Wednesday, October 16, 2024

FIRST MEETING OF PROJECT STEERING COMMITTEE FOR THE SOFF IMPLEMENTATION IN TANZANIA.









Morogoro, Tanzania; 16th October 2024.

The Project Steering Committee (PSC) of the Systematic Observation Financing Facility (SOFF) Implementation in Tanzania held its first meeting on Wednesday, 16th October 2024 at Morena Hotel Morogoro, reviewing and approving tools and documents for efficient and effective implementation of the (SOFF) Project - investment phase in Tanzania in accordance with project objectives, budget and timeline

During the opening session, the acting Director General of Tanzania Meteorological Authority (TMA), Permanent Representative of Tanzania with the world Meteorological  Organization (WMO) and the Vice Chair of the Intergovernmental Panel on Climate Change (IPCC), Dr. Ladislaus Chang'a thanked members of PSC for accepting to be part of the National Level SOFF - PSC, which will oversee the project Implementation in Tanzania, he also expressed his gratitude to the SOFF Secretariat and WMO for recommending Tanzania to be part of SOFF funding beneficiary.

''Your acceptance demonstrates your commitment to enhancing weather and climate data for resilience to support sustainable socio-economic development of the country, regional level and globally”. Emphasized Dr. Chang'a when addressing the members.

In addition, Dr. Chang'a said establishment of the SOFF project will address the data gap and international exchange of weather and climate data by providing technical and financial assistance to meet the Global Basic Observation Network (GBON) requirements.

Earlier on his remarks, the Resident Representative of United Nation Development Programme (UNDP) in the United Republic of Tanzania, Mr. Shigeki Komatsubara congratulated the TMA leadership and experts for their commitment to excellence that keep Tanzania at the forefront of climate adaptation and resilience effort.

He also emphasized that SOFF project will provide continuous operational and maintenance support for TMA and ensuring that Tanzania weather stations are effectively maintained long after the project has ended, Mr. Komatsubara insisted “UNDP is fully committed to this effort and stands ready to provide the necessary support to see this project through to its successful completion”.

On the other hand, the representative from United Nations Environment Programme (UNEP), Ms. Clara Makenya underscored the importance of collaborative efforts in addressing various environmental challenges, including in strengthening climate actions. She emphasized the need for ensuring the project implementation aligns with international standards and best practice since UNEP serves as a global leader in environmental governance, advocating for sustainable development.

SOFF is a fundamental component of the Early Warning for All initiative, acting as a delivery mechanism that enables countries to meet GBON standards. In Tanzania, it represents a vital opportunity to enhance meteorological infrastructure. Spanning from July 2024 to December 2027, the project is set to invest approximately USD 9 million provided by the United Nations Multi-Partner Trust Fund (UNMTPF).

KAMATI TENDAJI YA MRADI WA SOFF YAKUTANA KUIDHINISHA MPANGO KAZI WA UTEKELEZAJI WA MRADI TANZANIA.

 








Morogoro, Tanzania; 16 Oktoba 2024.
Kamati Tendaji ya Utekelezaji wa Mradi wa Mfuko wa Umoja wa Mataifa wa Kuimarisha Uangazi wa Hali ya Hewa (SOFF) imekutana kwa mara kwanza katika ukumbi wa hoteli ya Morena, Morogoro, tarehe 16 Oktoba 2024, ikiwa na lengo la kupitia na kuidhinisha nyaraka muhimu za kuanza rasmi utekelezaji wa Mradi huo nchini Tanzania.

Wakati wa ufunguzi wa kikao hicho, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA), Mwakilishi wa Kudumu wa Tanzania katika Shirika la Hali ya Hewa Duniani (WMO) na Makamu Mwenyekiti wa Jopo la Kimataifa la Sayansi ya Mabadiliko ya Hali ya Hewa na Tabianchi (IPCC), Dkt. Ladislaus Chang'a aliwashukuru wajumbe wa kamati tendaji kwa kukubali kuwa sehemu ya kusimamia utekelezaji wa Mradi wa SOFF Tanzania. Aidha, Dkt. Chang’a alitoa shukrani zake za dhati kwa Sekretarieti ya SOFF na WMO kwa kuichagua Tanzania kuwa miongoni mwa wanufaika wa ufadhili wa fedha za Mfuko huo takribani dola za kimarekani milioni 9.

