair of the Intergovernmental Panel on Climate Change (IPCC), said:

TMA is happy  and committed to contribute in strengthening the provision of meteorological services including early warning systems in the continent in the spirit of not leaving any one behind, taping in our differentiated capabilities and using our individual and collective strengths. These missions to South Sudan and Burundi are  consistent with TMA Vision and are examples of our shared commitment to strengthen the Implementation of the  Agenda 2063, the Africa we want, and the World Meteorological Organization Strategic Plan (2024 – 2027).”

 

TANZANIA YACHANGIA UIMARISHWAJI WA HUDUMA ZA HALI YA HEWA


  Dar es Salaam, Tanzania – 16 Julai 2025

Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) inaendelea kujizatiti katika kuimarisha huduma za hali ya hewa katika ukanda wa Afrika Mashariki, ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa maazimio ya kikao cha Wakuu wa taasisi za Hali ya Hewa wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) kilichofanyika tarehe 23 hadi 24 Mei, 2024 Entebbe, Uganda.

Kama sehemu ya utekelezaji wa maazimio,  Dkt. Mafuru Kantamla, Meneja wa Ofisi ya Utabiri Hali ya Hewa, alitoa  mafunzo ya utoaji wa utabiri wa hali mbaya ya hewa sambamba na utoaji wa tahadhari ya hali mbaya ya hewa kwa wataalamu wa  hali ya hewa wa Sudan Kusini (SSMS). Mafunzo hayo yalifanyika mjini Juba kuanzia tarehe 16 hadi 19 Juni 2025.

Wakati huo huo, wataalamu wa Mfumo wa Usimamizi wa Ubora (QMS) kutoka TMA, Dkt. Geofrid Chikojo na Bw. Danford Nyenyema walitekeleza awamu mbili za mafunzo kwa Taasisi ya Hali ya Hewa ya Burundi (IGEBU) katika mchakato wa kuanzisha utekelezaji wa QMS. Mafunzo haya yalifanyika kuanzia tarehe 27 hadi 31 Januari 2025 na kuendelea tena tarehe 9 hadi 13 Juni 2025. Aidha, mafunzo haya yalilenga kuweka misingi ya maandalizi ya taratibu za kazi, kuandaa nyaraka za QMS na kufanya ukaguzi wa ndani.

Mafunzo haya yote yamefanyika kwa kushirikiana na Shirika la Hali ya Hewa Duniani (WMO) na yamefadhiliwa kupitia Mradi wa CREWS Afrika Mashariki.

Akizungumza kuhusu mafanikio haya, Dkt. Ladislaus Chang’a, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TMA na Makamu Mwenyekiti wa IPCC alisema:

“TMA imejipanga kikamilifu kuchangia katika kuimarisha utoaji wa huduma za hali ya hewa, ikiwa ni pamoja na mifumo ya tahadhari za hali ya hewa barani Afrika, kwa kuzingatia dhana ya kutomwacha yeyote nyuma, kutumia uwezo wetu wa kipekee na nguvu zetu binafsi na za pamoja. Ziara hizi za kitaalamu nchini Sudan Kusini na Burundi ni sehemu ya utekelezaji wa Dira ya TMA na ni mfano wa dhamira yetu ya pamoja ya kuimarisha utekelezaji wa Ajenda 2063 ya Afrika Tunayoitaka, pamoja na Mpango Mkakati wa Shirika la Hali ya Hewa Duniani (2024–2027).”

 

Wednesday, July 2, 2025

DKT CHANG’A AFANYA MAZUNGUMZO YA KITALAMU NA KATIBU MKUU WA SHIRIKA LA HALI YA HEWA DUNIANI (WMO)

 


Geneva, 2 Julai 2025

Katibu Mkuu wa Shirika la Hali ya Hewa Duniani (World Meteorological Organization - WMO) Prof. Celeste Saulo ameahidi kushirikiana na Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) katika kuboresha huduma za hali ya hewa kwa matumizi katika sekta mbalimbali za kiuchumi na kijamii.

