Wednesday, February 13, 2019

WANAHABARI NA WATAALAM WA HALI YA HEWA WAKAA MEZA MOJA KUJADILI UTABIRI WA MVUA ZA MASIKA.

Washiriki wa warsha ya wanahabari kuhusu msimu wa mvua za masika,  mwezi Machi hadi Mei 2019 katika picha ya pamoja


Tarehe 13 Februari 2019

Ikiwa ni mwendelezo wa ushirikishwaji wa wadau mbalimbali katika kuhakikisha huduma za hali ya hewa zinawafikia wananchi kwa wakati na kwa lugha inayoeleweka. Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imekutana na wanahabari kutoka vyombo mbalimbali vya habari nchini kujadili mwelekeo wa msimu wa mvua za MASIKA kwa 2019 kabla ya kutolewa rasmi kwa umma tarehe 14 Februari 2019.

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa mkutano huo katika ukumbi wa mikutano wa ‘Law School’, Dkt. Ladislaus Chang’a ambaye ni Mkurugenzi wa Utafiti na Matumizi ya tarifa za hali ya hewa wa TMA alisema kuwa dhamira ya kukutana na wanahabari ni muendelezo wa dhamira na utaratibu wa TMA wa kuimarisha ushilikishwaji na kuendelea kuwajengea uwezo wanahabari ili wazielewe vizuri zaidi taaarifa za hali ya hewa na hususani utabiri na hivyo waweze kuzifikisha taarifa, kuhabarisha na kuelimisha jamii kwa ufasaha na ufanisi zaidi.

Aidha wanahabari walitumia fursa hiyo kujadili na kutoa mapendekezo ya kuboresha ufungashwaji na usambazaji wa tarifa za hali ya hewa ili ziendelee kuwafikia walengwa kwa wakati na kwa ufasaha zaidi. Pia walielezea umuhimu wa kuwajengea uwezo wanahabari kuzielewa kwa kina tarifa za hali ya hewa na mabadiliko yake.

Mkutano huo wa siku moja umeandaliwa chini ya mwamvuli wa Awamu ya Pili ya Programu ya Kidunia ya Utoaji wa Huduma za Hali ya Hewa ya GFCS yaani “Global Framework for Climate Services Adaptation Programme in Africa (APA) II” hapa Tanzania yenye lengo la kuimarisha huduma za hali ya hewa katika nyanja ya utoaji, usamabazaji na utumiaji wa huduma hizo. Mkutano huu ulijumuisha wanahabari kutoka kwenye vituo vya televisheni, redio, magazeti, blogs na mitandao ya kijamii

IMETOLEWA NA MONICA MUTONI
OFISI YA UHUSIANO
MAMLAKA YA HALI YA HEWA TANZANIA

No comments:

Post a Comment

Featured Post

DKT. KIJAZI: KIWANGO CHA USAHIHI WA UTABIRI WA MSIMU WA VULI 2019 KIWE CHA JUU ZAIDI.

Mkurugenzi mkuu wa TMA na Makamu wa Tatu wa Rais wa Shirika la Hali ya Hewa Duniani Dkt. Agnes Kijazi (katikati mwenye suti nyeusi) waka...