"Uwepo wenu ni ushahidi tosha wa dhamira yenu ya kusaidia kuboresha huduma za hali ya hewa kwa nchi yetu, kikanda na Duniani kote, huduma ambazo zitaenda kusaidia shughuli mbalimbali za kijamii na kiuchumi”, alisema Dkt. Chang'a.

Aidha, Dkt. Chang'a aliongeza kuwa uanzishwaji wa mradi wa SOFF utasidia nchi kukabiliana na changamoto ya upatikanaji wa data za hali ya hewa na mfumo wa mawasiliano wa ubadilishanaji wa data hizo kimataifa kwa kuwezesha masuala ya muhimu ya kiufundi na kifedha.

Kwa upande wake, Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) nchini, Ndg. Shigeki Komatsubara alieleza jinsi anavyoridhishwa na uongozi mzuri na utendaji kazi wa TMA na wataalamu wake kwa ujumla, na kuifanya Tanzania kuwa mfano wa kuigwa katika bara la Afrika.

Aidha, alisisitiza kuwa mradi wa SOFF utatoa msaada endelevu wa uendeshaji na matengenezo na usimamizi kwa vituo vya hali ya hewa vitakavyojengwa kuwa katika hali nzuri na endelevu kwa muda mrefu kwa kuwa UNDP imejipanga kikamilifu katika kufikia malengo na mafanikio hayo.

Naye Mwakilishi kutoka Shirika la Mazingira la Umoja wa Mataifa (UNEP), Bi Clara Makenya aliendelea kusisitiza umuhimu mkubwa wa kuimarisha ushirikiano katika kukabiliana na changamoto za mabadiliko ya hali ya hewa na kuimarisha huduma za hali ya hewa. Bi Clara pia alifafanua jukumu la UNEP katika kufanikisha mradi huo, ikiwa ni pamoja na kusimamia viwango vya ubora katika utekelezaji wa mradi hususan eneo la mazingira kwa kuratibu na kutoa ushauri pale inapobidi kwa maendeleo endelevu ya nchi na dunia kwa ujumla.


Monday, October 7, 2024

TANZANIA YAWA MWENYEJI WA MKUTANO WA MAFUNZO YA MIFUMO YA UANGAZI WA HALI YA HEWA DUNIANI KWA NCHI ZA KANDA YA AFRIKA MASHARIKI NA KASKAZINI.


 









7 Oktoba, 2024, Dar es Salaam: 

Tanzania kupitia Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) kwa kushirikiana na Shirika la Hali ya Hewa Duniani (WMO) imekuwa Mwenyeji wa mkutano wa Mafunzo ya WMO kwa wataalamu wa hali ya hewa kutoka nchi Wanachama wa WMO Kanda ya Afrika Mashariki na Kaskazini. Lengo likiwa ni kuwajengea uwezo wataalamu wa Hali ya Hewa wanaofanya kazi katika vituo hivyo vya “WMO Regional WIGOS Centres (RWCs)”  vya kanda ya Afrika Mashariki na Kaskazini Afrika. 

Akifungua rasmi mafunzo hayo yanayofanyika katika Hoteli ya Four Points by Sheratons,kuanzia tarehe 7-11 Oktoba, 2024,  Mgeni rasmi na Mwenyekiti wa Bodi ya TMA, Mhe. Jaji Mshibe Ally Bakari alisema suala muhimu kwa Taasisi za Hali ya Hewa za Afrika ni kuimarisha upatikanaji wa taarifa za hali ya hewa zenye ubora kwa maendeleo ya kijamii na kiuchumi, hivyo mafunzo hayo yatasaidia kuboresha zaidi shughuli zinazofanywa, ikiwa ni pamoja na kuboresha mtandao wa kubadilishana data ili kuboresha zaidi utabiri wa matukio ya hali mbaya ya hewa katika nchi wanachama wa WMO.

Aidha, Jaji Mshibe aliishukuru Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuendelea kuwekeza katika uboreshaji wa miundo mbinu ya huduma za hali ya hewa. Jaji Mshibe aliwashukuru pia WMO na washirika wengine kwa jitihada zao za kuimarisha huduma za hali ya hewa barani Afrika, ikiwemo kuanzisha mfuko wa uwezeshaji wa huduma za uangazi wa hali ya hewa ambapo kupitia jitihada hizo, kiasi cha dola za kimarekani milioni 9 zimeidhinishwa kuboresha huduma za hali ya hewa nchini Tanzania.