Ameyasema hayo wakati wa kikao baina yake na Dkt. Ladislaus Chang’a, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya hali ya Hewa Tanzania (TMA), ambaye pia ni Mwakilishi wa kudumu wa Tanzania katika WMO na Makamu wa Mwenyekiti wa Jopo la Kimataifa la Sayansi ya Mabadiliko ya Hali ya Hewa na Tabianchi (IPCC) wakati wa kikao cha 69 cha Kamati Kuu Tendaji ya IPCC (Intergovernmental Panel on Climate Change-IPCC (69th IPCC Bureau),tarehe 02 Julai 2025 Jijini Geneva, Uswisi. Kikao hicho kilikuwa na lengo la kujadiliana kuhusu maendeleo ya utoaji wa huduma za hali ya hewa na mipango ya kuendeleza ushirikiano.

Prof. Celeste Saulo ameipongeza TMA kwa uwekezaji mkubwa katika sekta ya hali ya hewa kupitia Serikali hususan katika miundombinu ya kisasa ya hali ya hewa na kwa kuendelea kufanya vizuri katika utoaji wa huduma za hali ya hewa nchini pamoja na kusaidia nchi nyingine katika sekta ya hali ya hewa. Prof. Celeste Saulo ameahidi kuendelea kusaidia katika kuboresha huduma za hali ya hewa na mafunzo kwa wataalamu wa hali ya hewa kupitia programu mbalimbali za WMO ikiwa ni pamoja na eneo la mafunzo ya akili mnemba (Artificial Inteligence-AI). Aidha, Prof. Saulo amesisitiza kuwa, Taasisi za Hali ya hewa za nchi wanachama ndizo zenye jukumu mahsusi la kutoa huduma za hali ya hewa katika nchi Wanachama wa WMO hivyo uwekezaji katika sekta hii utaboresha zaidi huduma hizi kwa jamii.

“ Taasisi za hali ya hewa kama TMA ndizo zenye jukumu mahsusi na chanzo cha kuaminika cha huduma za hali ya hewa kwa mujibu wa miongozo ya WMO na napongeza TMA kwa kuendelea kutumia vyema uwekezaji wa Serikali ya Tanzania kutoa huduma bora za hali ya hewa. Pia napongeza TMA kwa kuwa mstari wa mbele kusimamia vyema programu za WMO na kusaidia nchi nyingine kikanda ili kuboresha zaidi huduma huduma za hali ya hewa katika nchi zao na kikanda” Alisema Prof. Celeste Saulo.

Katika Kikao hicho, Dkt. Ladislaus Chang’a ameeleza dhamira ya TMA ya kuboresha huduma za hali ya hewa na kusimamia vyema programu za WMO zinazotekelezwa nchini na kikanda. 

“TMA itaendelea kutoa wataalamu wake mahiri kuchangia katika utekelezaji wa programu mbalimbali za WMO kwa manufaa ya Dunia nzima na tutaendelea kusaidia wenzetu hasa katika kanda ya Afrika kwa uzoefu wa utaalamu tulio nao, kwa msaada wa WMO na  uwekezaji mkubwa wa Serikali katika tasnia ya hali ya hewa nchini” Alisema Dkt. Chang’a.

Aidha, Dkt. Chang’a alimjulisha Katibu Mkuu wa WMO kuwa, Taasisi za Hali ya Hewa za Nchi wanachama wa WMO ambazo wataalamu wa TMA wametoa msaada wa kiufundi Barani Afrika hivi karibuni ni pamoja na Lesotho, Namibia, Burundi, Zimbabwe na Sudan Kusini, ambapo nchi hizo waliwezeshwa katika maeneo mbalimbali yakiwemo ya uboreshaji wa “Mfumo wa Usimamizi wa Ubora wa huduma (Quality Management System-QMS and Competency Assessment )”, Utabiri wa Hali Mbaya ya Hewa, Utabiri wa Hali ya Hewa kwa Kutumia Modeli za Kihesabu/Kompyuta (Numerical Weather Prediction-NWP)”, “Mchakato wa kisheria katika sekta ya hali ya hewa na Usambazaji wa Huduma za Hali ya Hewa kwa Umma. 


