Saturday, June 13, 2015

MATUKIO KATIKA PICHA MKUTANO WA BARAZA KUU LA SHIRIKA LA HALI YA HEWA DUNIANI (WMO)




Ujumbe wa Tanzania unaendelea kushiriki katika kikao cha Mkutano Mkuu wa Kumi na saba wa Shirikia la Hali ya Hewa Duniani (WMO-Congress 17), mijini Geneva, nchini Uswisi. Ujumbe huo umeshiriki katika matukio mbalimbali ya mkutano huo ikiwa ni pamoja na Dkt. Agnes Kijazi kushiriki katika siku ya Jinsia ya WMO (WMO Gender Day), kutoa mada zilizotoa uzoefu wa Tanzania wa utekelezaji wa program za utekelezaji wa programu ya utoaji wa huduma bora za hali ya hewa kwa jamii “Global Framework for Climate Services (GFCS) na programu ya uendelezaji wa mitandao ya upimaji wa hali ya hewa na mawasiliano (WMO Integrated Observation System and WMO Information System-WIGOS/WIS). Kwa habari zaidi angalia picha za matukio mbalimbali ya Mkutano huo hapa. 


Mh. Balozi na Mwakilishi wa Kudumu wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa, Geneva na Murugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Dkt. Agnes Kijazi na Ujumbe wa Tanzania wakishiriki katika Mkutano Mkuu wa Kumi na Saba wa Shirika la Hali ya Hewa Duniani (WMO- Congress-17), Geneva, Uswisi


“WMO Gender Day”, Siku ya Ijumaa, Tarehe 5 Juni 2015 ilikuwa siku ya Jinsia (WMO Gender Day) ya Mkutano wa Kumi na saba wa Shirika la hali ya hewa Duniani (WMO-Congress 17). Dkt. Agnes Kijazi, Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Hali ya Hewa na Mwakilishi wa Kudumu wa Tanzania katika Shirika la Hali ya Hewa Duniani (WMO) alikuwa miongoni mwa zaidi ya wajumbe 50 na wafanyakazi wa WMO walioshiriki katika ufunguzi wa siku hii na kujadili masuala mbalimbali katika nyanja ya usawa na uwezeshaji wa wanawake katika taasisi za hali ya hewa na WMO. Maoni yaliyotokana na majadiliano ya siku hii yatajumuishwa na kutengeneza Mpango Mkakati wa WMO utakaolenga masuala ya jinsia (WMO Gender Action Plan)

Vile vile siku ya tarehe 6 Juni 2015, Dr. Kijazi alishiriki katika warsha ya Uongozi ya viongozi wanawake ikiwa na lengo kuwajengea uwezo zaidi wa uongozi wajumbe waliohudhuria katika mkutano mkuu wa kumi na saba wa WMO.


Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania, Dr Agnes Kijazi akiwasilisha mada ya uzoefu wa Tanzania katika utoaji wa huduma za hali ya hewa kwa jamii (Global Framework for Climate Services (GFCS)) katika Mkutano Mkuu wa Kumi na Saba wa Shirika la Hali ya Hewa Duniani (WMO Congress-17), Geneva, Uswisi.

Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA), Dr. Agnes Kijazi akiwasilisha mada ya uzoefu wa Tanzania katika utekelezaji wa Programu ya "WMO Intergrated Global Observation Systems (WIGOS)" katika Mkutano Mkuu wa kumi na saba wa Shirika la Hali ya Hewa Duniani (WMO), Geneva, Uswisi.


Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA), Dr. Agnes Kijazi na Mkurugenzi wa utabiri Dr. Hamza Kabelwa wakiwa katika majadiliano na maafisa wa Shirika la Hali ya hewa Duniani (WMO) na Marekani wakati wa majadiliano yanayohusu namna ya kuboresha huduma za hali ya hewa kwa jamii hususan utoaji wa tahadhari “ Early Warning” katika Mkutano Mkuu wa kumi na saba wa Shirika la Hali ya Hewa Duniani (WMO), Geneva, Uswisi.


Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA), Dr. Agnes Kijazi na Mtabiri Mwandamizi katika Ofisi ya Mahusiano ya Kimataifa ya TMA, Ndugu. Wilbert Timiza wakifuatili mwenendo wa Mkutano Mkuu wa kumi na saba wa Shirika la Hali ya Hewa Duniani (WMO), Geneva, nchini Uswisi.


No comments:

Post a Comment

Featured Post

DKT. KIJAZI: KIWANGO CHA USAHIHI WA UTABIRI WA MSIMU WA VULI 2019 KIWE CHA JUU ZAIDI.

Mkurugenzi mkuu wa TMA na Makamu wa Tatu wa Rais wa Shirika la Hali ya Hewa Duniani Dkt. Agnes Kijazi (katikati mwenye suti nyeusi) waka...