Sunday, August 31, 2014

TMA YAKUTANA NA WADAU WA HALI YA HEWA KUTOKA SEKTA MBALIMBALI KUJADILI UTABIRI WA MSIMU WA MVUA ZA OKTOBA HADI DESEMBA 2014




Kaimu Mwenyekiti wa Bodi ya Ushauri ya TMA  Mhandisi James Ngeleja (aliyesimama) akielezea umuhimu wa mikutano ya wadau wa hali ya hewa kutoka sekta mbalimbali alipofungua rasmi mkutano wa wadau wa hali ya hewa kutoka sekta mbalimbali nchini kwa niaba ya mwenyeki wa bodi hiyo Ndugu Morrison Mlaki wenye kujadili utabiri wa msimu wa mvua za Oktoba hadi Desemba 2014.



Mkurugenzi Mkuu wa TMA Dkt. Agnes Kijazi akizungungumza na wadau wa hali ya hewa kutoka sekta mbalimbali nchini lengo la TMA kukutana na wadau hao wakati wa ufunguzi wa mkutano huo wa wadau wa hali ya hewa kutoka sekta mbalimbali



Baadhi ya wadau wa hali ya hewa kutoka sekta mbalimbali nchini wakifuatilia mada zilizokuwa zinatolewa na baadhi ya wajumbe



Kaimu Mwenyekiti wa Bodi ya Ushauri ya TMA  Mhandisi James Ngeleja (wa tano kutoka kulia mstari wa mbele), baadhi ya wajumbe wa Bodi hiyo pamoja na Mkurugenzi  Mkuu wa TMA Dkt Agnes KIjazi (wan ne kutoka kulia mstari wa mbele) katika picha ya pamoja na wadau wa hali ya hewa kutoka sekta mbalimbali zikiwemo kilimo, afya, maafa,media,mifugo,nishati, utalii n.k

Friday, August 22, 2014

WANANCHI WAFURAHISHWA NA UPATIKANAJI WA TAARIFA ZA HALI YA HEWA KWA WAVUVI, WAKULIMA,WAFUGAJI NA WASAFIRISHAJI KATIKA UKANDA WA ZIWA VICTORIA KUPITIA SIMU ZA MKONONI NA VYOMBO VYA HABARI VYA KIJAMII



Picha: Mwakilishi wa Waziri wa Uchukuzi Mhandisi Warioba Sanya (watatu kutoka kushoto), Mkurugenzi Mkuu TMA Dkt. Agnes Kijazi (wapili kutoka kushoto),Mwakilishi wa Katibu Mkuu WMO Bw. Samuel Muchemi (wa kwanza kushoto)  na mwenyekiti wa madiwani wilaya ya Sengerema Bw. Ibrahimu Kazungu kwenye picha ya pamoja na washiriki wa warsha inayohusu uboreshaji wa huduma za hali ya hewa katika maeneo ya Ziwa Victoria kwa sekta ya wakulima na wafugaji, wavuvi na wasafirishaji, yenye lengo la kupata mrejesho kutoka kwa jamii inayoishi Kanda ya Ziwa, kuanzia tarehe 18-20 Agosti 2014 katika hotel ya Gold Crest-Mwanza


Na. Monica Mutoni


Mamlaka ya Hali ya Hewa kwa kushirikiana na Shirika la Hali ya Hewa Duniani ilianzisha huduma ya kutoa taarifa za hali ya hewa hususan tahadhari kupitia simu za mkononi na vyombo vya habari vya kijamii kama redio, na magazeti. Huduma hiyo ilizinduliwa rasmi mwaka jana 17 Julai 2013 huko Sengerea mkoani Mwanza na Naibu Waziri wa Uchukuzi Dkt Charles Tizeba.
Katika kuhakikisha huduma hii inafanya kazi kwa ufanisi TMA pamoja na WMO wameandaa warsha inayohusu uboreshaji wa huduma za hali ya hewa katika maeneo ya Ziwa Victoria kwa sekta ya wakulima na wafugaji, wavuvi na wasafirishaji, yenye lengo la kupata mrejesho kutoka kwa jamii inayoishi Kanda ya Ziwa, kuanzia tarehe 18-20 Agosti 2014 katika hotel ya Gold Crest-Mwanza
Akiongea kwa niaba ya Waziri wa Uchukuzi Bw. Warioba ambaye ni Katibu Tawala Mkoa wa Mwanza alisema ‘ Huduma hii ni nzuri hasa ikizingatiwa ongezeko la matukio ya hali mbaya ya hewa katika maeneo ya Ziwa Victoria’ Vilevile aliishukuru WMO kwa kufadhili huduma hiyo na wananchi wa Wilaya ya Sengerema kuitumia vizuri huduma hii.
Nae Mkurugenzi Mkuu wa TMA Dkt Agnes Kijazi alisema ‘Katika kuhakikisha TMA inazidi kuziboresha huduma zake, wataalam wa TMA wameweza kutembelea maeneo mbalimbali ya Wilaya ya Sengerema ili kujua zaidi majanga yanayoikumbuka wilaya hiyo, hii itasaidia namna ya uandaaji wa taarifa zinazohitajika na wananchi, aliongezea ‘kwa kupitia mradi huu TMA imeweza kuorodhesha namba za simu za mkononi kwa wakazi zaidi ya 350, ambapo watu hawa hutumiwa utabiri wa hali ya hewa pamoja na tahadhari hivyo kuweza kutumia kwa shughuli zao na  kusambaziana, vilevile taarifa hizi hutumwa kwa wasimamizi wa mradi huu wilayani na vyombo mbalimbali vya habari’
Kwa upande wa WMO, mwakilishi kutoka WMO Bw. Samuel Muchemi alielezea kwa kiufupi nia ya mradi huo’aliipongeza TMA kwa umakini wake katika kutekeleza mradi huu, kwa kulinganisha na shukrani na shuhuda zilizotolewa na wavuvi, wakulima, wafugaji na na wasafirishaji.Aidha warsha itapitia rasimu ya mkataba wa makubaliano (MoU) na Kanuni za ufanyaji kazi (Standard Operating Procedures)
TMA kwa kushirikiana na wadau mbalimbali vikiwemo vyombo vya habari imejikita katika kuhakikisha jamii inapata taarifa za hali ya hewa kwa wakati hususan kipindi cha matukio makubwa yatokanayo na hali mbaya ya hewa kama vile tsunami,mvua kubwa, ukame, upepo mkali, mawimbi makubwa n.k hivyo kuisaidia jamii kujihadhari na madhara hayo.

IMETOLEWA NA MAMLAKA YA HALI YA HEWA TANZANIA.

Featured Post

DKT. KIJAZI: KIWANGO CHA USAHIHI WA UTABIRI WA MSIMU WA VULI 2019 KIWE CHA JUU ZAIDI.

Mkurugenzi mkuu wa TMA na Makamu wa Tatu wa Rais wa Shirika la Hali ya Hewa Duniani Dkt. Agnes Kijazi (katikati mwenye suti nyeusi) waka...