Monday, November 17, 2025

TANZANIA YAIMARISHA UWEZO WA BURUNDI KATIKA USIMAMIZI WA UBORA WA HUDUMA ZA HALI YA HEWA



30 Oktoba, 2025: Bunjumbura, Burundi

Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA), ikishirikiana na Shirika la Hali ya Hewa Duniani (WMO) na Taasisi ya Hali ya Hewa ya Burundi (IGEBU), ilifanikiwa kufanya mafunzo ya kujenga uwezo wa Mfumo wa Udhibiti wa Ubora (QMS) kwa wafanyakazi zaidi ya arobaini (40) wa IGEBU, mjini Bujumbura, Burundi, kuanzia tarehe 13 hadi 30 Oktoba 2025. Mafunzo hayo yalitolewa na wataalamu wa TMA kupitia mfumo wa ushirikiano wa kimataifa wa huduma za hali ya hewa katika ukanda wa Afrika Mashariki.

Kupitia mpango wa WMO wa Athari za Hali ya Hewa na Mifumo ya Tahadhari ya Mapema Afrika Mashariki (CREWS), mafunzo hayo yalilenga kujenga uwezo wa kitaasisi wa IGEBU ili kuoanisha mifumo yake kwa kiwango cha udhibiti ubora cha ISO 9001:2015. Wataalamu wa QMS kutoka TMA, walitoa mafunzo endelevu kwa wafanyakazi wa IGEBU, kuwaongoza kupitia  ukaguzi wa ndani na mipango ya usimamizi.

Akizungumza wakati wa kufunga mafunzo hayo katika ukumbi wa Chandelier, Bujumbura, Burundi, Mkurugenzi wa Ofisi ya WMO Kanda ya Afrika, Dkt. Agnes Kijazi alipongeza dhamira ya IGEBU na mchango wa Tanzania katika kujenga uwezo wa kikanda.

"Dhamira hii ni ushuhuda wa kile kinachoweza kupatikana kupitia ushirikiano kwa kuwekeza katika mifumo bora, kuimarisha imani katika huduma za hali ya hewa, msingi wa ustahimilivu na maendeleo endelevu." Alisema, Dkt Kijazi.

Katika hatua nyingine, Mkurugenzi wa Taasisi ya Hali ya Hewa ya Burundi (IGEBU), Bw. Deogratius Babonwanayo, alitoa shukrani kwa mafunzo yaliyotolewa na kuthibitisha dhamira ya IGEBU ya kuelekea kwenye Mfumo wa Udhibiti Ubora (QMS). 

Naye Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanania (TMA) na Makamu Mwenyekiti wa Jopo la Kimataifa la Mabadiliko ya Sayansi ya Hali ya Hewa na Tabianchi (IPCC), Dkt. Ladislaus Chang’a alishiriki kwa njia ya mtandao, akithibitisha kuendelea kujitolea kwa TMA katika maendeleo ya kikanda kupitia ushirikiano na kubadilishana ujuzi.

Mafunzo ya QMS yalilenga kuimarisha mifumo ya ndani ya IGEBU na kuimarisha mshikamano wa kikanda katika kutoa huduma za hali ya hewa zenye ubora. Juhudi hizo zinaletwa na msukumo wa kimataifa wa WMO ili kuhakikisha nchi zote zinaweza kutoa taarifa za hali ya hewa zenye ubora kwa wakati, zitakazoaminika na zinazoweza kutekelezeka kwa ajili ya kufanya maamuzi sahihi katika shughuli zote za kijamii na kiuchumi na kulinda maisha ya watu na mali zao.

Friday, November 14, 2025

Tanzania Strengthens Burundi’s Path Toward Quality Management in Meteorological Services: Tanzania–Burundi Partnership in Action

 













30 October 2025, Bujumbura, Burundi

The Tanzania Meteorological Authority (TMA), in close collaboration with the World Meteorological Organization (WMO) and the Institut Géographique du Burundi (IGEBU), successfully concluded a Quality Management System (QMS) capacity-building mission in Bujumbura, Burundi, from 13 to 30 October 2025. This technical assistance, delivered by TMA experts through a South–South cooperation framework, reflects Tanzania’s leadership in advancing operational excellence in meteorological services across East Africa.

Implemented through the WMO Climate Risk and Early Warning Systems (CREWS) East Africa initiative, the mission focused on building the institutional and human capacity of IGEBU to align its processes with the ISO 9001:2015 QMS standard. The TMA delegation, composed of QMS experts Mr. Geofrid Chikojo and Mr. Danford Nyenyema, provided sustained on-the-ground mentorship to IGEBU staff, guiding them through training sessions, internal audit simulations, and management planning.

The closing ceremony, held at Le Chandelier in Bujumbura, was graced by Dr. Agnes Kijazi, Director of the WMO Regional Office for Africa, who praised both IGEBU’s commitment and Tanzania’s contribution to regional capacity-building.

She remarked, “This mission is a powerful testament to what can be achieved through South–South collaboration. By investing in quality systems, we are strengthening trust in our climate and weather services, the cornerstone of resilience and sustainable development.”

In her address, Dr. Kijazi also acknowledged the instrumental role of TMA in supporting peer institutions in the region, noting that such technical missions promote long-term sustainability, standardization, and shared excellence across African National Meteorological and Hydrological Services (NMHSs).

The event was also attended by the Permanent Representative of Burundi with WMO Mr Deogratius Babonwanayo, who expressed appreciation for the support received and reaffirmed IGEBU’s commitment to moving toward QMS certification. The Permanent Representative of Tanzania with WMO and IPCC Vice Chair, Dr. Ladislaus Chang’a participated virtually, reaffirming TMA’s dedication to regional advancement through cooperation and knowledge exchange.

