Saturday, August 9, 2025

TMA YANYAKUA KOMBE MAONESHO YA NANE NANE 2025.

 






Morogoro, tarehe 08/08/2025

Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imenyakua kombe kupitia maonesho ya Nane Nane 2025 yaliyofanyika katika Mkoa wa Morogoro. Ushindani wa TMA kupitia kundi la ushindani lililohusisha taasis za serikali upande wa Mawakala na Mamlaka za serikali nchini, umeifanya TMA kuibuka kidedea kwa kushika nafasi ya pili kwenye ambapo Mamlaka ya Hifadhi za Taifa (TANAPA) ilishika nafasi ya kwanza na Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) ikishika nafasi ya tatu.

Aidha, TMA imelipokea kombe hilo kwa furaha kubwa na kutoa shukrani zao za dhati kwa waratibu wa maonesho hayo kwa kutambua mchango mkubwa wa TMA katika kuhudumia wadau mbalimbali kwenye maonesho hayo, ambapo wageni zaidi ya 2942 wameweza kuhudumiwa katika nyanja mbalimbali ikiwemo elimu ya sayansi ya hali ya hewa.

Thursday, August 7, 2025

VIONGOZI WAKUMBUSHWA KUHAMASISHA WANANCHI KUTUMIA TAARIFA ZA TMA


 









Morogoro, tarehe 07 Agosti 2025

Katibu Tawala wa Mkoa wa Pwani Bi. Pili Mnyema amewakumbusha viongozi mbalimbali nchini kuendelea na jitihada za kuhamasisha wananchi kutumia taarifa za hali ya hewa zinazotolewa na Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA), aliyasema hayo alipokuwa akizungumza na wananchi kupitia vyombo vya habari katika Maonesho ya Nane Nane 2025 yanayoendelea kwenye viwanja vya Nane Nane, Morogoro.

“Kama viongozi tunajukumu la kuwaelimisha na kuwahamasisha wananchi wetu ikiwemo wakulima, wafugaji na wavuvi ili watumie utabiri wa hali ya hewa unaotolewa na Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania, itawasaidia wananchi kujikinga na athari zinazoweza kujitokeza kutokana na mabadiliko ya hali ya hewa yaliyopo”. Alisisitiza Bi. Pili Mnyema

Kwa upande wa Meneja wa Kanda ya Mashariki-TMA, Bi. Hidaya Senga ameelezea njia mbalimbali zinazotumiwa na TMA katika usambazaji wa taarifa zake kama vile vyombo vya habari, tovuti, mitandao ya kijamii pamoja ushirikiano mkubwa na Taasis za kisekta ambao umesaidia kufikia wadau wengi wa sekta mbalimbali.

Bi. Hidaya ameongezea kwa kuwashauri wanafunzi kutembelea banda la TMA lililopo katika maonesho hayo ya Nane Nane ili kujifunza teknolojia mpya inayotumika TMA kwa kuona mtambo wa kisasa unaojiendesha wenyewe (Automatic Weather Station) kwa uhalisia zaidi.

Wednesday, August 6, 2025

ELIMU YA HUDUMA MAHUSUSI ZA HALI YA HEWA ZAWAVUTIA WENGI NANENANE MOROGORO

 










Morogoro, 06 Agosti 2025;

Elimu ya huduma mahususi za hali ya hewa inayotolewa na Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imeendelea kuwavutia wadau wengi waliotembelea katika banda la TMA kupitia maonesho ya NaneNane 2025 yanayoendelea kufanyika katika viwanja vya NaneNane, Morogoro.

“ Sikuwahi kufikiria kama TMA inauwezo wa kuniandalia utabiri katika maeneo ya shamba langu, kwa kweli imenivutia sana” Alizungumza hayo mmoja wa wadau waliotembelea banda la TMA kupitia maonesho ya NaneNane, Morogoro Ndg. Seif Sempanga, Mkulima mwenye Ekari Zaidi ya 300, Kilindi Tanga.

Aidha, kupitia ujio wa wanafunzi kutoka shule mbalimbali mkoani Morogoro, wameshukuru sana kupata elimu ya mchakato mzima wa uandaaji utabiri wa hali ya hewa, namna taarifa za hali ya hewa zinavyosaidia huduma za usafirishaji ikiwemo usafiri wa anga na maji pamoja na sekta ya utalii.

