Tuesday, June 25, 2019

WADAU PEMBA KUSINI WAPATA ELIMU YA MATUMIZI SAHIHI YA HUDUMA ZA HALI YA HEWA MAJINI





Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imeendesha warsha maalum kwa wadau kutoka sekta mbalimbali kisiwani Pemba  kuhusu huduma za hali ya hewa katika bahari ya Hindi ili kuboresha uelewa wa matumizi sahihi  ya taarifa zitolewazo na TMA.

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa warsha hiyo, mgeni rasmi Mhe. Hemed Suleiman Abdala ambaye pia ni mkuu wa mkoa Pemba Kusini aliwataka washiriki kutambua lengo la semina ni pamoja na kupata uelewa wa matumizi sahihi ya utabiri wa hali ya hewa na tahadhari za kila siku zinazotolewa na TMA  ili kukidhi malengo ya huduma hizo nchini.
Katika hotuba yake mgeni rasmi alisisitiza kwa kutambua mchango mkubwa toka TMA katika kuboresha uelewa wa wadau toka katika sekta mbalimbali hapa nchini juu ya matumizi sahihi ya taarifa za hali ya hewa
na kufurahishwa na hatua ya kufika kisiwani Pemba.
 “Napenda kuishukuru na kuipongeza TMA kwa kuandaa na kufanikisha warsha hii muhimu kufanyika kisiwani Pemba kwani  itasaidia kutuepusha na maafa hususani wavuvi, hasa wale wachache wanaofanya shughuli zao kwa mazoea na kupelekea kukumbwa na maafa” alisema mkuu wa mkoa wa Pemba.

Aidha alimalizia kwa kuwataka washiriki wawe mabalozi wazuri katika maeneo yao ya kazi kwa kutoa elimu hiyo muhimu ambayo itasaidia kujiepusha na maafa yanayoweza kujitokeza.

IMETOLEWA NA OFISI YA UHUSIANO
MAMLAKA YA HALI YA HEWA TANZANIA

No comments:

Post a Comment

Featured Post

DKT. KIJAZI: KIWANGO CHA USAHIHI WA UTABIRI WA MSIMU WA VULI 2019 KIWE CHA JUU ZAIDI.

Mkurugenzi mkuu wa TMA na Makamu wa Tatu wa Rais wa Shirika la Hali ya Hewa Duniani Dkt. Agnes Kijazi (katikati mwenye suti nyeusi) waka...