Tuesday, September 30, 2014

TMA YAZINDUA JARIDA LA KLIMATOLOGIA LA TATHIMINI YA HALI YA HEWA KWA MWAKA 2011

Kaimu Mwenyekiti wa Bodi ya Ushauri Eng. James Ngeleja akizindua jarida la Klimatolojia la tathimin ya hali ya hewa kwa mwaka 2011, pembeni Dkt. Agnes Kijazi mkurugenzi mkuu wa TMA akifuatilia uzinduzi huo( mwenye guo nyekundu)

Mkurugenzi Mkuu wa TMA Dkt. Agnes Kijazi akiongea na vyombo vya habari juu ya umuhimu wa kuanzishwa kwa jarida hili
Kaimu Mkurugenzi wa Utafiti Dkt. Hashim Ng'ongolo akiwakaribisha wageni waalikwa katika uzinduzi wa  jarida la klimatolojia la tathimin ya hali ya hewa kwa mwaka 2011 uliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa TMA makao makuu 
Wajumbe wa Bodi ya Ushauri ya TMA katika picha ya pamoja mara baada ya uzinduzi wa  jarida la klimatolojia la tathimin ya hali ya hewa kwa mwaka 2011. TMA itaendelea kutoa matoleo mengine ya kuanzia mwaka 2012 mpaka 2014. Tolea la hivi sasa limepewa namba
ISSN 1821-9411

 


Monday, September 22, 2014

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI DR. CHARLES TIZEBA AFUNGUA MKUTANO WA WAKUU WA TAASIS ZA HALI YA HEWA KUTOKA NCHI ZA KUSINI MWA AFRIKA (SADC)

Naibu Waziri wa Uchukuzi Dkt. Charles Tizeba akihutubia wakuu wa taasis za hali ya hewa kutoka kusini mwa Afrika (SADC) katika mkutano wao uliofanyika mjini Arusha katika hoteli ya Palace.
Mkurugenzi Mkuu wa TMA Dkt. Agens Kijazi akimkaribisha mgeni rasmi ambaye ni Naibu Waziri wa Uchukuzi Dkt. Charles Tizeba kuhutubia wakuu wa taasisi za hali ya hewa Kusini mwa Afrika (SADC). Mkutano huu ulihudhuriwa na nchi wanachama wa SADC pamoja na ujumbe kutoka Shirika la Hali ya Hewa Duniani (WMO).
Naibu Waziri wa Uchukuzi Dkt. Charles Tizeba( wa tatu kutoka kushoto waliokaa), Mkurugenzi Mkuu wa TMA Dkt. Agnes Kijazi (wa pili kutoka kushoto walikaa) katika picha ya pamoja na washiriki wa mkutano wa wakuu wa taasisi za hali ya hewa kutoka nchi za Kusini mwa Afrika.

TRAINING WORKSHOP FOR FORECASTERS AND AGROMETEOROLOGIST ON USE OF NWP AND SATELLITE PRODUCTS FOR IMPROVEMENT OF WEATHER FORECASTS

Guest of Honour Acting Director General Mr. Ibrahim Nassib (fifth from right first line) on the group photo with  forecasters and agrometeorologist during a training workshop on use of NWP and satellite products for weather forecasts improvement.
Guest of Honour Acting Director General Mr. Ibrahim Nassib and Director of Forecasting Services Dr. Hamza Kabelwa (infront)  on an official opening of a training workshop on use of NWP and satellite products for weather forecasts improvement.

Tuesday, September 16, 2014

MKUU WA MKOA WA ARUSHA AAGIZA MAMLAKA ZA HALI YA HEWA KUSINI MWA AFRIKA KUSHIRIKIANA KATIKA KUTATUA CHANGAMOTO ZA HUDUMA ZA HALI YA HEWA KATIKA KANDA YA SADC.





Mgeni rasmi katika ufunguzi wa mkutano wa nane wa umoja wa taasis za hali ya hewa kusini mwa Afrika, Mkuu wa Wilaya ya Monduli Mhe. Jowika Kasunga (wan ne kutoka kushoto), Mkurugenzi Mkuu wa TMA ambaye pia ni mjumbe wa Bodi ya MASA na mwenyeji wa mkutano huo Dkt. Agnes Kijazi katika picha ya pamoja na washiriki wa mkutano huo.