Awali, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TMA na Mwakilishi wa kudumu wa WMO, ambaye pia ni Makamu Mwenyekiti wa Jopo la Kimataifa la Sayansi ya Mabadiliko ya Hali ya Hewa na Tabianchi, Dkt. Ladislaus Chang’a, alieleza umuhimu wa kuimairsha uangazi na kuongeza upataikanaji wa data kwa ajili ya kuimairsha utoaji wa tahadhari za matukio ya hali mbaya ya hewa na kukabiliana na changamoto ya mabadiliko ya hali ya hewa. Aidha Dkt. Chang’a alieleza kuwa Tanzania kupitia TMA imejipanga kuendelea kushiriki katika kuongoza na kuwa kinara katika baadhi ya jitihada za kuimarisha huduma za hali ya hewa Barani Afrika. “ Tumejiandaa vyema kuwa mwenyeji wa Mkutano huu mkubwa wa Kikanda, na pia kama mwenyeji wa Kituo cha mfumo wa Kidunia wa  kufuatilia vituo vya uangazi wa hali ya hewa kwa nchi za Afrika Mashariki” alisema Dkt. Chang’a. TMA itawasilisha mada zenye kueleza uzoefu wake katika utekelezaji wa jukumu hilo. 

Kwa upande wake, Mwakilikishi kutoka WMO alisema kumekuwa na changamoto ya matukio mbalimbali ya Hali mbaya ya Hewa hivyo ushirikiano wetu utasaidia katka kutoa tahadhari za mapema juu ya matukio ya Hali mbaya ya Hewa na tahadhali za mapema”.Alisema, Abubakari Salih Babiker

Washiriki wa mkutano huo wametoka Taasisi za Hali ya Hewa za nchi za Tanzania, Tunisia, Algeria, Egypt, Sudan, South Sudan, Kenya, Uganda, Rwanda, Burundi, Somalia, Ethiopia, Djibouti, Madagascar, Comoros, Sychelles, Mauritius, Morocco, Afrika Kusini na waalikwa kutoka Oman na Sekretarieti ya Shirika la Hali ya Hewa Duniani.

Thursday, September 12, 2024

MHE. MWIGULU: SERIKALI ITAENDELEA KUIPA KIPAUMBELE TMA

 



12 Septemba 2024, Arusha: Waziri wa Fedha, Mhe. Mwigulu Lameck Nchemba ameipongeza Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) na kuahidi kuwa Serikali kupitia Wizara ya Fedha itaendelea kuipa kipaumbele kwa kuwa huduma za hali ya hewa zinasaidia katika mipango mbalimbali ya maendeleo.

“Wataalam wa hali ya hewa mnafanya kazi nzuri, utabiri unaotolewa hivi sasa ni wa usahihi na umesaidia sana katika masuala ya kiuchumi na kijamii na mipango ya nchi kwa ujumla”. Alizungumza Dkt. Mwigulu alipotembelea banda la TMA katika viwanja vya AICC, Arusha wakati akifunga rasmi Jukwaa la 16 la Ununuzi la Afrika Mashariki. 

Matumizi sahihi ya huduma za hali ya hewa ni suala mtambuka kwani husaidia katika mipango na uendeshaji wa shughuli za kiuchumi na kijamiii hususani katika kupunguza madhara yatokanayo na hali mbaya ya hewa kwa umma

Wednesday, September 11, 2024

TMA YASISITIZA UMUHIMU WA MATUMIZI YA HUDUMA ZA HALI YA HEWA KWA WADAU WA UNUNUZI













 10 Septemba 2024, Arusha:

Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imetoa elimu kwa wadau mbalilmbali wa Ununuzi kuhusu matumizi sahihi ya huduma za hali ya hewa pamoja na kuchangia gharama za upatikanaji wa huduma hizo katika utekelezaji wa miradi mbalimbali ya ujenzi nchini. 

Hayo yalizungumzwa na Mkurugenzi wa Huduma za Utabiri, Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA), Dkt. Hamza Kabelwa katika mada aliyoiwasilisha katika Jukwaa la 16 la Ununuzi la Afrika Mashiriki katika Ukumbi wa AICC, Arusha, linalofanyika tarehe 09 hadi 12 Sepetemba, 2024.

