Saturday, November 29, 2014

HALI YA HEWA YAENDELEA KUWANOA WATAALAMU WAKE KATIKA KUKIDHI VIWANGO VYA SHIRIKA LA HALI YA HEWA DUNIANI (WMO)




Mkurugenzi Mkuu wa TMA Dkt. Agnes Kijazi ambaye pia alikuwa mgeni rasmi akizungumza na wahitimu wa mafunzo ya huduma za hali ya hewa kwa ajili ya usafiri wa anga kutoka Chuo cha Hali ya Hewa Kigoma



Mwakilishi wa wahitimu Bi. Pamela Levira akisoma risala ya wahitimu kwa mgeni rasmi katika mahafali ya pili ya mafunzo ya huduma za hali ya hewa kwa ajili ya usafiri wa anga kutoka Chuo cha Hali ya Hewa Kigoma

Mgeni rasmi, Mkurugenzi Mkuu wa TMA Dkt. Agnes Kijazi katika picha ya pamoja na wahitimu wa mafunzo ya huduma za hali ya hewa kwa ajili ya usafiri wa anga kutoka Chuo cha Hali ya Hewa Kigoma,Kulia kwake mwenye tai nyekundu ni Mkuu wa Chuo cha Hali ya Hewa Kigoma Bw. Joseph Aliba


Mamlaka ya Hali ya Hewa nchini iliendesha mafunzo ya hali ya hewa kwaajili ya usafiri wa anga ‘Aeronautical Meteorology’. Mafunzo haya yalikuwa yakiendeshwa chini ya Chuo cha Hali ya Hewa Kigoma ikiwa ni kuhakikisha wafanyakazi wa Mamlaka ya hali ya Hewa (TMA) kwa upande wa huduma za hali ya hewa kwa usafiri wa anga wanakidhi vigezo vilivyowekwa na WMO. Mafunzo haya ni ya pili kutolewa hapa nchini kupitia Chuo cha Hali ya Hewa Kigoma.
Akifunga mafunzo hayo, Mgeni rasmi katika mahafali ya pili ya Kozi ya Hali ya Hewa kwa ajili ua Usafiri wa Anga; Mkurugenzi Mkuu wa TMA, Dkt Agnes Kijazi alimpongeza Mkuu wa Chuo kwa kufanikisha kuendesha mafunzo hayo kwa mara ya pili ambayo ni moja ya utekelezaji wa vigezo vilivyowekwa kimataifa na WMO. ‘Kuendesha mafunzo haya kutawezesha Mamlaka kuwa na wataalamu wa kutosha wanaokubalika kimataifa kutoa huduma za hali ya hewa kwaajili ya usafiri wa anga, hivyo Mamlaka itakuwa imefikia viwango vilivyowekwa na Shirika la Hali ya Hewa Duniani, vinavyozitaka taasisi za hali ya hewa duniani kuwa na na wataalamu wenye shahada ya hali ya hewa na ujuzi unaotakiwa kwaajili ya kutoa huduma katika usafiri wa anga’Alisema Dk. Kijazi. Aidha aliwataka wahitimu kutumia ujuzi waliopata ili kufanya kazi kwa ufanisi na hviyo kuchangia katika maendeleo ya taifa.
Kwa upande wake Mkuu wa chuo cha hali ya hewa Kigoma Bwana Joseph Aliba alisema Chuo cha Hali ya Hewa Kigoma kimepata usajili wa kudumu toka NACTE na waalimu wote wamesajiliwa na NACTE.
Akiongea kwa niaba ya wahitimu Bi Pamela Levira ameishukuru Mamlaka kwa kuwajengea uwezo  wa kufanya kazi kwa kujiamini katika kutoa huduma za hali hewa katika sekta ya usafiri wa anga.
Chuo cha Hali ya Hewa Kigoma  ni chuo pekee Tanzania kinachotoa elimu ya ngazi ya cheti na diploma kwa taalamu ya hali ya hewa. Chuo kimepata usajili wa NACTE kwa leseni ya kuendesha mafunzo ya nje ya mipaka ya nchi ‘cross boarder license’.
Imetolewa na : Monica Mutoni Ofisa Uhusiano- Mamlaka ya Hali ya Hewa

TANZANIA METEOROLOGICAL AGENCY CONTINUES TO BUILD EMPLOYEE’S CAPACITY TO MEET WORLD METEOROLOGICAL ORGANIZATION (WMO) REQUIREMENTS







