Wednesday, September 19, 2018

DKT.KIJAZI ASISITIZA USHIRIKIANO KATIKA KUFANIKISHA UTEKELEZAJI WA PROGRAMU YA KIDUNIA YA HUDUMA ZA HALI YA HEWA AWAMU YA PILI.


Tarehe 17 Septemba 2018; Shirika la Hali ya Hewa Duniani (WMO) kwa kushirikiana na Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) wameshirikiana katika kuandaa kikao kazi cha kwanza cha utekelezaji wa programu ya kidunia ya huduma za hali ya hewa kwa awamu ya II. Kikao kazi hicho kilifanyika katika ukumbi wa mkutano uliopo Golden Jubilee, Dar es Salaam. 

Malengo ya kikao kazi hicho ni kupitia taarifa za utekelezaji wa awamu ya kwanza ya programu ya kidunia ya huduma za hali ya hewa ili kutambua mafanikio yaliyopatikana, changamoto zake na namna ya uboreshaji wa utekelezaji wa awamu ya pili katika kufanikisha malengo ya awamu ya pili. Programu ya Kidunia ya huduma za hali ya hewa awamu ya pili imedhaminiwa na shirika la misaada la Norway (Norwegian Agency for Development Cooperation (NORAD)) na kutekelezwa na nchi ya Tanzania na Malawi pekee kwa nchi za Afrika.

Akifungua kikao kazi hicho katika hotuba ya Dkt. Agnes Kijazi, mkurugenzi mkuu wa TMA na mwakilishi wa kuduma wa WMO kutoka Tanzania  iliyowasilishwa kwa niaba yake na mkurugenzi wa utafiti na matumizi ya huduma za hali ya hewa, Dkt. Ladislaus Chang’a alisisistiza ushirikiano wa taasisi shiriki katika utekelezaji wa proramu ya kidunia ya huduma za hali ya hewa kwa awamu ya pili kwa vile umuhimu wake umeonekana wakati wa utekelezaji wa awamu ya kwanza ambapo shughuli mbalimbali ikiwemo mipango na mikakati ya kufanikisha programu ilifanyika kwa ushirikiano wa pamoja. Aliongezea kwa kukitaka kikao kazi hicho kuhakikisha shughuli/mikakati ya utekelezaji wa awamu ya pili inaendana na malengo ya mfumo wa taifa wa huduma za hali ya hewa (NFCS). Malengo ya NFCS yalitokana na utekelezaji wa awamu ya kwanza katika kutambua changamoto zake.

Kikao kiliwajumuisha watendaji wa utekelezaji wa programu kutoka  Ofisi ya Waziri Mkuu (Kitengo cha Uratibu wa Maafa),), Wizara ya Afya, Maendeleo ya jamii,Jinsia na watoto, Wizara ya Kilimo, Shirika la Afya Duniani (WHO), Shirika la Mpango wa Chakula Duniani (WFP), Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania, Chama cha Msalaba Mwekundu Tanzania pamoja na washiriki wengine kutoka Shirika la Halin ya Hewa Dunia (WMO) na Shirika la Kimataifa la Msalaba mwekundu na Hilali Nyekundu (IFRC). Tanzania inatarajia kuzindua rasmi programu ya kidunia ya huduma za hali ya hewa kwa awamu ya pili, tarehe 18 Septemba 2018, katika ukumbi wa  Golden Jubilee Towers, Dar es Salaam.

Imetolewa:
Monica Mutoni,
Ofisi ya Uhusiano,
Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA)


Tuesday, September 18, 2018

TANZANIA YAZINDUA PROGRAMU YA KIDUNIA YA HUDUMA ZA HALI YA HEWA (GFCS) AWAMU YA PILI.


Dar es Salaam 18/09/ 2018

Tanzania imezindua rasmi programu ya kidunia ya huduma za hali ya hewa kwa awamu ya pili, tarehe 18 Septemba 2018, katika ukumbi wa  Golden Jubilee Tower, Dar es Salaam. Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania kwa kushirikiana na Shirika la Hali ya Hewa Duniani (World Meteorological Organization) kupitia ufadhili wa Serikali ya Norway imekuwa ikitekeleza Mfumo wa Kidunia wa Huduma za Hali ya Hewa “Global Framework for Climate Service-GFCS (2014-2016)”. Washirika wengine katika mradi huu hapa nchini ni Wizara ya Kilimo, Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Shirika la Mpango wa Chakula Duniani – WFP, Shirika la Afya Duniani – WHO, Shirika la Msalaba Mwekundu Tanzania.

Utekelezaji wa programu ya GFCS hapa Tanzania ulianza mwezi Februari 2014 kwa warsha ya uzinduzi iliyojumuisha wadau wa masuala ya hali ya hewa wa ndani na nje ya nchi. Lengo kuu la warsha lilikuwa ni kukubaliana namna bora ya utekelezaji na usimamizi wa programu ambapo  mfumo wa utekelezaji na usimamizi uliundwa rasmi ikiwa ni pamoja na mapendekezo ya TANDREC kwasasa TADMAC kuwa msimamizi mkuu wa GFCS, na kuchagua rasmi wilaya za Kiteto na Longido kuwa maeneo ya majaribio ya utekelezaji wa programu sambamba na Mfumo wa Taifa wa Huduma za Hali ya Hewa “National Framework for Climate Services (NFCS)” uanze kutekelezwa kwa kushirikiana na wadau mbalimbali.
Akizindua rasmi programu hiyo, Katibu Mkuu Ofisi ya waziri Mkuu (Sera na Uratibu) Prof. faustin Kamuzora alisisitiza kuwa programu hii imekuja wakati muafaka kwa vile serikali imekuwa na jitihada za kukabiliana na majanga yatokanayo na hali mbaya ya hewa, aidha alisisitiza umuhimu wa utekelezaji wa program hiyo huhakikishe taarifa za hali ya hewa zinawafikia wananchi hususani wa maeneo ya vijinini kwa wakati na usahihi huku akiipongeza TMA kwa ongezeko la usahihi wa utabiri unaotolewa kwa kipindi cha miaka ya hivi karibuni.