Dkt. Kabelwa alieleza kuwa, kiasi kikubwa cha matumizi ya fedha kinahusisha ununuzi, ni vyema huduma za hali ya hewa zikapewa kipaumbele katika utekelezaji wa Mipango ya Ununuzi na miradi mbalimbali ya maendeleo nchini ili kuongeza thamani ya fedha katika mradi. “Kwa kipindi cha hivi karibuni tumeshuhudia miradi mingi ikisimama kutokana na madhara yatokanayo na hali mbaya ya hewa, ni muda muafaka sasa wadau wanaohusika kuhakikisha wanatumia huduma hizo wakati wa ubunifu na kabla ya kuanza utekelezaji wa miradi yao”. Alisisitiza Dkt. Kabelwa.

Aidha, washiriki walijulishwa kwamba, huduma hizo mahsusi zinahitaji kuchangiwa gharama kidogo ambazo ziliwasilishwa rasmi katika hotuba ya Waziri wa Fedha ya Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa mwaka 2024/25, kifungu cha 158 ilikieleza mapendekezo ya mabadiliko ya kufanya marekebisho ya Sheria ya Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania, sura 157 kuhusu Ada za Hali ya hewa kwa usalama wa uendeshaji wa Miradi ya Ujenzi. Lengo likiwa ni kuongeza tija na ufanisi wa utendaji kazi na kuimarisha usalama wa watu na mali.

Katika hatua nyingine, wataalaam kutoka TMA kupitia maonesho yanayoendelea katika viwanja vya AICC, walieleza pia huduma za hali ya hewa zinahitaji uwekezaji wa miundombinu ya kisasa na gharama kubwa za uendeshaji ili kuwezesha utoaji wa huduma bora, hivyo ni vyema kwa wadau mbalimbali kujitokeza kutumia huduma hizo sambamba na kuchangia gharama kidogo ya huduma mahsusi.

Saturday, September 7, 2024

TMA YAWAKUMBUSHA WAHANDISI KUZINGATIA HUDUMA ZA HALI YA HEWA KATIKA UTEKELEZAJI WA MIRADI

 








06 Septemba 2024, Dar es Salaam: 

Wahandisi nchini wamekumbushwa umuhimu wa huduma za hali ya hewa sambamba na kuchangia gharama za upatikanaji wa huduma hiyo katika utekelezaji wa miradi yao. Hayo yalizungumzwa na Mkurugenzi wa Huduma za Utabiri, Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA), Dkt. Hamza Kabelwa katika mada iliyowasilishwa katika Mkutano wa  21 wa Wahandisi uliyojumuisha wahandisi wa ndani na nje ya nchi katika Ukumbi wa Mlimani City, Dar es Salaam, tarehe 05 hadi 06 Sepetemba, 2024.

Dkt. Kabelwa alieleza kuwa, katika hotuba ya Waziri wa Fedha ya Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa mwaka 2024/25, kifungu cha 158 ilijumuisha mapendekezo ya mabadiliko ya kufanya marekebisho ya sheria ya Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania, sura 157 kuhusu Ada za Hali ya hewa kwa usalama wa uendeshaji wa miradi ya ujenzi. “Lengo la hatua hiyo ni kuongeza mapato yatakayowezesha utoaji wa huduma mahsusi za hali ya hewa ili kuongeza tija na ufanisi wa utendaji kazi na kuimarisha usalama wa watu na mali katika maeneo ya miradi ya ujenzi, ambapo mchakato wa upatikanaji wa huduma hizo unahitaji uwekezaji wa miundombinu ya kisasa na gharama kubwa za uendeshaji”. Alifafanua Dkt. Kabelwa. 




Monday, August 26, 2024

TANZANIA YAWANOA WATAALAMU WA HALI YA HEWA AFRIKA KUHUSU MATUMIZI YA RADA ZA HALI YA HEWA.