“Namshukuru Mungu nimekuja kutembelea banda la TMA, nimejifunza mengi ambayo mengine sikuwahi kufikiria kuwa TMA wanafanya kazi kubwa namna hii, kumbe uwepo wa mvua inasaidia sekta ya utalii kuneemeka katika upatikanaji wa wanyama wengi kutokana na uwepo wa malisho na maji ya kutosha” alisema hayo mwanafunzi Nusiata Alexanda, kidato cha tatu kutoka shule ya sekondari ya sharte, Morogoro.

Monday, August 4, 2025

TMA YATUMIA FURSA YA MAONESHO YA NANENANE KUTOA ELIMU KWA JAMII









Dodoma, 03 Agosti 2025

Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imetumia fursa ya Maonesho NaneNane 2025 Kitaifa  yanayofanyika katika Viwanja vya Nzuguni, Dodoma kutoa elimu kwa jamii kuhusu huduma zitolewazo pamoja na jukumu kubwa la TMA la kudhibiti shughuli za hali ya hewa nchini.

Kupitia maonesho haya, wananchi na wadau mbalimbali wakiwemo wakulima, wavuvi na wafugaji wamepata elimu ya moja kwa moja kutoka kwa wataalamu wa TMA wakiwemo viongozi.

TMA imeeleza namna taarifa za hali ya hewa zinavyokusanywa, kuchakatwa na kuchambuliwa kupitia mifumo ya kisasa, na jinsi huduma hizo zinavyoweza kusaidia jamii.Aidha, TMA imeeleza umuhimu wa kuendesha shughuli za hali ya hewa zenye kukidhi viwango vya kitaifa na kimataifa.

Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TMA ,Dkt.Ladislaus Chang'a na Makamu Mwenyekiti wa Jopo la Kimataifa la Sayansi ya Mabadiliko ya Hali ya Hewa na Tabianchi (IPCC), akiwahudumia wateja kwenye Banda la Mamlaka aliwahimiza wadau wote kufuatilia utabiri wa kila siku, utabiri wa msimu pamoja na tahadhari za hali mbaya ya hewa, huku akisisitiza matumizi sahihi ya taarifa hizo katika shughuli zote za kiuchumi na kijamii.

Aidha, aliishukuru Serikali kwa kuendelea kuwekeza katika miundombinu ya hali ya hewa na  rasilimali watu na hivyo kuleta maendeleo makubwa ya utendaji kazi wa Mamlaka.

Mamlaka ya Hali ya HewaTanzania inashiriki katika maonesho ya NaneNane Dodoma, Zanzibar, Mbeya na Morogoro.Kauli Mbiu ya mwaka huu ni  “Chagua Viongozi Bora kwa Maendeleo ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi 2025”.

Wednesday, July 23, 2025

BODI YA TMA YAFANYA ZIARA YA KIKAZI RADA YA HALI YA HEWA BANGULO, PUGU NA KITUO CHA HALI YA HEWA JNIA














Dar es Salaam; Tarehe 23 Julai, 2025;

Bodi ya Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imefanya ziara ya kikazi ya kukagua utendaji kazi wa Mamlaka katika kituo cha Rada ya Hali ya Hewa, Bangulo, Pugu na Ofisi za TMA zilizopo katika Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere, Dar es Salaam, tarehe 23 Julai 2025.Ziara hiyo iliongozwa na Mwenyekiti wa Bodi Mhe. Jaji Mshibe Ali Bakari na Makamu Mwenyekiti, Dkt. Emmanuel Mpeta.

Akizungumza wakati wa ziara hiyo, Jaji Mshibe alisema lengo la ziara ni kukagua  na kutathmini usimamzi na utendaji kazi wa miundombinu ya TMA  na kutathmini  utekelezaji wa Maagizo na Maelekezo ya Bodi katika kuboresha huduma na pia kutambua changamoto zilizopo,  na kuona Taasisi ilipo na inapoelekea. “Bodi imekuwa ikitoa maelekezo hivyo leo ilikuwa ni siku maalum kuangalia utekelezaji wake”.Alisema Jaji Mshibe.

Alisisitiza kuwa TMA ya sasa imepiga hatua kubwa katika uboreshaji wa miundombinu ya utoaji huduma. Aidha, aliishukuru Serikali ya Awamu ya Sita kwa kuendelea kuiwezesha Mamlaka kwa miundombinu ya kisasa.

Kwa upande wake, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TMA na  Makamu Mwenyekiti wa Jopo la Kimataifa la Mabadiliko ya Tabianchi Dkt, Ladislaus Chang’a aliishukuru Bodi kwa kutembelea  na kujionea utendaji kazi wa Mamlaka katika  Uangazi, Uchakataji wa data na utoaji wa utabiri na kujionea miundombinu ya Kisasa ambayo Serikali imeiwezesha TMA kuipata. Pia alishukuru Bodi  kwa maelekezo ambayo wamekuwa wakiyatoa kupitia vikao mbalimbali vya bodi, na kuiwezesha TMA kuendelea kuwa bora.