Mamlaka ya Hali ya Hewa kwa niaba ya serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imekuwa mwenyeji wa mkutano wa kila mwaka wa umoja wa taasis za hali ya hewa katika nchi za Kusini mwa Afrika (MASA). Mkutano huo unafanyika mkoani Arusha. Akifungua mkutano huo kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Arusha mgeni rasmi ambaye ni mkuu wa Wilaya ya Monduli Mhe. Jowika W. Kasunga alizitaka taasis za hali ya hewa kusini mwa Afrika ikiwemo TMA kushirikiana katika kutatua changamoto zinazoikabili sekta ya hali ya hewa. ‘Wote tunakubaliana kwamba umoja ni nguvu, hivyo taasis za hali ya hewa zinapaswa kudumisha umoja na ushirikiano ili kukabiliana na changamoto zinazozikabili huduma za hali ya hewa kusini mwa Afrika’ alisema Mhe. Kasunga. 

Mkurugenzi wa Mamlaka ya Hali ya Hewa ya Malawi na Mwenyekiti wa umoja huo alisema, lengo kuu la mkutano huu ni kujaribu kutatua changamoto za taasis za hali ya hewa kusini mwa Afrika.

Kwa niaba ya TMA, Mkurugenzi Mkuu wa TMA Dkt. Agnes Kijazi aliwakaribisha wageni wote Arusha na kuwatakia majadiliano yenye mafanikio. Dkt Kijazi alisema ni matarajio yake kwamba mkutano huo utatoa mapendekezo yatakayoweza kuboresha huduma za hali ya hewa katika nchi za kusini mwa bara la Afrika.  
   
MASA ni umoja wa taasis zinazotoa huduma za hali ya hewa kusini mwa Afrika (SADC) wenye lengo la kuboresha huduma za hali ya hewa kwa nchi za ukanda wa kusini mwa Afrika. MASA ni umoja ulioanzishwa kisheria wenye katiba, mpango kazi na Bodi. Wajume wa Bodi ni wakuu wa taasis za hali ya hewa katika nchi za SADC ambapo nchi tano (5) ni wajumbe wa Bodi. Nchi hizo ni Malawi,Zimbabwe,Zambia, Afrika Kusini na Tanzania 

IMETOLEWA NA MONICA MUTONI - MAMLAKA YA HALI YA HEWA TANZANIA.

Thursday, September 4, 2014

MWELEKEO WA MVUA KWA KIPINDI CHA OKTOBA - DISEMBA 2014 NCHINI


Dondoo muhimu kwa ufupi:

Taarifa hii inatoa tathmini ya mvua za masika (Machi - Mei) 2014 na mwelekeo wa mifumo ya hali ya hewa na mvua kwa kipindi  cha mwezi Oktoba hadi Disemba, 2014(Vuli).


1. Mwelekeo wa mvua kwa kipindi cha Oktoba-Disemba, 2014 Vuli unaonyesha kuwa;
·        Hali ya mvua inatarajiwa kuwa ya  kuridhisha katika maeneo mengi ya       nchi hata hivyo mvua za wastani hadi chini ya wastani zinatarajiwa  katika baadhi ya maeneo ya kusini mwa nchi hususan mkoa wa Ruvuma.
·        Msimu huu mvua zinatarajiwa kuanza mapema mwezi Septemba katika maeneo ya ziwa Viktoria, nyanda za juu kaskazini mashariki na pwani ya kasikazini
 2. Athari na Ushauri
·        Mvua za kutosha zinatarajiwa kwa shughuli za  kilimo katika maeneo mengi ya nchi.
·        Vina vya maji katika mito na mabwawa vinatarajiwa kuongezeka katika maeneo mengi ya nchi.
·        Maji yatumike kwa uangalifu na kuzingatia taratibu za uvunaji, uhifadhi na matumizi endelevu ya rasilimali maji
·        Matukio ya migogoro inayosababishwa na mifugo, wanyamapori na shughuli za binadamu na kilimo hayatarajiwi kujitokeza kwa kiasi kikubwa.
·        Vipindi vya mvua kubwa vinaweza kuongeza matukio ya mafuriko na uharibifu wa mali na miundombinu.
·        Milipuko ya magonjwa yanayosababishwa  na kutuama kwa maji na utiririshaji wa majitaka usiodhibitiwa inaweza kujitokeza.
·        Hatua stahiki katika utunzaji wa mazingira, upatikanaji wa maji safi na salama, na usambazaji wa madawa, maji na chakula ikiwa ni hatua za kujiandaa na kukabiliana na majanga yanayoweza kutokea


Imetolewa na Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania





Featured Post

DKT. KIJAZI: KIWANGO CHA USAHIHI WA UTABIRI WA MSIMU WA VULI 2019 KIWE CHA JUU ZAIDI.

Mkurugenzi mkuu wa TMA na Makamu wa Tatu wa Rais wa Shirika la Hali ya Hewa Duniani Dkt. Agnes Kijazi (katikati mwenye suti nyeusi) waka...