Friday, July 12, 2019

MAMENEJA WA TMA WATAKIWA KUWEKA MIKAKATI BORA YA MAWASILIANO YA HUDUMA ZA HALI YA HEWA.





Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) Dkt. Ladislaus Chang’a  katika picha ya pamoja na washiriki wa warsha ya mafunzo ya mawasiliano ya kimkakati ya huduma za hali ya hewa kwa jamii, tarehe 11/07/2019, Kibaha, Pwani


Mameneja kutoka Ofisi za Kanda za Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) wametakiwa kuhakikisha wanaweka mikakati bora ya mawasiliano ya huduma za hali ya hewa katika kanda zao.


Maelekezo hayo yalitolewa na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TMA Dkt. Ladislaus Chang’a wakati wa ufunguzi wa warsha ya mafunzo ya mawasiliano ya kimkakati ya huduma za hali ya hewa kwa jamii ,yaliyoandaliwa kwaajili ya kuwajengea uwezo wakuu hao wa vituo vya kanda jinsi ya kuwasiliana kwa njia bora na rahisi. Mafunzo hayo yalifanyika Kibaha, Pwani tarehe 10-11 Julai 2019, na kuwakutanisha mameneja kutoka ofisi za kanda-TMA, wataalam wa hali ya hewa kutoka Kituo Kikuu cha Utabiri (CFO) na mtaalam wa mawasiliano kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu.

‘Mtakapo fikia mwisho wa mafunzo haya, nahitaji kupata mikakati bora ya mawasiliano ya huduma zetu katika maeneo ya kazi (kanda) zenu yenye lengo la kuboresha usambazaji wa taarifa za hali ya hewa na hivyo kuchangia nchi yetu kufika malengo ya Serikali ya uchumi wa kati’, alisema Dkt. Chang’a


Aidha, aliendelea kwa kuwataka viongozi hao wa Mamlaka kuhakikisha wanaboresha utendaji wao wa kazi kwa kuongeza juhudi kwenye kila kinachofanyika hususani njia mahususi za kuwafikia wadau na jamii kwa ujumla.

Warsha hiyo ya mafunzo imeandaliwa na TMA kwa udhamini wa ‘Department for International Development (DFID)’ kupitia mradi wa Weather and Climate Information services for Africa (WISER), wenye lengo la kuimarisha upatiakanaji, usambazaji na matumizi ya taarifa za hali ya hewa.

IMEANDALIWA NA;
OFISI YA UHUSIANO
MAMLAKA YA HALI YA HEWA TANZANIA (TMA)

 

 

No comments:

Post a Comment

Featured Post

DKT. KIJAZI: KIWANGO CHA USAHIHI WA UTABIRI WA MSIMU WA VULI 2019 KIWE CHA JUU ZAIDI.

Mkurugenzi mkuu wa TMA na Makamu wa Tatu wa Rais wa Shirika la Hali ya Hewa Duniani Dkt. Agnes Kijazi (katikati mwenye suti nyeusi) waka...