Tuesday, December 11, 2018

NAIBU WAZIRI WA NCHI OFISI YA MAKAMU WA RAIS MUUNGANO NA MAZINGIRA MHE. MUSSA SIMA AONGOZA UJUMBE WA TANZANIA KATIKA MKUTANO WA MABADILIKO YA TABIANCHI – POLAND

Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. Mussa Sima akisalimiana na Prof. Petteri Taalas Katibu Mkuu wa Shrika la Hali ya Hewa Duniani.  Naibu Waziri Sima anaongoza ujumbe wa Tanzania katika Mkutano wa 24 wa Nchi wanachama wa Mkataba wa Umoja wa Mataifa wa Mabadiliko ya Tabianchi unaoendelea Katowice Poland. Kushoto ni Dkt. Freddy Manyika Kaimu Mkurugenzi Msaidizi anayesshughulikia masuala ya mabadiliko ya tabianchi Idara ya Mazingira Ofisi ya Makamu wa Rais.
Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. Mussa Sima  (wa kwanza kutoka kushoto) wakijadiliana jambo na Prof. Petteri Taalas Katibu Mkuu wa Shirika la Hali ya Hewa Duniani (World Meteorological Organization) pamoja na Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania  Dkt. Agnes Kijazi ,Katowice Poland.
Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. Mussa Sima  (wa pili kutoka kushoto) katika picha ya pamoja na Prof. Petteri Taalas Katibu Mkuu wa Shirika la Hali ya Hewa Duniani (World Meteorological Organization), Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania  Dkt. Agnes Kijazi na  Dkt. Freddy Manyika Kaimu Mkurugenzi Msaidizi anayesshughulikia masuala ya mabadiliko ya tabianchi Idara ya Mazingira Ofisi ya Makamu wa Rais. mara baada ya kushuhudia WMO ikisaini Mkataba na Global Climate Fund wenye lengo la kuzisaidia taasis za hali ya hewa Duniani kushiriki katika utekelezaji wa makubaliano ya mabadiliko ya tabianchi.
Prof. Petteri Taalas Katibu Mkuu wa Shirika la Hali ya Hewa Duniani (World Meteorological Organization) katika picha ya pamoja na Mhe. Mboni Mhita (MB) na mjumbe wa bunge la  Pan-Africa, Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania  Dkt. Agnes Kijazi na  Bw. Marcellin Kokou Nakpon,  Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Hali ya Hewa ya Benin akimwakilisha Rais wa RA1- Afrika baada ya kikao cha pamoja ( kati ya RA1-Afrika, Tanzania na WMO ) kilichojadili masuala mbali mbali yanayohusu Ushiriki wa Taasisi za hali ya hewa za Afrika katika kutekeleza programu za WMO na misaada WMO inayoweza kutoa kuziwezesha taasisi hizo ikiwa pamoja na kuongeza wataalam kutoka Afrika katika Secretariat ya WMO.

No comments:

Post a Comment

Featured Post

DKT. KIJAZI: KIWANGO CHA USAHIHI WA UTABIRI WA MSIMU WA VULI 2019 KIWE CHA JUU ZAIDI.

Mkurugenzi mkuu wa TMA na Makamu wa Tatu wa Rais wa Shirika la Hali ya Hewa Duniani Dkt. Agnes Kijazi (katikati mwenye suti nyeusi) waka...