Akitoa ufafanuzi wa faida za uwekezaji wa miundombinu ya kisasa katika sekta ya hali ya hewa nchini alisema “ Kupitia rada za hali ya hewa, Mamlaka imefanikiwa kuboresha utabiri wa hali ya hewa pamoja na kuendesha mafunzo ya rada kwa nchi za Afrika Mashariki na Kati,  wataalamu wa hali ya  hewa kutoka nchi 10 za  Afrika Mashariki na Kati walipata mafunzo mjini Mwanza , Tanzania na  kuendelea  kuipa heshima kubwa nchi yetu”. 

Aliongeza kwa kufafanua kuwa, Serikali imeendelea kuhakikisha usimamizi wa mitambo hii ya kisasa inakuwa endelevu kwa kuajiri na kuwezesha wataalamu kupata mafuzo husika, ambapo mpaka sasa TMA ina  wahandisi 30.

Katika hatua nyingine wajumbe wa Bodi walipata fursa ya kutembelea Kompyuta Kubwa ya Kisasa (Computer Cluster) yenye uwezo mkubwa wa kuchambua na kuchakata taarifa za hali ya hewa na kuimarisha utoaji utabiri katika maeneo madogomadogo na mahsusi kwa haraka na usahihi zaidi. 

Thursday, July 17, 2025

TANZANIA STRENGTHENS REGIONAL METEOROLOGICAL CAPACITIES IN EAST AFRICA


 Dar es Salaam, Tanzania – 16th July 2025

The Tanzania Meteorological Authority (TMA) continues to demonstrate strong leadership in strengthening meteorological services across East Africa, following the implementation of resolutions from the East African Community (EAC) Heads of Meteorological Services meeting held in Entebbe, Uganda from 23rd to 24th May 2024.

As part of this effort, Dr. Mafuru Kantamla, Manager of the Central Forecasting Office, conducted a training workshop on severe weather forecasting for the South Sudan Meteorological Services (SSMS). The training held in Juba from 16th  to 19th  June 2025, brought together operational forecasters to develop and strengthen their skills in generating five-days weather forecasts and issuing early warnings for high-impact weather events.

In a parallel initiative, TMA Quality Management System (QMS) experts, Dr. Geofrid Chikojo and Mr. Danford Nyenyema, conducted the Inception Phase for QMS implementation at Burundi’s Meteorological Service (IGEBU) from 27th  to 31st  January 2025 and  9th  to 13th  June 2025. The experts facilitated IGEBU on the preparation and establishment of key QMS documents, procedures, and internal auditing processes.

These missions were carried out in collaboration with the World Meteorological Organization (WMO), supported through the Climate Risk and Early Warning Systems East Africa (CREWS EA) Project.

Commenting on these developments, Dr. Ladislaus Chang’a, Acting Director General of TMA and Vice Chair of the Intergovernmental Panel on Climate Change (IPCC), said:

TMA is happy  and committed to contribute in strengthening the provision of meteorological services including early warning systems in the continent in the spirit of not leaving any one behind, taping in our differentiated capabilities and using our individual and collective strengths. These missions to South Sudan and Burundi are  consistent with TMA Vision and are examples of our shared commitment to strengthen the Implementation of the  Agenda 2063, the Africa we want, and the World Meteorological Organization Strategic Plan (2024 – 2027).”

 

TANZANIA YACHANGIA UIMARISHWAJI WA HUDUMA ZA HALI YA HEWA


  Dar es Salaam, Tanzania – 16 Julai 2025

Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) inaendelea kujizatiti katika kuimarisha huduma za hali ya hewa katika ukanda wa Afrika Mashariki, ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa maazimio ya kikao cha Wakuu wa taasisi za Hali ya Hewa wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) kilichofanyika tarehe 23 hadi 24 Mei, 2024 Entebbe, Uganda.

Kama sehemu ya utekelezaji wa maazimio,  Dkt. Mafuru Kantamla, Meneja wa Ofisi ya Utabiri Hali ya Hewa, alitoa  mafunzo ya utoaji wa utabiri wa hali mbaya ya hewa sambamba na utoaji wa tahadhari ya hali mbaya ya hewa kwa wataalamu wa  hali ya hewa wa Sudan Kusini (SSMS). Mafunzo hayo yalifanyika mjini Juba kuanzia tarehe 16 hadi 19 Juni 2025.