Friday, June 27, 2025

MKUU WA MAKAPTENI ZANZIBAR AELEZEA MIPANGO YA SAFARI INAVYOTEGEMEA TAARIFA ZA HALI YA HEWA.

 





Zanzibar, Tarehe 25 Juni 2025:

Mkuu wa Makapteni Zanzibar, Kapteni Kadadi Hassan Shea, ameelezea namna taarifa za hali ya hewa zinavyowasaidia katika kupanga safari zao baharini na kuepukana na hasara zinazoweza kujitokeza.

Alizungumza hayo kupitia vyombo vya habari alipokuwa ametembelea banda la Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) lililokuwa katika maonesho ya Maadhimisho ya Siku ya Mabaharia Duniani yaliyofanyika katika viwanja vya Mnazi Mmoja, Zanzibar kuanzia Tarehe 22 hadi 25 Juni 2025.

"Taarifa za hali ya hewa zinatusaidia sana katika kufanya mipango ya safari zetu baharini ili kuepusha au kupunguza hasara zinazoweza kujitokeza, mfano kukiwa na utabiri wa uwepo wa upepo mkali huwa tunajipanga kwa kuchukua mizigo kidogo katika kukabiliana nao, na kama kuna utabiri wa uwepo wa mvua tunachukua maamuzi ya kupakia mizigo, kama vile saruji, kwenye makontena," alielezea Kapteni Shea.

Kaptain shea aliongezea kuwa maonesho haya yanawapa fursa Mabaharia kukutana na kufahamiana na taasisi mbalimbali ili kuunganisha nguvu ya pamoja katika kuihudumia jamii kwa usalama na faida zaidi.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa TMA Ofisi ya Zanzibar, Ndg. Masoud Makame Faki, alisema ushiriki wa Mamlaka katika maonesho hayo yanajielezea kupitia kauli mbiu yake inayosema "Bahari Yetu, Wajibu Wetu na Fursa Yetu," ambapo kupitia kipengele cha wajibu wetu TMA inawajibika katika kuelezea namna huduma za hali ya hewa zinavyoweza kusaidia katika kuokoa maisha ya mabaharia, wasafiri na mali kwa ujumla.

Monday, June 23, 2025

TMA YASHIRIKI KATIKA MAONESHO YA KUADHIMISHA WIKI YA UTUMISHI WA UMMA 2025.

 


Dodoma, tarehe 18 Juni 2025.

 

Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imepata fursa ya kushiriki katika maonesho ya kuadhimisha wiki ya utumishi wa Umma yanayofanyika katika viwanja vya Chinangali Park, Dodoma kuanzia tarehe 16 hadi 23 Juni 2025.

 

Kupitia maonesho hayo wageni kutoka sekta mbalimbali nchini wameendelea kutembelea banda la TMA ikiwemo Waziri wa Nchi – Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene ili kujifunza masuala mbalimbali yalioandaliwa katika utoaji elimu juu ya huduma zitolewazo na TMA kwa manufaa ya jamii na maendeleo ya Taifa,

 

Kaulimbiu ya maonesho hayo ni “Kujenga Mifumo Thabiti ya Utoaji Huduma kwa Maendeleo Endelevu”.

 

Monday, June 2, 2025

TMA YAPONGEZWA KWA KUIMARISHA USHIRIKISHWAJI WA WADAU KATIKA KUONGEZA UELEWA WA MATUMIZI SAHIHI YA TAARIFA ZA HALI YA HEWA NA SHERIA YA MAMLAKA YA HALI YA HEWA TANZANIA.












Dodoma; Tarehe 30 Mei, 2025;

Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imepongezwa na kuhimizwa kuendeleza ushirikiano na wadau wa sektambalimbali za kiuchumi na Kijamii ili kuongeza uelewa wamatumizi sahihi ya huduma za hali ya hewa pamoja na ufanisikatika  uzingatiaji wa sheria Namba 2 ya mwaka 2019 ya mamlaka ya hali ya hewa Tanzania.