Naye, mkurugenzi mkuu wa TMA Dkt. Agnes Kijazi alimshukuru mgeni rasmi na wafadhili wa programu hiyo kwa ushirikiano wao huku akifafanua lengo la uzinduzi wa awamu ya pili ni kuanzishwa rasmi utekelezaji wa shughuli za program kwa awamu nyingine. Ikiwa na lengo la kuongeza uelewa wa matumizi ya taarifa za hali ya hewa kwa watumiaji walio katika hatari ya kuathirika na hali ya hewa hasa hasa katika kukabiliana na maafa yatokanayo na hali mbaya ya hewa, usalama wa chakula na afya

Kwa upande wa wafadhili wa programu hiyo kupitia serikali ya Norway, mwakilishi kutoka WMO Bi. Erica Allis alisema kuwa WMO imeamua kuzindua awamu ya pili ya utekelezaji wa programu hiyo kutokana na mafanikio yaliyopatikana katika utekeleza wa awamu ya kwanza na uhitaji wa utekelezaji wa kina zaidi kama vile kufanyiwa kazi mahitaji ya mfumo wa taifa wa hali ya hewa, utoaji wa taarifa za hali ya hewa zenye ubora zaidi kwa maeneo madogo madogo na mafunzo kwa wataalamu ndani na nje sambamba na usambazaji kupitia mfumo wa simu za mkononi FARMSMS

Mwakilishi kutoka Norway aliongezea kwa kusema kuwa wanatambua uhitaji wa taarifa za hali ya hewa kwa jamii  kwahiyo ni wakati muafaka kwa wadau wanaoshiriki katika utekelezaji wa programu hii kujifunza kutoka katika awamu ya kwanza na kufanya maboresho ya utekelezaji wake ili jamii ikanufaike zaidi na programu hii.

Uzinduzi huo ulihudhuriwa na wadau mbali mbali kutoka wizara za serikali, mashirikia ya kimataifa, mashirika ya elimu, mashirika ya siyo ya kiserikali, taasisi za utafiti, wanahabari na wengine wengi.
Imetolewa:
Monica Mutoni,
Ofisi ya Uhusiano,
Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA)


Sunday, September 16, 2018

THE 16TH MEETING OF THE GFCS PROJECT DELIVERY TEAM (PDT) OF TANZANIA AFFIRM PREPARATIONS FOR GFCS PHASE TWO IMPLEMENTATION

The sixteenth meeting of the Project Delivery Team (PDT) for GFCS implementation in Tanzania was held on 13th September at Ubungo Plaza, Dar es Salaam. This was the first meeting in the context of implementation of GFCS Adaptation Programme in Africa (APA) Phase II.

The meeting was officiated by opening remarks from the Permanent Representative of the United Republic of Tanzania with World Meteorological Organization, Dr. Agnes Kijazi. In her remarks, she expressed her thanks and appreciation to PDT members for the excellent work in implementation of Phase I that culminated with the preparation and launching of the National Framework for Climate Services for Tanzania. She urged the PDT to work with more momentum and focus their efforts and skills in effective implementation of Phase II activities and also the National Framework. The APA aims to increase the resilience of people most vulnerable to the impact of weather and climate-related hazards by developing user-driven climate services for food security, health and disaster risk reduction in Tanzania and Malawi.

The PDT, which normally meet on Quarterly basis, is responsible for monitoring progress on implementation of the programme activities, planning and implementation of joint activities. Members of the PDT include participants from Tanzania World Food Program (WFP-TZ), Vice President Office (VPO), Prime Minister’s Office (PMO), Ministry of Health, Community Development, Gender, Elderly and Children (MoHCDGEC), Ministry of Agriculture (MoA), World Health Organization (WHO), Tanzania RedCross Society (TRCS), Tanzania Meteorological Agency (TMA) and the University of Dar es Salaam (UDSM)

The PDT deliberated on the preparation for the implementation of Phase II of the GFCS Adaptation Programme in Africa, funded by Norwegian Agency for Development Cooperation (NORAD).

PDT members reviewed and endorsed the programme for the technical meeting scheduled to take place on 17th September 2018 and the programme for the official launching of the phase II that will be held on 18th September 2018 at Golden Jubilee towers, in Dar es Salaam.


Released by: Monica Mutoni, Communication Officer, TMA

Featured Post

DKT. KIJAZI: KIWANGO CHA USAHIHI WA UTABIRI WA MSIMU WA VULI 2019 KIWE CHA JUU ZAIDI.

Mkurugenzi mkuu wa TMA na Makamu wa Tatu wa Rais wa Shirika la Hali ya Hewa Duniani Dkt. Agnes Kijazi (katikati mwenye suti nyeusi) waka...