Wakati huo huo, wataalamu wa Mfumo wa Usimamizi wa Ubora (QMS) kutoka TMA, Dkt. Geofrid Chikojo na Bw. Danford Nyenyema walitekeleza awamu mbili za mafunzo kwa Taasisi ya Hali ya Hewa ya Burundi (IGEBU) katika mchakato wa kuanzisha utekelezaji wa QMS. Mafunzo haya yalifanyika kuanzia tarehe 27 hadi 31 Januari 2025 na kuendelea tena tarehe 9 hadi 13 Juni 2025. Aidha, mafunzo haya yalilenga kuweka misingi ya maandalizi ya taratibu za kazi, kuandaa nyaraka za QMS na kufanya ukaguzi wa ndani.

Mafunzo haya yote yamefanyika kwa kushirikiana na Shirika la Hali ya Hewa Duniani (WMO) na yamefadhiliwa kupitia Mradi wa CREWS Afrika Mashariki.

Akizungumza kuhusu mafanikio haya, Dkt. Ladislaus Chang’a, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TMA na Makamu Mwenyekiti wa IPCC alisema:

“TMA imejipanga kikamilifu kuchangia katika kuimarisha utoaji wa huduma za hali ya hewa, ikiwa ni pamoja na mifumo ya tahadhari za hali ya hewa barani Afrika, kwa kuzingatia dhana ya kutomwacha yeyote nyuma, kutumia uwezo wetu wa kipekee na nguvu zetu binafsi na za pamoja. Ziara hizi za kitaalamu nchini Sudan Kusini na Burundi ni sehemu ya utekelezaji wa Dira ya TMA na ni mfano wa dhamira yetu ya pamoja ya kuimarisha utekelezaji wa Ajenda 2063 ya Afrika Tunayoitaka, pamoja na Mpango Mkakati wa Shirika la Hali ya Hewa Duniani (2024–2027).”

 

Wednesday, July 2, 2025

DKT CHANG’A AFANYA MAZUNGUMZO YA KITALAMU NA KATIBU MKUU WA SHIRIKA LA HALI YA HEWA DUNIANI (WMO)

 


Geneva, 2 Julai 2025

Katibu Mkuu wa Shirika la Hali ya Hewa Duniani (World Meteorological Organization - WMO) Prof. Celeste Saulo ameahidi kushirikiana na Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) katika kuboresha huduma za hali ya hewa kwa matumizi katika sekta mbalimbali za kiuchumi na kijamii.

Ameyasema hayo wakati wa kikao baina yake na Dkt. Ladislaus Chang’a, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya hali ya Hewa Tanzania (TMA), ambaye pia ni Mwakilishi wa kudumu wa Tanzania katika WMO na Makamu wa Mwenyekiti wa Jopo la Kimataifa la Sayansi ya Mabadiliko ya Hali ya Hewa na Tabianchi (IPCC) wakati wa kikao cha 69 cha Kamati Kuu Tendaji ya IPCC (Intergovernmental Panel on Climate Change-IPCC (69th IPCC Bureau),tarehe 02 Julai 2025 Jijini Geneva, Uswisi. Kikao hicho kilikuwa na lengo la kujadiliana kuhusu maendeleo ya utoaji wa huduma za hali ya hewa na mipango ya kuendeleza ushirikiano.

Prof. Celeste Saulo ameipongeza TMA kwa uwekezaji mkubwa katika sekta ya hali ya hewa kupitia Serikali hususan katika miundombinu ya kisasa ya hali ya hewa na kwa kuendelea kufanya vizuri katika utoaji wa huduma za hali ya hewa nchini pamoja na kusaidia nchi nyingine katika sekta ya hali ya hewa. Prof. Celeste Saulo ameahidi kuendelea kusaidia katika kuboresha huduma za hali ya hewa na mafunzo kwa wataalamu wa hali ya hewa kupitia programu mbalimbali za WMO ikiwa ni pamoja na eneo la mafunzo ya akili mnemba (Artificial Inteligence-AI). Aidha, Prof. Saulo amesisitiza kuwa, Taasisi za Hali ya hewa za nchi wanachama ndizo zenye jukumu mahsusi la kutoa huduma za hali ya hewa katika nchi Wanachama wa WMO hivyo uwekezaji katika sekta hii utaboresha zaidi huduma hizi kwa jamii.

