Saturday, March 23, 2019

BARAZA: WAZIRI KAMWELWE AIPONGEZA TMA KWA KUFANIKIWA KUPATA SHERIA MPYA ILIYOSAINIWA NA MHE RAIS.

Mhe. Isack Kamwelwe katika picha ya pamoja na menejiment ya TMA
Mhe. Isack Kamwelwe katika picha ya pamoja na wajumbe wa baraza la wafanyakazi wa TMA

Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Mhe. Mhandisi Isack Kamwelwe ameipongeza Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania(TMA) kwa kufanikiwa kupata sheria mpya ya huduma za hali ya hewa nchini. Waziri Kamwelwe alizungumza hayo wakati akilifungua rasmi Baraza la Wafanyakazi wa TMA, tarehe 22 Machi 2019.

‘Napenda kutumia nafasi hii kipekee kabisa kuipongeza Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania chini ya uongozi wa Wizara yangu kwa sheria iliyopitishwa na Bunge la jamhuri ya Muungano wa Tanzania mwezi Januari, 2019 na kusainiwa na Mhe. Raisi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuri’.  Alizungumza mhe. Kamwelwe

Mhe Kamwele aliongezea kwa kusema sheria hii inaipa TMA mamlaka kamili ya kutoa huduma na kuhakiki shughuli zote zinazohusiana na hali ya hewa katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa TMA, Dkt. Agnes Kijazi alimshukuru mhe waziri kwa kukubali kufungua baraza la wafanyakazi wa TMA na kuelezea madhumuni ya baraza hilo.

‘Madhumuni makuu ya Baraza hili ni kupokea, kujadili na kupitisha mapendekezo ya bajeti ya Mamlaka kwa kipindi cha mwaka wa fedha 2019/2020’. Alizungumza Dkt. Kijazi

‘Aidha, mapendekezo hayo ya bajeti yanazingatia vipaumbele vitakavyo iwezesha Mamlaka kufikia malengo yake na kuongeza ubora na ufanisi katika utoaji wa  huduma za hali ya hewa kwa umma kwa lengo la kupunguza athari za hali mbaya ya hewa na hivyo kuchangia katika kukuza pato la Taifa’. Aliongezea Dkt. Kijazi


No comments:

Post a Comment

Featured Post

DKT. KIJAZI: KIWANGO CHA USAHIHI WA UTABIRI WA MSIMU WA VULI 2019 KIWE CHA JUU ZAIDI.

Mkurugenzi mkuu wa TMA na Makamu wa Tatu wa Rais wa Shirika la Hali ya Hewa Duniani Dkt. Agnes Kijazi (katikati mwenye suti nyeusi) waka...