Sunday, February 10, 2019

WATAALAMU WA HALI YA HEWA KUHAKIKISHA USAHIHI WA UTABIRI WA MVUA ZA MASIKA UNAKUWA WA HALI YA JUU


Katikati ya waliokaa ni mkurugenzi mkuu wa Mamlaka ya Hali ya Hewa dkt. Agnes Kijazi kwenye picha ya pamoja na wataalam wa hali ya hewa, wakati akifungua warsha ya wataalamu wa hali ya hewa katika kuandaa utabiri wa mvua za msimu wa Masika (Machi hadi Mei 2019).





Matukio mbalimbali kwa picha wakati wataalam wa hali ya hewa wakichambua mifumo ya hali ya hewa katika maandarizi ya utabiri wa hali ya hewa kwa msimu wa masika (Machi hadi Mei 2019)

Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) Dkt. Agnes Kijazi amewata wataalam wa hali ya hewa kutumia utalaam wao walionao kuhakikisha maandalizi ya utabiri wa hali ya hewa kwa msimu wa mvua za masika (Machi hadi Mei2019) unaendelea kuwa sahihi zaidi katika kiwango cha juu na wenye ubora utakaosaidia maendeleo ya kiuchumi katika taifa letu. Dkt. Kijazi alizungumza hayo wakati wa kufungua warsha ya wataalamu wa hali ya hewa katika kuandaa utabiri huo. 
 Warsha hiyo itafuatiwa na warsha ya wataalamu mabingwa wote wa hali ya hewa pamoja warsha ya wadau wa huduma za hali ya hewa na warsha ya wanahabari kabla ya kutoa  rasmi mwelekeo wa msimu wa mvua za MASIKA 2019 tarehe 14 Februari 2019.

No comments:

Post a Comment

Featured Post

DKT. KIJAZI: KIWANGO CHA USAHIHI WA UTABIRI WA MSIMU WA VULI 2019 KIWE CHA JUU ZAIDI.

Mkurugenzi mkuu wa TMA na Makamu wa Tatu wa Rais wa Shirika la Hali ya Hewa Duniani Dkt. Agnes Kijazi (katikati mwenye suti nyeusi) waka...