“ Taasisi za hali ya hewa kama TMA ndizo zenye jukumu mahsusi na chanzo cha kuaminika cha huduma za hali ya hewa kwa mujibu wa miongozo ya WMO na napongeza TMA kwa kuendelea kutumia vyema uwekezaji wa Serikali ya Tanzania kutoa huduma bora za hali ya hewa. Pia napongeza TMA kwa kuwa mstari wa mbele kusimamia vyema programu za WMO na kusaidia nchi nyingine kikanda ili kuboresha zaidi huduma huduma za hali ya hewa katika nchi zao na kikanda” Alisema Prof. Celeste Saulo.

Katika Kikao hicho, Dkt. Ladislaus Chang’a ameeleza dhamira ya TMA ya kuboresha huduma za hali ya hewa na kusimamia vyema programu za WMO zinazotekelezwa nchini na kikanda. 

“TMA itaendelea kutoa wataalamu wake mahiri kuchangia katika utekelezaji wa programu mbalimbali za WMO kwa manufaa ya Dunia nzima na tutaendelea kusaidia wenzetu hasa katika kanda ya Afrika kwa uzoefu wa utaalamu tulio nao, kwa msaada wa WMO na  uwekezaji mkubwa wa Serikali katika tasnia ya hali ya hewa nchini” Alisema Dkt. Chang’a.

Aidha, Dkt. Chang’a alimjulisha Katibu Mkuu wa WMO kuwa, Taasisi za Hali ya Hewa za Nchi wanachama wa WMO ambazo wataalamu wa TMA wametoa msaada wa kiufundi Barani Afrika hivi karibuni ni pamoja na Lesotho, Namibia, Burundi, Zimbabwe na Sudan Kusini, ambapo nchi hizo waliwezeshwa katika maeneo mbalimbali yakiwemo ya uboreshaji wa “Mfumo wa Usimamizi wa Ubora wa huduma (Quality Management System-QMS and Competency Assessment )”, Utabiri wa Hali Mbaya ya Hewa, Utabiri wa Hali ya Hewa kwa Kutumia Modeli za Kihesabu/Kompyuta (Numerical Weather Prediction-NWP)”, “Mchakato wa kisheria katika sekta ya hali ya hewa na Usambazaji wa Huduma za Hali ya Hewa kwa Umma. 


Friday, June 27, 2025

MKUU WA MAKAPTENI ZANZIBAR AELEZEA MIPANGO YA SAFARI INAVYOTEGEMEA TAARIFA ZA HALI YA HEWA.

 





Zanzibar, Tarehe 25 Juni 2025:

Mkuu wa Makapteni Zanzibar, Kapteni Kadadi Hassan Shea, ameelezea namna taarifa za hali ya hewa zinavyowasaidia katika kupanga safari zao baharini na kuepukana na hasara zinazoweza kujitokeza.

Alizungumza hayo kupitia vyombo vya habari alipokuwa ametembelea banda la Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) lililokuwa katika maonesho ya Maadhimisho ya Siku ya Mabaharia Duniani yaliyofanyika katika viwanja vya Mnazi Mmoja, Zanzibar kuanzia Tarehe 22 hadi 25 Juni 2025.

"Taarifa za hali ya hewa zinatusaidia sana katika kufanya mipango ya safari zetu baharini ili kuepusha au kupunguza hasara zinazoweza kujitokeza, mfano kukiwa na utabiri wa uwepo wa upepo mkali huwa tunajipanga kwa kuchukua mizigo kidogo katika kukabiliana nao, na kama kuna utabiri wa uwepo wa mvua tunachukua maamuzi ya kupakia mizigo, kama vile saruji, kwenye makontena," alielezea Kapteni Shea.

Kaptain shea aliongezea kuwa maonesho haya yanawapa fursa Mabaharia kukutana na kufahamiana na taasisi mbalimbali ili kuunganisha nguvu ya pamoja katika kuihudumia jamii kwa usalama na faida zaidi.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa TMA Ofisi ya Zanzibar, Ndg. Masoud Makame Faki, alisema ushiriki wa Mamlaka katika maonesho hayo yanajielezea kupitia kauli mbiu yake inayosema "Bahari Yetu, Wajibu Wetu na Fursa Yetu," ambapo kupitia kipengele cha wajibu wetu TMA inawajibika katika kuelezea namna huduma za hali ya hewa zinavyoweza kusaidia katika kuokoa maisha ya mabaharia, wasafiri na mali kwa ujumla.

Featured Post

DKT. KIJAZI: KIWANGO CHA USAHIHI WA UTABIRI WA MSIMU WA VULI 2019 KIWE CHA JUU ZAIDI.

Mkurugenzi mkuu wa TMA na Makamu wa Tatu wa Rais wa Shirika la Hali ya Hewa Duniani Dkt. Agnes Kijazi (katikati mwenye suti nyeusi) waka...