TMA has conducted a second short course in Aviation Meteorology for Meteorologists to ensure that the standard required by WMO is met. This training was facilitated by Kigoma National Meteorological Training Centre (KNMTC).
The Director General of TMA, Dr Agnes Kijazi, congratulated the Management of KNMTC, during the graduation ceremony held on 28th November 2014, for facilitating the training for the second time. “Conducting this training will enable Meteorologists to meet WMO requirements on Aviation Meteorology.’’, says Dr Agnes Kijazi. The participants were also asked to utilize the knowledge gained to excel in their daily aviation duties.
Speaking on behalf of graduates Ms  Pamela, appreciate the effort done by TMA to ensure staff competence on provision of aeronautical services.
Kigoma National Meteorological Training Centre is the only centre in Tanzania which is able to provide a Meteorological Certificate and Diploma level. The Centre is registered under NACTE and also has a cross border license. It is planning to extend its training both in Tanzania and internationally.  
Issued by: Monica Mutoni, TMA Public Relation Office.

Wednesday, November 19, 2014

TMA CALLS FOR TANZANIA SCIENTISTS TO PARTICIPATE ON CLIMATE CHANGE RELATED RESEARCH AND IN IPCC PROCESS.




Picture: Guest of Honour Eng. James Ngeleja (  2nd from left) on behalf of the Chairperson of TMA Ministerial Advisory Board, TMA-Director General Dr. Agnes Kijazi,  (3rd  from Left) on a group photo with workshop participants on the Workshop on the latest findings of IPCC (IPCC AR5) held on 18th November 2014, Blue Pearl Hotel.

Tanzania Meteorological Agency (TMA) held a sensitization workshop on the latest Iintergovernmental Panel on Climate Change (IPCC) findings (IPCC fifth assessment report), on 18th November 2014, at Blue Pearl hotel, Dar es Salaam. When officiating the opening of the workshop, the guest of Honour Eng. James Ngeleja, who represented the chairman of the Ministerial Advisory Board of Tanzania Meteorological Agency Mr. Morisson Mlaki called for scientists in Tanzania to actively participate on climate change related research and IPCC process. On his speech he noted the low participation of Africa scientists in the IPCC Process, and the low number of scientific research on climate change in peer reviewed journals.  I am aware that we have a large research gaps in many thematic areas including in climate change and marine ecosystem, climate change and Agriculture, climate change and Health, and climate change and livelihoods. More studies need to be conducted focusing on climate change attributions in the respective thematic areas. I therefore pose a challenge to all scientists present here today to come up with recommendations that will ensure enhanced participation of our scientists in the IPCC process, and enhance involvement of Tanzanian scientists in climate change related research. This endeavor will in turn contribute to the next IPCC Assessment cycle (Sixth Assessment Report, AR6)’. Said Mr. Morisson Mlaki in his speech.
Dr. Agnes L. Kijazi, the Director General of Tanzania Meteorological Agency and Permanent Representative of the United Republic of Tanzania with the World Meteorological Organization (WMO) welcomed all workshop participants and thanked WMO for supporting the workshop through the GFCS programme. Dr. Kijazi said such workshop is of its kind and the first to be held in Tanzania where scientists and decision makers sat together under the same roof to discuss the findings and the implications of the latest IPCC report (AR5).
           
The Intergovernmental Panel on Climate Change (IPCC) is the leading international body for the assessment of climate change. It was established by the United Nations Environment Programme (UNEP) and the World Meteorological Organization (WMO) in 1988 to provide the world with a clear scientific view on the current state of knowledge in climate change and its potential environmental and socio-economic impacts. The workshop was attended by participant  from higher learning institutions  government ministries and NGO’s that included scientists and decision makers from Commission for science and Technology (COSTECH), Sokoine University of Agriculture (SUA), University of Dar es Salaam (UDSM), University of Dodoma (UDOM), Ardhi University (ARU) Vice President Office (Environment), Ministry of Agriculture and Food Security, Ministry of Health, Tanzania RedCross Society, World Food Programme(WFP), Centre for Weather Climate and Research (CWCAR) Climate Consult, National Environment Management Council (NEMC), Environment Protection and Management Services (EPMS), the Prime Minister – Disaster Management Department.

RELEASED BY: MONICA MUTONI; PUBLIC RELATION OFFICER, TANZANIA METEOROLOGICAL AGENCY

Featured Post

DKT. KIJAZI: KIWANGO CHA USAHIHI WA UTABIRI WA MSIMU WA VULI 2019 KIWE CHA JUU ZAIDI.

Mkurugenzi mkuu wa TMA na Makamu wa Tatu wa Rais wa Shirika la Hali ya Hewa Duniani Dkt. Agnes Kijazi (katikati mwenye suti nyeusi) waka...