Thursday, November 22, 2018

VIONGOZI TUGHE WATAKIWA KUWA VIELELEZO VYA UADILIFU KWENYE MAENEO YA KAZI


Halmashauri ya TUGHE ya Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) na menejiment ya TMA wamejumuika katika kikao kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa TMA makao makuu,Ubungo Plaza tarehe 22 Novemba 2018.

Katika kikao hicho, mkurugenzi mkuu wa TMA Dkt.Agnes Kijazi aliwataka viongozi wa TUGHE kuwa vielelezo vya uadilifu kwenye maeneo yao ya kazi.

Aliongezea kuwa ni vyema viongozi  wa TUGHE na menejiment ya TMA kuweka vipaumbele vya ufanisi wa kazi ili kufanikisha maendeleo ya nchi kupitia huduma za hali ya hewa zinazotolewa na TMA

Wakati huo huo alisisitiza haki iende sambamba na wajibu kwa kuzingatia utendaji kazi wa pamoja (team work)

Kwa upande wa TUGHE katibu wake,bw.Benjamin Bikulamchi alishukuru Menejiment ya TMA kwa ushirikiano uliopo baina yao pamoja na kutoa pongezi kwa kazi nzuri inayofanyika katika kuboresha maslahi ya wafanyakazi

Kikao hicho cha siku moja kilijadili masuala mbalimbali kwa manufaa ya Mamlaka kwa ujumla
Halmashauri ya TUGHE katika picha ya pamoja na Mkurugenzi Mkuu wa TMA, Dkt. Agnes Kijazi na baadhi ya viongozi wa TMA
Halmashauri ya TUGHE katika picha ya pamoja na baadhi ya wajumbe wa halmashauri hiyo wanaotarajiwa kustaafu
Matukio mbalimbali katika picha wakati wa kikao hicho


No comments:

Post a Comment

Featured Post

DKT. KIJAZI: KIWANGO CHA USAHIHI WA UTABIRI WA MSIMU WA VULI 2019 KIWE CHA JUU ZAIDI.

Mkurugenzi mkuu wa TMA na Makamu wa Tatu wa Rais wa Shirika la Hali ya Hewa Duniani Dkt. Agnes Kijazi (katikati mwenye suti nyeusi) waka...