 

Hayo yalisemwa na mwenyekiti wa Bodi ya Chuo cha Hali yahewa Tanzania(NMTC) Dkt, Emmanuel Mpeta KatikaUfunguzi wa warsha ya uelewa wa huduma  za hali ya hewazinazotolewa na Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania kwawadau kuitoka sekta mbalimbali nchiniwakiwemoWanahabariMafunzo haya yalifanyika kuanzia Tarehe 27 – 30, Mei 2025  kwenye ukumbi wa Royal village jijiniDodoma.

 

Nawapongeza TMA kwa kuendelea kuwashirikisha wadauwa sekta mbalimbali  kw lengo la kuimarisha matumizi yataarifa ya za hali ya hewa katika shughuli za kijamii nakiuchumiWarsha hii ni fursa muhimu ya kuboresha hudumaza hali ya hewa na kuimarisha matumizi sahihi ya huduma zahali ya hewa zinazotolewa na Mamlaka ya Hali ya HewaTanzania, ikiwemo uzingatiaji wa Sheria ya Mamlaka ya Haliya Hewa Na.2 ya 2019 katika shughuli zinazotumia au zinazotakiwa kutumia huduma za hali ya hewa nchiniWarshahii pia ni fursa ya kujenga na kuimarisha uelewa kuhusiana nachangamoto na fursa za mabadiliko ya hali ya hewa na Tabianchi.” alisema DktMpeta

 

Dkt Mpeta alisisitiza pia umuhimu wa wadau wote kuzingatiasheria Na 2 ya Mamlaka ya hali ya hewa Tanzania katikashughuli zao za kila siku za kiuchumi na kijamii. “Utekelezajiwa sheria ya Mamlaka unaambatana na jukumu la kusimamiahuduma za hali ya hewa pamoja na udhibiti  wa shughuli zahali ya hewa hapa nchiniMkutano huu ni muhimu katikakuwajengea wadau uelewa wa nini wanapaswa kufanya kwamujibu wa Sheria”.

 

Kwa upande wake, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TMA na Makamu Mwenyekiti wa Jopo la Kimataifa la Mabadiliko yaTabianchi DktLadislaus Chang’a aliwashukuru wafadhili waMradi wa  “WISER” na washirika wengine kwa kuendeleakushirikiana na TMA katika kuimarisha huduma za hali yahewa.

AidhaDktChang’a alisisitiza umuhimu wa  kuzingatiamatumizi sahihi ya huduma za hali ya hewa katika kufanyamaamuzi stahiki wakati woteVilevile aliendelea kuvishukuruvyombo vya habari kwa kuendelea kuwa kiungo cha kutoahabari sahihi za hali ya hewa kwa jamii.

 

Warsha hii imehusisha wadau kutoka sekta mbalimbali zakiuchumi na kijamii nchini kama vile nishatikilimomajihabarimaafaSerikali za Mitaa pamoja na Sekta binafsiMamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania inaendelea na  juhudi zakuhakikisha jamii inapata uelewa mpana wa taarifa za hali yahewa kwa ajili ya kuongeza ufanisi wa matumizi ya taarifa hizi kwenye shughuli za kiuchumi na kijamii.

Saturday, May 24, 2025

SULUHU MGAWANYO WA MAPATO WA HUDUMA ZA USAFIRI WA ANGA NCHINI YAPATIKANA.

 









Dar es Salaam; Tarehe 23 Mei 2025;

Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA), Mamlaka ya Viwanja vya Ndege (TAA), Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) pamoja na Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL) wafanikisha upatikanaji wa suluhu ya mgawanyo wa mapato yatokanayo na huduma za usafiri wa anga nchini.

Suluhu hiyo imepatikana kupitia kusainiwa kwa mkataba wa makubaliano ya pamoja baina ya wakuu wa taasis hizo katika ukumbi wa mikutano wa TAA uliopo katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, tarehe 23 Mei 2025.

