Thursday, December 13, 2018

TANZANIA YASHIRIKI MAJADILIANO YA HUDUMA ZA HALI YA HEWA KWA USAFIRI WA ANGA KWA KUANGALIA FURSA NA CHANGAMOTO ZILIZOPO KATIKA AFRIKA.

Washiriki wa Mkutano wa Afrika wa Huduma za Hali ya Hewa kwa Usafiri wa Anga (World Meteorological Organization African Conference on Meteorology for Aviation – ACMA-2018), tarehe 28 Novemba 2018, Saly, Senegal.

Shirika la Hali ya Hewa Duniani (WMO) kwa kushirikiana na Wadau limeandaaa mkutano wa Afrika kuhusu Utoaji wa Huduma za Hali ya Hewa kwa Usalama wa Usafiri wa Anga (2018 African Conference on Meteorology for Aviation (ACMA-2018), uliofanyika Saly- Senegal.

Mkutano huo ulifanya majadiliano na kupeana uzoefu wa huduma za hali ya hewa kwa usafiri wa anga ili kuwa na uelewa wa pamoja wa fursa na changamoto zilizopo katika Afrika. Aidha, ulilenga kujua vipaumbele na vihatarishi vya utoaji wa huduma za hali ya hewa kuhusiana na mpango wa Shirika la Usafiri wa Anga Duniani ICAO Global Air Navigation Plan (GANP) and aviation System Block Upgrades (ASBU) methodology.

Vile vile, Tanzania ilipata nafasi ya kujadili kwa pamoja na wanachama wengine athari za mabadiliko ya hali ya hewa kwa upande wa usafiri wa anga hususan katika Afrika na kujua mahitaji ya wadau. Aidha,kufanyika kwa mkutano huo ni utekelezaji wa Azimio la Pili la Mkutano wa Nchi Wanachama wa Shirika la Hali ya Hewa Duniani(WMO) kanda ya Afrika (Resolution 2 of the sixteenth session of WMO Regional Association I - Africa) uliofanyika Praia, Cabo Verde Februari, 2015.

Makubaliano ya mkutano huo yatawasilishwa kwenye mkutano wa 17 ujulikanao kama seventeenth session of WMO Regional Association I unaotarajiwa kufanyika Cairo, Misri mwezi Februari, 2019.

Tanzania iliwakilishwa katika mkutano huo na Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) na Mwakilishi wa Kudumu wa Tanzania katika Shirika la Hali ya Hewa Duniani (WMO) – Dkt. Agnes Kijazi pamoja na Mkurugenzi wa Huduma za Utabiri – Dkt. Hamza Kabelwa na Meneja wa kitengo cha kusimamia Viwango wa Ubora na Vihatarishi – Dkt Geofrid Chikojo. Mkutano huo pia ulihudhuriwa na wajumbe wengine wakiwemo kutoka Shirika la KImataifa la Usafiri wa Usalama wa Anga (ICAO), Shirika la Hali ya Hewa Duniani (WMO), Taasisi ya Hali ya Hewa Uingereza (UK Met Office), Taasisi ya Hali ya Hewa Finland (FMI), Wakala wanaosimamia kutoa na Kudhibiti Usafiri wa Anga Nchi za Mangharibi (ASECNA)
Dkt. Agnes Kijazi mmoja wa washiriki akichangia mada kwenye Mkutano wa Afrika wa Huduma za Hali ya Hewa kwa Usafiri wa Anga (World Meteorological Organization African Conference on Meteorology for Aviation – ACMA-2018), tarehe 28 Novemba 2018, Saly, Senegal.
Washiriki kutoka TMA wakipongeza jambo wakati wa Mkutano wa Afrika wa Huduma za Hali ya Hewa kwa Usafiri wa Anga (World Meteorological Organization African Conference on Meteorology for Aviation – ACMA-2018), tarehe 28 Novemba 2018, Saly, Senegal.


No comments:

Post a Comment

Featured Post

DKT. KIJAZI: KIWANGO CHA USAHIHI WA UTABIRI WA MSIMU WA VULI 2019 KIWE CHA JUU ZAIDI.

Mkurugenzi mkuu wa TMA na Makamu wa Tatu wa Rais wa Shirika la Hali ya Hewa Duniani Dkt. Agnes Kijazi (katikati mwenye suti nyeusi) waka...