Monday, June 18, 2018

MAADHIMISHO YA WIKI YA UTUMISHI WA UMMA MWAKA 2018


Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) inawaalika wadau wake wote kutembelea ofisi za hali ya hewa ambazo ziko nchini kote kati ya tarehe 20-22 Juni 2018 ili kutoa maoni na ushauri kuhusu uboreshaji wa huduma za hali ya hewa zitolewazo na Mamlaka.

Kwa Makao Makuu ya Mamlaka iliyopo Ubungo Plaza, Barabara ya Morogoro, Mamlaka itakutana na wadau tarehe 21/06/2018 kati ya saa 3.30 asubuhi hadi saa 9.00 mchana, ghorofa ya tatu chumba namba 309. Aidha, unaweza kuwasilisha kero na maoni kwa siku zote za maadhimisho kupitia barua pepe met@meteo.go.tz na ofisi za kanda zifuatazo:
Kanda ya Mashariki: Kituo cha Hali ya Hewa, Morogoro, Simu: 023-2603794
Kanda ya Ziwa: Kituo cha Hali ya Hewa, Mwanza, Simu: 028-2505338
Kanda ya Kati: Kituo cha Hali ya Hewa, Dodoma, Simu: 026-2351594
Kanda ya Kusini: Kituo cha Hali ya Hewa, Mtwara, Simu: 023-2333847
Kanda ya Nyanda za Juu Kusini Magharibi : Kituo cha Hali ya Hewa, Mbeya, Simu: 025-2503096
Kanda za Nyanda za Juu Kaskazini-mashariki: Kituo cha Hali ya Hewa, KIA, Simu: 0272554224
Kanda ya Magharibi: Kituo cha Hali ya Hewa, Tabora, Simu: 026-2604258
Ofisi ya Hali ya Hewa Zanzibar, Simu: 024-2231958
Ofisi ya Hali ya Hewa, Uwanja wa Ndege wa Kimataifa, JNIA, Simu: 022-2110290

Kwa taarifa zaidi wasiliana na Ofisi ya hali ya hewa iliyopo karibu nawe au Ofisi ya Masoko na Uhusiano wa Umma kwa namba +255 22 2460706-8. Kauli mbiu: Kuimarisha Ushirikishwaji wa Jamii katika utoaji Huduma:Vijana washirikishwe kuleta mabadiliko barani Afrika. Imetolewa na: Mkurugenzi Mkuu MAMLAKA YA HALI YA HEWA TANZANIA S.L.P. 3056 DAR ES SALAAM Simu: 255 22 2460706-8 Faksi: 255 22 2460735/2460700 Barua pepe: met@meteo.go.tz Tovuti: www.meteo.go.tz

No comments:

Post a Comment

Featured Post

DKT. KIJAZI: KIWANGO CHA USAHIHI WA UTABIRI WA MSIMU WA VULI 2019 KIWE CHA JUU ZAIDI.

Mkurugenzi mkuu wa TMA na Makamu wa Tatu wa Rais wa Shirika la Hali ya Hewa Duniani Dkt. Agnes Kijazi (katikati mwenye suti nyeusi) waka...