Thursday, May 26, 2016

HALI YA HEWA TUGHE YAPATA UONGOZI MPYA


Uongozi mpya wa TUGHE katika picha ya pamoja.
Baadhi ya wanachama wa TUGHE wakiomba kura ili kuweza kupata nafasi mbali mbali za uongozi sambamba na zoezi la uchaguzi.
Wanachama wa TUGHE (Pichani) wachagua viongozi wapya katika uchaguzi uliofanyika tarehe 24 Mei 2016 kwenye ukumbi wa Makao Makuu-TMA. Viongozi waliochaguliwa ni pamoja na Mwenyekiti Bi. Aurelia Mwakalukwa, Katibu Bw. Benjamin Bikulamchi, Mwenyekiti wa kinamama Bi. Zainab Gumbo, Katibu wa kinamama Bi. Hamida Hassan na wajumbe.

 Na. Monica Mutoni

Tuesday, May 24, 2016

TV JOURNALIST WEATHER TRAINING DAR ES SALAAM, TANZANIA ON 20th MAY, 2016


This Public Weather Services training for Azam Journalists aimed at strengthening the link between the providers and users of public weather services, so that individuals, communities and organizations can make effective use of the available products and services and foster a better understanding and awareness of public weather services in terms of their availability, the terminology used, the way they can be used to the greatest effect and their socio-economic benefits as well as to easier communication among societies. The training aimed to meet World Met. Organization (WMO) requirements.

Training participants were from AZAM pay TV and training facilitators were from TMA and WMO.

Wednesday, May 18, 2016

SEVERE WEATHER EVENTS- EFFECTIVE PLANNING (SWEEP) TRAINING WORKSHOP HELD FROM 16 TO 27 MAY, 2016, DAR ES SALAAM, TANZANIA


Workshop is held under the auspice of the Pilot Project called “The Multi Hazard Early Warning Service (MHEWS)” which focuses on the coastal zone of Tanzania and across sectors of Marine transport, Fishing, Agriculture, and Oil & Gas. MHEWS project is being funded by DFID trough the WISER program.

The objective of  SWEEP Workshop is to ensure all stakeholders have a shared and consistent understanding of the features and benefits of the Multi-hazard Early Warning Services to effective planning.


Expected output is to equip participants with all the necessary skills and provide information on the characteristics of the extremes and enable improved warning messages, timely and effective communication among actors which will solely serve lives and property and enhance socio-economic development in the country.

Wednesday, May 11, 2016

UCHUKUZI SC VINARA MEI MOSI WABEBA VIKOMBE 11


Wachezaji wa Uchukuzi SC wakiwa wamevipanga vikombe 11 walivyotwaa kwenye michezo mbalimbali ya Mei Mosi, iliyomalizika juzi mkoani Dodoma


TIMU ya Uchukuzi SC iliyopo chini ya Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, imeibuka kinara kwenye mashindano ya Mei Mosi baada ya kutwaa vikombe 11 vya michezo mbalimbali. Timu hiyo inajumuisha wanamichezo kutoka Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania.

Timu hiyo imetwaa ubingwa katika michezo ya netiboli, baiskeli na bao  (wanaume), kamba (wanawake na wanaume); huku vikombe vya ushindi wa pili ni vya michezo ya bao (wanawake) na draft (wanaume); wakati vya ushindi wa tatu  ni katika soka, karata (wanaume), riadha (wanawake na wanaume).

Hata hivyo, kutokana na uwingi wa vikombe timu hiyo ilitangazwa  mshindi wa jumla  kwenye sherehe za Mei Mosi na kukabidhiwa kombe na Mh. Rais John Magufuli.

Timu nyingine na idadi ya vikombe zilizopata ni TAMISEMI saba kikiwemo cha ubingwa wa soka baada ya kuwafunga GGM katika fainali kwa magoli 2-0, huku TPDC wakiwa na vikombe vitano sawa na Tanesco.Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM), wamejikusanyia vikombe vinne, Ujenzi vikombe viwili, na Mawasiliano, Ukaguzi  na Halmashauri ya Nyasa kila mmoja wana kikombe kimoja kila mmoja.

Awali katika michezo iliyochezwa jana timu ya Uchukuzi SC iliwafunga Tamisemi kwa magoli 18-15 katika mchezo wa netiboli, ambapo wafungaji wake Tatu Kitula na Matalena Mhagama waliwapeleka puta wapinzani wao na hadi mapumziko walikuwa mbele kwa magoli 11-7.

Washindi wote walikabidhiwa kombe na mgeni rasmi Mwenyekiti wa Chama cha Wafanyakazi wa Reli Tanzania (TRAWU), Mussa Kalala, ambaye  katika hotuba yake aliwashutumu viongozi walioshindwa kupeleka timu zao kwenye mashindano hayo na kusema michezo mahala pa kazi husaidia kuijenga miili ya wafanyakazi kuendelea kuwa mikakamavu na kuwa na afya bora, ambapo hutoa huduma bora iliyotukuka na kuzalisha tija zaidi.




Featured Post

DKT. KIJAZI: KIWANGO CHA USAHIHI WA UTABIRI WA MSIMU WA VULI 2019 KIWE CHA JUU ZAIDI.

Mkurugenzi mkuu wa TMA na Makamu wa Tatu wa Rais wa Shirika la Hali ya Hewa Duniani Dkt. Agnes Kijazi (katikati mwenye suti nyeusi) waka...