Mkataba huo unafuatia kuundwa kwa mfumo wa kielektroniki (Ankara Jumuishi) utakaosaidia kuimarisha uwazi, ufanisi na tija katika mgawanyo wa mapato yatakayokuwa yamekusanywa kwa kuingizwa moja kwa moja kwenye taasis husika kulingana na asilimia zilizokubalika. Mfumo unatarajiwa kuanza kutumika kuanzia tarehe 1 Julai 2025.

Wakizungumza katika zoezi la utiaji saini, Mkurugenzi Mkuu wa TAA, Bw. Abdul Mombokaleo alieleza kuwa mfumo huo wa kielektroniki utarahisisha mgawanyo wa mapato na kuwezesha kila taasis kupata mgao wake kwa wakati ili kusukuma gurudumu la maendeleo ya nchi yetu. Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TMA na Makamu Mwenyekiti wa Jopo la Kimataifa la Sayansi ya Mabadiliko ya Hali ya Hewa na Tabianchi (IPCC), Dkt. Ladislaus Chang’a aliwashukuru viongozi wenzake kwa kufanikisha kukamilika kwa mfumo huo na kusisitiza kuwa mfumo huo utachangia sana kuongeza tija na ufanisi katika utendaji kwa kupunguza muda na nguvu kubwa iliyokuwa inatumika kufuatilia mapato yatokanayo na huduma zitolewazo na kila taasis

Aidha, Mkurugenzi Mtendaji wa ATCL, Mhandisi Peter Ulanga alipongeza muitikio kutoka pande zote wa kutekeleza maelekezo ya Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kufanya mifumo ya taasis za serikali kusomana, naye Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TCAA, Bw. Daniel Malanga alipongeza hatua iliyofikiwa sababu itaboresha utoaji huduma ndani ya viwanja vya ndege nchini.




TMA NA CRDB ZAWANOA MAAFISA UGANI MBEYA, NJOMBE, IRINGA NA SONGWE








Wataalamu wa Mamlaka ya Hali ya Hewa (TMA) kwa kushirikiana na Benki ya CRDB kupitia mradi wa Tanzania Agriculture Climate Adaptation Technology Deployment Project (TACATDP) wamewajengea uwezo Maafisa Ugani wa namna bora ya kutafsiri na kutumia taarifa za hali ya hewa hususani katika shughuli za kilimo.

Akizungumza wakati wa kufungua mafunzo hayo Meneja wa Kanda ya Nyanda za Juu Kusini Magharibi (TMA) Bw. Elias Elipiki, alisema mafunzo hayo yanawalenga Maafisa Ugani kwani wao ni daraja kati ya TMA na wakulima, hivyo mafunzo haya yanalenga kutoa elimu  ya namna sahihi ya kutafsiri taarifa za hali ya hewa zinazotolewa na Mamlaka na kuwawezesha wakulima kufanya mipango sahihi juu ya shughuli za kilimo kwa msimu husika.

Aidha, Meneja Uhusiano kutoka CRDB ambaye pia ni msimamizi wa utoaji wa mikopo inayozingatiwa uhifadhi wa mazingira katika mradi wa (TACATDP) Bw. Karim Kindole,  alisema CRDB na TMA wana ushirikiano katika kuwajengea uwezo Maafisa Ugani namna ya kudhibiti na kuwasaidia wakulima kupata taarifa sahihi za mabadiliko ya hali ya hewa.

Naye, Afisa Kilimo kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Mbarali Bw. Sostenesi Silayo, aliwashukuru TMA na CRDB kwa kuwapa nafasi Maafisa Ugani kupata elimu ambayo wataitumia katika kuwashauri wakulima kulima kilimo sahihi kutokana na hali ya hewa husika na kuongeza tija katika uzalishaji wa mazao mengi.

Featured Post

DKT. KIJAZI: KIWANGO CHA USAHIHI WA UTABIRI WA MSIMU WA VULI 2019 KIWE CHA JUU ZAIDI.

Mkurugenzi mkuu wa TMA na Makamu wa Tatu wa Rais wa Shirika la Hali ya Hewa Duniani Dkt. Agnes Kijazi (katikati mwenye suti nyeusi) waka...