Tuesday, August 14, 2018

TMA YAWA MWENYEJI WA MKUTANO WA MRADI WA HIGH IMPACT WEATHER LAKE SYSTEM (HIGHWAY)”

Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imekuwa mwenyeji wa mkutano wa Mradi wa HIGH Impact Weather lAke sYstem (HIGHWAY)” unaojadili namna ya kuongeza uwezo za nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) zilizoko kwenye eneo la bonde la Ziwa Victoria katika kupima na kufuatilia mifumo ya hali ya hewa hususani ile inayosababisha hali mbaya ya hewa ndani ya Ziwa Victoria kwa lengo la kuokoa maisha ya watu na mali zao "HIGH Impact Weather lAke sYstem (HIGHWAY) Gap Analysis". Mradi wa HIGHWAY unafadhiliwa na Shirika la Maendeleo la Nchini Uingereza (DFID) kupitia program yake ya Weather and Climate Information Services for Africa (WISER)” na kutekelezwa kwa ushirikiano na Sekretariet ya EAC, Shirika la Hali ya hewa Duniani(WMO), na Taasisi za Hali ya Hewa za nchi wanachama wa EAC.  Mkutano huu unafanyika Jijini Arusha kuanzia tarehe 13 hadi 14 Agosti 2018.

1 comment:

Featured Post

DKT. KIJAZI: KIWANGO CHA USAHIHI WA UTABIRI WA MSIMU WA VULI 2019 KIWE CHA JUU ZAIDI.

Mkurugenzi mkuu wa TMA na Makamu wa Tatu wa Rais wa Shirika la Hali ya Hewa Duniani Dkt. Agnes Kijazi (katikati mwenye suti nyeusi) waka...