26 Agosti 2024, Mwanza, Tanzania: 

Katika kuwajengea uwezo wataalamu wa hali ya hewa kutoka Taasisi za Hali ya Hewa barani Afrika, Kitengo cha Elimu na Mafunzo cha Shirika la Hali ya Hewa Duniani kwa kushirikiana na Chuo cha Taifa cha Hali ya Hewa kinachoendeshwa na Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA), wameandaa mafunzo mahsusi ya matumizi ya data na taarifa za Rada za Hali ya HewaMafunzo hayo yanafanyika katika Ukumbi wa Malaika,Mwanza, tarehe 26 hadi 30 Agosti 2024.

Akifungua rasmi mafunzo hayo, Waziri wa Uchukuzi, Mhe. Prof. Makame Mnyaa Mbarawa (Mb); alieleza lengo la mafunzo hayo ni kuimarisha zaidi uwezo wa wataalamu wa hali ya hewa na wataalam wengine husika kutoka baadhi ya Nchi za Afika Mashariki na Kusini mwa Afrika katika matumizi bora ya taarifa za Rada za hali ya hewa kwa ajili ya kuboresha utabiri wa hali ya hewa na utoaji wa tahadhari za matukio ya hali mbaya ya hewa kwa jamii.

Aidha, alieleza kuwa mafunzo hayo yanaendana na utekelezaji wa mpango ulioasisiwa na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa wa utoaji wa Tahadhari kwa Wote (Early Warning for All EW4ALL) ifikapo mwishoni mwa mwaka 2027, pamoja na Sera ya Shirika la Hali ya Hewa Duniani (WMO) ya ubadilishanaji wa data za hali ya hewa Kimataifa (“WMO Unified Data Policy”). Mafunzo hayo yana umuhimu mkubwa kwa nchi wanachama wa WMO kanda ya Afrika (WMO RA1) katika kuongeza uwezo unaohitajika zaidi wa utoaji wa huduma za hali ya hewa na tahadhari kupitia taasisi za hali ya hewa za nchi husika kukabiliana na ongezeko la idadi na ukubwa wa matukio ya hali mbaya ya hewa katika muktadha wa mabadiliko ya hali ya hewa na hivyo kuchangia kuokoa maisha ya watu na mali zao.

Alisisitiza umuhimu wa kufanya uwekezaji wa miundo mbinu ya kisasa ya hali ya hewa kama vile rada, akifafanua kuwa Tanzania imekuwa kilelezo bora katika kufanya uwekezaji huo pamoja na kuwajengea uwezo wataalamu wa hali ya hewa nchini, na hivyo kuchochea fursa ya kuandaa mafunzo hayo.

Awali, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TMA na Mwakilishi wa kudumu wa WMO, ambaye pia ni Makamu Mwenyekiti wa Jopo la Kimataifa la Sayansi ya Mabadiliko ya Hali ya Hew ana Tabianchi, Dkt. Ladislaus Chang’a, alieleza kuwa TMA imejiandaa vyema kupitia wataalamu wake katika kutoa mafunzo hayo “Wataalamu watakao toa mafunzo ni wabobezi, na kati yao wamepata mafunzo kutoka Marekani na Finland na vilevile ni wakufunzi kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam”. Alisema Dkt. Chang’a.

Kwa upande wake, Mwakilikishi kutoka WMO (Ofisi ya Mafunzo), Bi. Eunjin CHOI aliishukuru Serikali ya Tanzania kwa kufanikisha mafunzo hayo muhimu ya matumizi ya taarifa na data za rada za hali ya hewa. “Kupitia ushirikiano huu, kwa pamoja tunaweza kuendeleza malengo yetu ya kuboresha huduma za hali ya hewa, si tu kwa Tanzania bali duniani kote”. Alisisitiza Bi. Eunjin.

Tanzania inatoa mafunzo kwa wataalamu wa hali ya hewa kutoka baadhi ya nchi Wanachama wa Shirika la Hali ya Hewa Duniani (WMO) kanda ya Afrika ambao ni Burundi, Comoro, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Kenya, Msumbiji, Malawi, Mauritius, Rwanda, Seychelles, Sudan Kusini, Uganda, Tanzania na Zambia.

Featured Post

DKT. KIJAZI: KIWANGO CHA USAHIHI WA UTABIRI WA MSIMU WA VULI 2019 KIWE CHA JUU ZAIDI.

Mkurugenzi mkuu wa TMA na Makamu wa Tatu wa Rais wa Shirika la Hali ya Hewa Duniani Dkt. Agnes Kijazi (katikati mwenye suti nyeusi) waka...