Thursday, February 28, 2019

KAMWELE APONGEZA UTENDAJI KAZI MAMLAKA YA HALI YA HEWA TANZANIA (TMA)

Matukio mbalimbali kwa picha wakati Mhe. Kamwele akitembelea vitengo mbalimbali vya Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA)


Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Mhe. Mhandisi. Isack Kamwele amepongeza utendaji kazi wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA). Mhe. Kamwele alitoa pongezi hizo wakati alipotembelea Ofisi za TMA, Ubungo Plaza, Dar es Salaam, tarehe 27 Februari  2019 na alipata taarifa ya utendaji kazi wa mamlaka na kutembelea baadhi ya sehemu za kazi kabla ya kuzungumza na wafanyakazi. Mhe. Kamwele alipokelewa na uongozi na menejiment ya TMA, ikiongonzwa na mwenyekiti wa bodi ya ushauri Dkt. Buruhani Nyenzi na kaimu mkurugenzi mkuu Dkt. Ladislaus Chang’a.

“Nawapongeza TMA kwa umakini na utekelezaji wa majukumu yenu, nakiri kusema ni moja ya taasisi makini kati ya taasisi zilizo chini ya wizara yangu nilizo tembelea”. Alizungumza mhe. Kamwele

Aidha, mhe. Kamwele alisisitiza kuboresha mfumo wa ushirikishwaji wa wadau na usambazaji wa taarifa za hali ya hewa, akitolea mfano mafuriko yaliyo bomoa barabara eneo la Dumila, kuwa baada ya kufuatilia taarifa za hali ya hewa waligundua TMA ilitoa taarifa hizo siku mbili kabla ya tukio na kuonesha rangi nyekundu yenye kumaanisha tahadhari kwa maeneo ya Kilindi lakini taarifa hiyo haikuwafikia walengwa.

Mhe. Kamwele alimalizia kwa kuahidi kutatua changamoto zinazoikabili TMA zikiwemo uhitaji wa ongezeko la vituo vya hali ya hewa, mitambo ya hali ya hewa, kupatikana kwa jengo la kituo kikuu cha utabiri n.k

Akitoa salamu za shukrani kwa upande wa TMA, mkurugenzi wa ofisi ya TMA Zanzibar, Bw. Mohamed Ngwali alimshukuru mhe. Waziri kwa pongezi sambamba na kutembelea na kuona shughuli zinazofanywa na TMA, na kuahidi kufanyia kazi maelekezo yote aliyoyatoa .

Imetolewa:
Ofisi ya Uhusiano
Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA)

No comments:

Post a Comment

Featured Post

DKT. KIJAZI: KIWANGO CHA USAHIHI WA UTABIRI WA MSIMU WA VULI 2019 KIWE CHA JUU ZAIDI.

Mkurugenzi mkuu wa TMA na Makamu wa Tatu wa Rais wa Shirika la Hali ya Hewa Duniani Dkt. Agnes Kijazi (katikati mwenye suti nyeusi) waka...