Throughout the mission, IGEBU established a dedicated internal audit team, conducted its first management review meeting, and mobilized over 40 staff members in practical training activities. A comprehensive internal audit simulation was successfully implemented, and a tailored roadmap for ISO 9001:2015 certification was developed.

This QMS mission not only strengthened IGEBU’s internal systems but also reinforced regional solidarity in delivering high-quality, user-oriented meteorological and climate services. The effort aligns with WMO’s global push to ensure that all countries can deliver quality, reliable, timely, and actionable weather and climate information and products  for informed decision making in all socio-economic activities and for protection of life and properties amid growing climate risks.

Monday, October 27, 2025

MWENENDO WA KIMBUNGA “CHENGE” KATIKA ENEO KUSINI MASHARIKI MWA BAHARI YA HINDI

 

Dar es Salaam, 27 Oktoba, 2025 Usiku:

Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) inaendelea kutoa taarifa ya mwenendo wa kilichokuwa Kimbunga “CHENGE” katika katika maeneo ya pwani ya nchi yetu.

 

Kimbunga “CHENGE” kimepoteza nguvu yake na kusambaratika kabisa wakati kikikaribia ukanda wa pwani ya nchi yetu. Hata hivyo, mvua na mawingu yaliyokuwa yakiambatana na kimbunga hicho yamesambaa katika maeneo ya ukanda wa pwani hususan katika mikoa ya Lindi, Pwani, Dar es salaam na Tanga pamoja na visiwa vya Unguja na Pemba na kusababisha vipindi vya mvua katika baadhi ya maeneo hayo. Kwa mfano hadi kufika saa 12 jioni ya leo, kituo cha hali ya hewa kilichopo uwanja wa ndege wa Julius Nyerere Dar es salaam kimeripoti mvua ya milimita 9.1 kwa kipindi cha saa 9 zilizopita. Vilevile katika kipindi hicho, kituo cha hali ya hewa kilichopo katika bandari ya Dar es Salaam kimeripoti mvua ya milimita 3.5.

 

Uchambuzi wa mifumo ya hali ya hewa unaonesha kuwa mabaki ya Kimbunga hicho yanatarajiwa kuendelea kusababisha vipindi vichache vya mvua kwa usiku wa leo tarehe 27 na siku ya kesho 28 ya Mwezi Oktoba, 2025 kwa maeneo ya mikoa ya Pwani, Dar es salaam na Tanga pamoja na visiwa vya Unguja na Pemba na maeneo jirani. Hata hivyo, hakuna madhara makubwa yanayotarajiwa.

 

Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) inaendelea kufuatilia mwenendo wa mabaki ya kimbunga “CHENGE” na athari zake kwa mifumo ya hali ya hewa hapa nchini na itaendelea kutoa taarifa kila inapobidi.

 

USHAURI: Watumiaji wa Bahari na wananchi kwa ujumla wanashauriwa kuendelea kufuatilia na kuzingatia taarifa za utabiri kutoka Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania pamoja na kupata ushauri na miongozo ya wataalam wa kisekta.

Saturday, October 25, 2025

MWENENDO WA KIMBUNGA “CHENGE” KATIKA ENEO LA KUSINI MAGHARIBI MWA BAHARI YA HINDI

 


Dar es Salaam, 25 Oktoba, 2025 Mchana:

Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) inaendelea kutoataarifa ya mwenendo wa Kimbunga “CHENGE katika Bahari ya Hindi, Kaskazini mwa Kisiwa cha Madagascar

 

Kimbunga “CHENGE” kimeendelea kusalia baharini nakusogea kuelekea magharibihuku kikipungua nguvu yake. Hadi asubuhi ya leo kilikuwa katika eneo la Bahari umbali watakribani kilometa 1,280 Mashariki mwa pwani ya kisiwa cha Mafia.

 

Uchambuzi wa mifumo ya hali ya hewa unaonesha kuwaKimbunga hicho kinatarajiwa kuendelea kusogea kuelekeaMagharibi zaidi mwa Bahari ya Hindi ulipo ukanda wa pwaniwa nchi yetu huku kikiendelea kupungua nguvu yake kadrikinavyosogeaHali hiyo inatarajiwa kusababisha uwezekanomdogo wa ongezeko kidogo la kasi ya upepo na mawimbimakubwa ya Bahari kati ya tarehe 26 hadi 28 ya Mwezi Oktoba, 2025 kwa maeneo ya ukanda wa pwani ya nchi yetuVilevileupo uwezekano mdogo wa vipindi vichache vya mvua kubwa kujitokeza hususani katika maeneo ya visiwa vyaUnguja na Pemba pamoja na mikoa ya Morogoro, Pwani, Dar es salaam na Tanga na maeneo jirani katika kipindi hicho cha tarehe 26 na 28 ya Mwezi Oktoba 2025.

 

Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) inaendeleakufuatilia mwenendo wa kimbunga CHENGE na athari zakekwa mifumo ya hali ya hewa hapa nchini na itaendelea kutoataarifa kila inapobidi.

 

USHAURI: Watumiaji wa Bahari na wananchi kwa ujumlawanashauriwa kuendelea kufuatilia na kuzingatia taarifa za utabiri kutoka Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania pamoja na kupata ushauri na miongozo ya wataalam wakisekta.

Featured Post

DKT. KIJAZI: KIWANGO CHA USAHIHI WA UTABIRI WA MSIMU WA VULI 2019 KIWE CHA JUU ZAIDI.

Mkurugenzi mkuu wa TMA na Makamu wa Tatu wa Rais wa Shirika la Hali ya Hewa Duniani Dkt. Agnes Kijazi (katikati mwenye suti nyeusi) waka...