Friday, March 24, 2017

NAIBU WAZIRI AZUNGUMZIA SIKU YA HALI YA HEWA DUNIANI KWA WANAHABARI

Naibu Waziri wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Mhe. Mhandisi Edwin Ngonyani akiongea na  vyombo vya habari (hawapo pichani)
Naibu Waziri wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Mhe. Mhandisi Edwin Ngonyani akijibu swali kwa  vyombo vya habari (hawapo pichani)
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania, Dkt. Agnes Kijazi akifafanua jambo kwa wanahabari (hawapo pichani)
Baadhi ya wanahabari katika picha



MAADHIMISHO YA SIKU YA HALI YA HEWA DUNIANI

TAREHE 23 MACHI, 2017

Kila mwaka ifikapo tarehe 23 Machi nchi wanachama 190 wa Shirika la Hali ya Hewa Duniani hujiunga kuadhimisha kuzaliwa kwa Shirika hilo lililoanzishwa tarehe 23 Machi, 1950 kulingana na kauli mbiu teule. Kauli mbiu ya mwaka huu ni ’Tuyaelewe mawingu na umuhimu wake’- ”(Understanding clouds)”.
Katika kuadhimisha Siku ya Hali ya Hewa Duniani (WMD), Shirika la Hali ya Hewa Duniani  limetambua umuhimu wa kuongeza uelewa wa mawingu ili kujua zaidi mchango wake katika mzunguko wa maji kati ya nchi kavu, baharini na angan,i na uhusiano wake na hali ya hewa ya muda mfupi na mrefu. Kama inavyojulikana kuwa mawingu yana umuhimu mkubwa sana katika mifumo ya hali ya hewa ya dunia na hivyo elimu juu ya tabia ya mawingu itasaidia katika kutabiri hali ya hewa na kutambua mabadiliko ya tabia nchi kwa wakati ujao. Wahenga huwa wanasema, Dalili ya Mvua ni Mawingu.
 
Kama ilivyo kwa wanachama wengine, Tanzania inaungana nao kuadhimisha siku hii inayofikia kilele leo tarehe 23 Machi, 2017 kwa kuwakaribisha wananchi wote kutembelea vituo vya hali ya hewa nchini ili kuona shughuli zitolewazo na Mamlaka na kujifunza. Aidha, Mamlaka itambelea na kutoa elimu kwa vijana wa baadhi ya shule na vyuo mbali mbali nchini kupitia ofisi zake zilizopo nchi nzima. Kutoa makala  za siku hiyo kwenye magazeti, vipindi kwenye radio, televisheni na mitandao ya kijamii kuhusu elimu juu ya mawingu na sayansi hali ya hewa kwa ujumla, hii itasaidia kuongeza wigo wa elimu kwa umma hususani mashuleni.

Tunawatakia maadhimisho mema ya Siku ya Hali ya Hewa Duniani

’Tuyaelewe mawingu na umuhimu wake’
(Understanding Clouds)

Kupata makala za Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Mhe. Prof Makame Mbarawa  na Mkurugenzi Mkuu wa TMA Dkt Agnes Kijazi ingia humu  http://www.meteo.go.tz/news/74


Tuesday, March 21, 2017

KWANINI NIYAELEWE MAWINGU NA UMUHIMU WAKE?


TEMBELEA OFISI ZETU  AU SIKILIZA VIPINDI MBALIMBALI KUPITIA VYOMBO VYA HABARI VILEVILE USIACHE KUTEMBELEA TOVUTI,MITANDAO YA KIJAMII NA BLOG YETU KUJIPATIA MAJIBU YA MASWALI YAKO



Monday, March 20, 2017

SIKU YA HALI YA HEWA DUNIANI 23 MACHI 2017



 KAULI MBIU: 'TUYAELEWE MAWINGU NA UMUHIMU WAKE' 'UNDERSTANDING CLOUDS'

 WANANCHI WOTE MNAKIBISHWA KUTEMBELEA VITUO VYETU VILIVOPO MAENEO MBALIMBALI NCHINI ILI KUPATA ELIMU ZAIDI YA SAYANSI YA HALI YA HEWA.

    'HALI YA HEWA KWA MAENDELEO ENDELEVU'

Thursday, March 9, 2017

DISTRICT LEVEL STAKEHOLDERS CONSULTATION WORKSHOP ON “THE NATIONAL FRAMEWORK FOR CLIMATE SERVICES (NFCS)” HELD ON 23RD FEBRUARY, 2017 IN KITETO DISTRICT, MANYARA REGION






NFCS workshop participants posing for a group photo in Kiteto (23rd February 2017).


As part of implementation of the Global Framework for Climate Services (GFCS) programme in Tanzania, Tanzania Meteorological Agency (TMA) organized a District Level Stakeholders Consultation Workshop on The National Framework for Climate Services (NFCS) in Kiteto District, Manyara Region, which was held on 23rd February, 2017. The main objective was to share the progress in the preparation of the NFCS to stakeholders and solicit more inputs and comments for its improvement. The workshop was attended by experts (from Kiteto District Council, Tanzania Red Cross and representatives from Civil Society Organizations), community leaders, policy makers, farmers and pastoralists.



The workshop was officiated by speech from the Guest of Honour, the District Executive Director (DED) of Kiteto District Council, Mr. Tamim Kambo, and the Director General of TMA and Permanent Representative of Tanzania with WMO, Dr. Agnes Kijazi.  In their speech, both Mr. Kambo  and Dr. Kijazi thanked the Royal Government of Norway, World Meteorological Organization  and all GFCS partners for supporting the initiatives to enhance climate services in Tanzania. 



The workshop programme comprised of presentations on the status of GFCS implementation in Tanzania and  the draft NFCS. After the presentations, participants were organized in three groups to review the draft NFCS and provide comments and inputs for its improvement.



Some of the key comments and recommendations from the stakeholders were:

ü  The document need to be aligned with the National strategies and policies including the National development vision (Vision  2025),

ü  Priority sectors need to be expounded to include Water, Energy and Tourism

ü  Livestock sector should be treated with more weight and should be mentioned in the document and should not be hidden in Agriculture

ü  More awareness on climate and climate change and socio-economic benefits of weather and climate information is needed. Awareness and sensitization should also target Tribal Leaders and Private Sectors

ü  The document should be produced in both English and Swahili.

ü  TMA should establish and expand observation and monitoring Network in Kiteto and other districts. 

Featured Post

DKT. KIJAZI: KIWANGO CHA USAHIHI WA UTABIRI WA MSIMU WA VULI 2019 KIWE CHA JUU ZAIDI.

Mkurugenzi mkuu wa TMA na Makamu wa Tatu wa Rais wa Shirika la Hali ya Hewa Duniani Dkt. Agnes Kijazi (katikati mwenye suti nyeusi) waka...